< Obadiah 1 >

1 The vision of Obadiah. Thus saith the Lord GOD concerning Edom: We have heard tidings from the LORD, and an ambassador is sent among the nations, [saying], Arise ye, and let us rise up against her in battle.
Maono ya Obadia. Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi kuhusu Edomu: Tumesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Inukeni, twendeni tukapigane vita dhidi yake.”
2 Behold, I have made thee small among the nations: thou art greatly despised.
“Angalieni, nitawafanya wadogo miongoni mwa mataifa, mtadharauliwa kabisa.
3 The pride of thine heart hath deceived thee, O thou that dwellest in the clefts of the rock, whose habitation is high; that saith in his heart, Who shall bring me down to the ground?
Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba na kufanya makao yako juu, wewe unayejiambia mwenyewe, ‘Ni nani awezaye kunishusha chini?’
4 Though thou mount on high as the eagle, and though thy nest be set among the stars, I will bring thee down from thence, saith the LORD.
Ingawa unapaa juu kama tai na kufanya kiota chako kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
5 If thieves came to thee, if robbers by night, (how art thou cut off!) would they not steal till they had enough? if grapegatherers came to thee, would they not leave some gleaning grapes?
“Ikiwa wevi wangekuja kwako, ikiwa wanyangʼanyi wangekujia usiku: Lo! Tazama ni maafa kiasi gani yangekuwa yanakungojea: je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji? Kama wachuma zabibu wangekuja kwako, je, wasingebakiza zabibu chache?
6 How are [the things of] Esau searched out! how are his hidden treasures sought up!
Lakini tazama jinsi Esau atakavyotekwa, jinsi hazina zake zilizofichwa zitatekwa nyara!
7 All the men of thy confederacy have brought thee on thy way, even to the border: the men that were at peace with thee have deceived thee, and prevailed against thee; [they that eat] thy bread lay a snare under thee: there is none understanding in him.
Wote ulioungana nao watakufukuza hadi mpakani, rafiki zako watakudanganya na kukushinda, wale wanaokula mkate wako watakutegea mtego, lakini hutaweza kuugundua.
8 Shall I not in that day, saith the LORD, destroy the wise men out of Edom, and understanding out of the mount of Esau?
“Katika siku hiyo,” asema Bwana, “je, sitaangamiza watu wenye hekima wa Edomu, watu wenye ufahamu katika milima ya Esau?
9 And thy mighty men, O Teman, shall be dismayed, to the end that every one may be cut off from the mount of Esau by slaughter.
Ee Temani, mashujaa wako watatiwa hofu, kila mmoja katika milima ya Esau ataangushwa chini kwa kuchinjwa.
10 For the violence done to thy brother Jacob shame shall cover thee, and thou shalt be cut off for ever.
Kwa sababu ya jeuri uliyofanya dhidi ya ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika; utaangamizwa milele.
11 In the day that thou stoodest on the other side, in the day that strangers carried away his substance, and foreigners entered into his gates, and cast lots upon Jerusalem, even thou wast as one of them.
Siku ile ulisimama mbali ukiangalia wakati wageni walipojichukulia utajiri wake na watu wa nchi nyingine walipoingia malango yake wakipiga kura kwa ajili ya Yerusalemu, ulikuwa kama mmoja wao.
12 But look not thou on the day of thy brother in the day of his disaster, and rejoice not over the children of Judah in the day of their destruction; neither speak proudly in the day of distress.
Usingemdharau ndugu yako katika siku ya msiba wake, wala kufurahia juu ya watu wa Yuda katika siku ya maangamizi yao, wala kujigamba sana katika siku ya taabu yao.
13 Enter not into the gate of my people in the day of their calamity; yea, look not thou on their affliction in the day of their calamity, neither lay ye [hands] on their substance in the day of their calamity.
Usingeingia katika malango ya watu wangu katika siku ya maafa yao, wala kuwadharau katika janga lao katika siku ya maafa yao, wala kunyangʼanya mali zao katika siku ya maafa yao.
14 And stand thou not in the crossway, to cut off those of his that escape; and deliver not up those of his that remain in the day of distress.
Usingengoja kwenye njia panda na kuwaua wakimbizi wao, wala kuwatoa watu wake waliosalia katika siku ya shida yao.
15 For the day of the LORD is near upon all the nations: as thou hast done, it shall be done unto thee; thy dealing shall return upon thine own head.
“Siku ya Bwana iko karibu kwa mataifa yote. Kama ulivyofanya, nawe utafanyiwa vivyo hivyo, matendo yako yatakurudia juu ya kichwa chako.
16 For as ye have drunk upon my holy mountain, so shall all the nations drink continually, yea, they shall drink, and swallow down, and shall be as though they had not been.
Kama vile ulivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, vivyo hivyo mataifa yote watakunywa mfululizo, watakunywa na kunywa, nao watatoweka kana kwamba hawajawahi kuwepo.
17 But in mount Zion there shall be those that escape, and it shall be holy; and the house of Jacob shall possess their possessions.
Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwepo na wale watakaookoka; nao utakuwa mtakatifu, nayo nyumba ya Yakobo itamiliki urithi wake.
18 And the house of Jacob shall be a fire, and the house of Joseph a flame, and the house of Esau for stubble, and they shall burn among them, and devour them: and there shall not be any remaining to the house of Esau; for the LORD hath spoken it.
Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto; nayo nyumba ya Esau itakuwa bua kavu, nao wataiwasha moto na kuiteketeza. Hakutakuwa na watakaosalimika kutoka nyumba ya Esau.” Bwana amesema.
19 And they of the South shall possess the mount of Esau; and they of the lowland the Philistines and they shall possess the field of Ephraim, and the field of Samaria: and Benjamin [shall possess] Gilead.
Watu kutoka nchi ya Negebu wataikalia milima ya Esau, na watu kutoka miteremko ya vilima watamiliki nchi ya Wafilisti. Watayakalia mashamba ya Efraimu na Samaria, naye Benyamini atamiliki Gileadi.
20 And the captivity of this host of the children of Israel, which are [among] the Canaanites, [shall possess] even unto Zarephath; and the captivity of Jerusalem, which is in Sepharad, shall possess the cities of the South.
Kundi la Waisraeli walioko uhamishoni Kanaani watarudi na kumiliki nchi mpaka Sarepta. Walioko uhamishoni Sefaradi kutoka Yerusalemu watamiliki miji ya Negebu.
21 And saviours shall come up on mount Zion to judge the mount of Esau; and the kingdom shall be the LORD’S.
Waokoaji watakwea juu ya Mlima Sayuni kutawala milima ya Esau. Nao ufalme utakuwa wa Bwana.

< Obadiah 1 >