< Proverbs 12 >

1 Whoso loveth correction loveth knowledge: but he that hateth reproof is brutish.
Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
2 A good man shall obtain favour of the LORD: but a man of wicked devices will he condemn.
Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
3 A man shall not be established by wickedness: but the root of the righteous shall never be moved.
Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
4 A virtuous woman is a crown to her husband: but she that maketh ashamed is as rottenness in his bones.
Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
5 The thoughts of the righteous are just: [but] the counsels of the wicked are deceit.
Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
6 The words of the wicked are of lying in wait for blood: but the mouth of the upright shall deliver them.
Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
7 The wicked are overthrown, and are not: but the house of the righteous shall stand.
Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
8 A man shall be commended according to his wisdom: but he that is of a perverse heart shall be despised.
Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
9 Better is he that is lightly esteemed, and hath a servant, than he that honoureth himself, and lacketh bread.
Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
10 A righteous man regardeth the life of his beast: but the tender mercies of the wicked are cruel.
Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
11 He that tilleth his land shall have plenty of bread: but he that followeth after vain [persons] is void of understanding.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
12 The wicked desireth the net of evil men: but the root of the righteous yieldeth [fruit].
Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
13 In the transgression of the lips is a snare to the evil man: but the righteous shall come out of trouble.
Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
14 A man shall be satisfied with good by the fruit of his mouth: and the doings of a man’s hands shall be rendered unto him.
Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
15 The way of the foolish is right in his own eyes: but he that is wise hearkeneth unto counsel.
Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
16 A fool’s vexation is presently known: but a prudent man concealeth shame.
Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
17 He that uttereth truth sheweth forth righteousness, but a false witness deceit.
Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
18 There is that speaketh rashly like the piercings of a sword: but the tongue of the wise is health.
Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
19 The lip of truth shall be established for ever: but a lying tongue is but for a moment.
Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
20 Deceit is in the heart of them that devise evil: but to the counsellors of peace is joy.
Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
21 There shall no mischief happen to the righteous: but the wicked shall be filled with evil.
Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
22 Lying lips are an abomination to the LORD: but they that deal truly are his delight.
Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
23 A prudent man concealeth knowledge: but the heart of fools proclaimeth foolishness.
Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
24 The hand of the diligent shall bear rule: but the slothful shall be put under taskwork.
Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
25 Heaviness in the heart of a man maketh it stoop; but a good word maketh it glad.
Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
26 The righteous is a guide to his neighbour: but the way of the wicked causeth them to err.
Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
27 The slothful man roasteth not that which he took in hunting: but the precious substance of men [is to] the diligent.
Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
28 In the way of righteousness is life; and in the pathway thereof there is no death.
Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

< Proverbs 12 >