< Numbers 29 >

1 And in the seventh month, on the first day of the month, ye shall have an holy convocation; ye shall do no servile work: it is a day of blowing of trumpets unto you.
“‘Katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu na msifanye kazi ya kawaida. Ni siku kwa ajili yenu ya kupiga tarumbeta.
2 And ye shall offer a burnt offering for a sweet savour unto the LORD; one young bullock, one ram, seven he-lambs of the first year without blemish:
Mtatayarisha sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri impendezayo Bwana ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
3 and their meal offering, fine flour mingled with oil, three tenth parts for the bullock, two tenth parts for the ram,
Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume, andaa unga sehemu ya kumi mbili za efa;
4 and one tenth part for every lamb of the seven lambs:
na pamoja na wana-kondoo saba kila mmoja aandaliwe na sehemu ya kumi ya efa ya unga.
5 and one he-goat for a sin offering, to make atonement for you:
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
6 beside the burnt offering of the new moon, and the meal offering thereof, and the continual burnt offering and the meal offering thereof, and their drink offerings, according unto their ordinance, for a sweet savour, an offering made by fire unto the LORD.
Hivi ni nyongeza ya sadaka za kuteketezwa kila mwezi na kila siku pamoja na sadaka zake za nafaka na sadaka za vinywaji kama ilivyoainishwa. Ni sadaka zinazotolewa kwa Bwana kwa moto, harufu inayopendeza.
7 And on the tenth day of this seventh month ye shall have an holy convocation; and ye shall afflict your souls; ye shall do no manner of work:
“‘Kwenye siku ya kumi ya mwezi huu wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Mtajikana wenyewe na msifanye kazi.
8 but ye shall offer a burnt offering unto the LORD for a sweet savour; one young bullock, one ram, seven he-lambs of the first year; they shall be unto you without blemish:
Toeni sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
9 and their meal offering, fine flour mingled with oil, three tenth parts for the bullock, two tenth parts for the one ram,
Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
10 a several tenth part for every lamb of the seven lambs:
na kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba andaa sehemu ya kumi ya unga laini kwa kila mmoja.
11 one he-goat for a sin offering; beside the sin offering of atonement, and the continual burnt offering, and the meal offering thereof, and their drink offerings.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho, na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, na sadaka zake za vinywaji.
12 And on the fifteenth day of the seventh month ye shall have an holy convocation; ye shall do no servile work, and ye shall keep a feast unto the LORD seven days:
“‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu, na hamtafanya kazi za kawaida. Adhimisheni sikukuu kwa Bwana kwa siku saba.
13 and ye shall offer a burnt offering, an offering made by fire, of a sweet savour unto the LORD; thirteen young bullocks, two rams, fourteen he-lambs of the first year; they shall be without blemish:
Toeni sadaka ya kuteketezwa mafahali wachanga kumi na watatu, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
14 and their meal offering, fine flour mingled with oil, three tenth parts for every bullock of the thirteen bullocks, two tenth parts for each ram of the two rams,
Pamoja na hao mafahali kumi na watatu, kila mmoja aandaliwe na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume wawili, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
15 and a several tenth part for every lamb of the fourteen lambs:
na kwa wana-kondoo kumi na wanne, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi ya efa ya unga laini.
16 and one he-goat for a sin offering; beside the continual burnt offering, the meal offering thereof, and the drink offering thereof.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka ya vinywaji.
17 And on the second day [ye shall offer] twelve young bullocks, two rams, fourteen he-lambs of the first year without blemish:
“‘Katika siku ya pili andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
18 and their meal offering and their drink offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the ordinance:
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
19 and one he-goat for a sin offering; beside the continual burnt offering, and the meal offering thereof, and their drink offerings.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
20 And on the third day eleven bullocks, two rams, fourteen he-lambs of the first year without blemish;
“‘Katika siku ya tatu andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
21 and their meal offering and their drink offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the ordinance:
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
22 and one he-goat for a sin offering; beside the continual burnt offering, and the meal offering thereof, and the drink offering thereof.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
23 And on the fourth day ten bullocks, two rams, fourteen he-lambs of the first year without blemish:
“‘Katika siku ya nne andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
24 their meal offering and their drink offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the ordinance:
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
25 and one he-goat for a sin offering; beside the continual burnt offering, the meal offering thereof, and the drink offering thereof.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
26 And on the fifth day nine bullocks, two rams, fourteen he-lambs of the first year without blemish:
“‘Katika siku ya tano andaeni mafahali tisa, kondoo dume wawili na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
27 and their meal offering and their drink offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the ordinance:
Pamoja na mafahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za kinywaji kulingana na idadi iliyoainishwa.
28 and one he-goat for a sin offering; beside the continual burnt offering, and the meal offering thereof, and the drink offering thereof.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
29 And on the sixth day eight bullocks, two rams, fourteen he-lambs of the first year without blemish:
“‘Katika siku ya sita andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
30 and their meal offering and their drink offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the ordinance:
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
31 and one he-goat for a sin offering; beside the continual burnt offering, the meal offering thereof, and the drink offerings thereof.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
32 And on the seventh day seven bullocks, two rams, fourteen he-lambs of the first year without blemish:
“‘Katika siku ya saba andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
33 and their meal offering and their drink offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the ordinance:
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
34 and one he-goat for a sin offering; beside the continual burnt offering, the meal offering thereof, and the drink offering thereof.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
35 On the eighth day ye shall have a solemn assembly: ye shall do no servile work:
“‘Katika siku ya nane mtakuwa na kusanyiko, na msifanye kazi ya kawaida.
36 but ye shall offer a burnt offering, an offering made by fire, of a sweet savour unto the LORD: one bullock, one ram, seven he-lambs of the first year without blemish:
Toeni sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
37 their meal offering and their drink offerings for the bullock, for the ram, and for the lambs, shall be according to their number, after the ordinance:
Pamoja na fahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka, na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
38 and one he-goat for a sin offering; beside the continual burnt offering, and the meal offering thereof, and the drink offering thereof.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
39 These ye shall offer unto the LORD in your set feasts, beside your vows, and your freewill offerings, for your burnt offerings, and for your meal offerings, and for your drink offerings, and for your peace offerings.
“‘Zaidi ya kile unachoweka nadhiri na sadaka zenu za hiari, andaeni hizi kwa ajili ya Bwana kwenye sikukuu zenu zilizoamriwa: sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za nafaka, sadaka za vinywaji, pamoja na sadaka zenu za amani.’”
40 And Moses told the children of Israel according to all that the LORD commanded Moses.
Mose akawaambia Waisraeli yale yote Bwana alimwagiza.

< Numbers 29 >