< Proverbs 28 >

1 The wicked flee when no man pursueth: but the righteous are bold as a lion.
Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza, bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
2 For the transgression of a land many are the princes thereof: but by men of understanding [and] knowledge the state [thereof] shall be prolonged.
Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi, bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.
3 A needy man that oppresseth the poor is [like] a sweeping rain which leaveth no food.
Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.
4 They that forsake the law praise the wicked: but such as keep the law contend with them.
Wale waiachao sheria huwasifu waovu, bali wale waishikao sheria huwapinga.
5 Evil men understand not judgment: but they that seek the LORD understand all things.
Watu wabaya hawaelewi haki, bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.
6 Better is the poor that walketh in his integrity, than he that is perverse in [his] ways, though he be rich.
Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.
7 Whoso keepeth the law is a wise son: but he that is a companion of gluttonous men shameth his father.
Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.
8 He that augmenteth his substance by usury and increase, gathereth it for him that hath pity on the poor.
Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno hukusanya kwa ajili ya mwingine, ambaye atawahurumia maskini.
9 He that turneth away his ear from hearing the law, even his prayer is an abomination.
Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
10 Whoso causeth the upright to go astray in an evil way, he shall fall himself into his own pit: but the perfect shall inherit good.
Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya, ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe, bali wasio na lawama watapokea urithi mwema.
11 The rich man is wise in his own conceit; but the poor that hath understanding searcheth him out.
Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.
12 When the righteous triumph, there is great glory: but when the wicked rise, men hide themselves.
Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa, bali waovu watawalapo, watu hujificha.
13 He that covereth his transgressions shall not prosper: but whoso confesseth and forsaketh them shall obtain mercy.
Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.
14 Happy is the man that feareth alway: but he that hardeneth his heart shall fall into mischief.
Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana, bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu huangukia kwenye taabu.
15 [As] a roaring lion, and a ranging bear; [so is] a wicked ruler over a poor people.
Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.
16 The prince that lacketh understanding is also a great oppressor: [but] he that hateth covetousness shall prolong his days.
Mtawala dhalimu hana akili, bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu atafurahia maisha marefu.
17 A man that is laden with the blood of any person shall flee unto the pit; let no man stay him.
Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua atakuwa mtoro mpaka kufa; mtu yeyote na asimsaidie.
18 Whoso walketh uprightly shall be delivered: but he that is perverse in [his] ways shall fall at once.
Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama hulindwa salama, bali yeye ambaye njia zake ni potovu ataanguka ghafula.
19 He that tilleth his land shall have plenty of bread: but he that followeth after vain [persons] shall have poverty enough.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.
20 A faithful man shall abound with blessings: but he that maketh haste to be rich shall not be unpunished.
Mtu mwaminifu atabarikiwa sana, bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka hataacha kuadhibiwa.
21 To have respect of persons is not good: neither that a man should transgress for a piece of bread.
Kuonyesha upendeleo si vizuri, hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.
22 He that hath an evil eye hasteth after riches, and knoweth not that want shall come upon him.
Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.
23 He that rebuketh a man shall afterward find more favour than he that flattereth with the tongue.
Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi, kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.
24 Whoso robbeth his father or his mother, and saith, It is no transgression; the same is the companion of a destroyer.
Yeye amwibiaye babaye au mamaye na kusema, “Si kosa,” yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.
25 He that is of a greedy spirit stirreth up strife: but he that putteth his trust in the LORD shall be made fat.
Mtu mwenye tamaa huchochea fitina, bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.
26 He that trusteth in his own heart is a fool: but whoso walketh wisely, he shall be delivered.
Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.
27 He that giveth unto the poor shall not lack: but he that hideth his eyes shall have many a curse.
Yeye ampaye maskini hatapungukiwa na kitu chochote, bali yeye awafumbiaye maskini macho hupata laana nyingi.
28 When the wicked rise, men hide themselves: but when they perish, the righteous increase.
Wakati waovu watawalapo, watu huenda mafichoni, bali waovu wanapoangamia, wenye haki hufanikiwa.

< Proverbs 28 >