< Numbers 14 >

1 And all the congregation lifted up their voice, and cried; and the people wept that night.
Usiku ule watu wote wa jumuiya walipaza sauti zao na kulia kwa sauti kuu.
2 And all the children of Israel murmured against Moses and against Aaron: and the whole congregation said unto them, Would God that we had died in the land of Egypt! or would God we had died in this wilderness!
Waisraeli wote wakanungʼunika dhidi ya Mose na Aroni, nalo kusanyiko lote wakawaambia, “Laiti tungekuwa tumefia humo nchi ya Misri! Au humu kwenye hili jangwa!
3 And wherefore doth the LORD bring us unto this land, to fall by the sword? Our wives and our little ones shall be a prey: were it not better for us to return into Egypt?
Kwa nini Bwana anatuleta katika nchi hii ili tufe kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watachukuliwa kama nyara. Je, isingekuwa bora kwetu kurudi Misri?”
4 And they said one to another, Let us make a captain, and let us return into Egypt.
Wakasemezana wao kwa wao, “Inatupasa kumchagua kiongozi na kurudi Misri.”
5 Then Moses and Aaron fell on their faces before all the assembly of the congregation of the children of Israel.
Ndipo Mose na Aroni wakaanguka kifudifudi mbele ya kusanyiko lote la Kiisraeli lililokusanyika hapo.
6 And Joshua the son of Nun and Caleb the son of Jephunneh, which were of them that spied out the land, rent their clothes:
Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwa watu wale waliokwenda kuipeleleza nchi, wakararua nguo zao,
7 and they spake unto all the congregation of the children of Israel, saying, The land, which we passed through to spy it out, is an exceeding good land.
wakasema na kusanyiko lote la Kiisraeli, wakawaambia, “Nchi tuliyopita katikati yake na kuipeleleza ni nzuri sana sana.
8 If the LORD delight in us, then he will bring us into this land, and give it unto us; a land which floweth with milk and honey.
Ikiwa Bwana anapendezwa nasi, atatuongoza kuingia katika nchi ile, nchi itiririkayo maziwa na asali, naye atatupa nchi hiyo.
9 Only rebel not against the LORD, neither fear ye the people of the land; for they are bread for us: their defence is removed from over them, and the LORD is with us: fear them not.
Ila tu msimwasi Bwana. Wala msiwaogope watu wa nchi hiyo, kwa sababu tutawameza. Ulinzi wao umeondoka, lakini Bwana yupo pamoja nasi. Msiwaogope.”
10 But all the congregation bade stone them with stones. And the glory of the LORD appeared in the tent of meeting unto all the children of Israel.
Lakini kusanyiko lote likazungumza juu ya kuwapiga kwa mawe. Ndipo utukufu wa Bwana ukaonekana katika Hema la Kukutania kwa Waisraeli wote.
11 And the LORD said unto Moses, How long will this people despise me? and how long will they not believe in me, for all the signs which I have wrought among them?
Bwana akamwambia Mose, “Watu hawa watanidharau mpaka lini? Wataendelea kukataa kuniamini mimi mpaka lini, ingawa nimetenda ishara za miujiza miongoni mwao?
12 I will smite them with the pestilence, and disinherit them, and will make of thee a nation greater and mightier than they.
Nitawapiga kwa tauni na kuwaangamiza, lakini nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa lenye nguvu kuliko wao.”
13 And Moses said unto the LORD, Then the Egyptians shall hear it; for thou broughtest up this people in thy might from among them;
Mose akamwambia Bwana, “Ndipo Wamisri watasikia juu ya jambo hili! Kwa uweza wako uliwapandisha watu hawa kutoka miongoni mwao.
14 and they will tell it to the inhabitants of this land: they have heard that thou LORD art in the midst of this people; for thou LORD art seen face to face, and thy cloud standeth over them, and thou goest before them, in a pillar of cloud by day, and in a pillar of fire by night.
Nao watawaambia wenyeji wa nchi hii jambo hili. Wao tayari wameshasikia kwamba wewe, Ee Bwana, upo pamoja na watu hawa, na kuwa wewe, Ee Bwana, umeonekana uso kwa uso, nalo wingu lako hukaa juu yao. Tena wewe unawatangulia kwa nguzo ya wingu mchana na kwa nguzo ya moto usiku.
15 Now if thou shalt kill this people as one man, then the nations which have heard the fame of thee will speak, saying,
Ikiwa utawaua watu hawa wote mara moja, mataifa ambayo yamesikia taarifa hii kukuhusu wewe watasema,
16 Because the LORD was not able to bring this people into the land which he sware unto them, therefore he hath slain them in the wilderness.
‘Bwana alishindwa kuwaingiza watu hawa katika nchi aliyowaahidi kwa kiapo; hivyo akawaua jangwani.’
17 And now, I pray thee, let the power of the Lord be great, according as thou hast spoken, saying,
“Basi sasa nguvu za Bwana na zionekane, sawasawa na vile ulivyosema:
18 The LORD is slow to anger, and plenteous in mercy, forgiving iniquity and transgression, and that will by no means clear [the guilty]; visiting the iniquity of the fathers upon the children, upon the third and upon the fourth generation.
‘Bwana si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo na mwenye kusamehe dhambi na uasi. Lakini haachi kumwadhibu mwenye hatia, huadhibu watoto kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata kizazi cha tatu na cha nne.’
19 Pardon, I pray thee, the iniquity of this people according unto the greatness of thy mercy, and according as thou hast forgiven this people, from Egypt even until now.
Kwa kadiri ya upendo wako mkuu, usamehe dhambi ya watu hawa, kama vile ulivyowasamehe tangu wakati walitoka Misri mpaka sasa.”
20 And the LORD said, I have pardoned according to thy word:
Bwana akajibu, “Nimewasamehe kama ulivyoomba.
21 but in very deed, as I live, and as all the earth shall be filled with the glory of the LORD;
Hata hivyo, kwa hakika kama niishivyo, na kwa hakika kama utukufu wa Bwana uijazavyo dunia yote,
22 because all those men which have seen my glory, and my signs, which I wrought in Egypt and in the wilderness, yet have tempted me these ten times, and have not hearkened to my voice;
hakuna hata mmoja wa watu hawa ambao waliuona utukufu wangu na ishara za miujiza niliyotenda huko Misri na huko jangwani, lakini ambaye hakunitii na akanijaribu mara hizi kumi,
23 surely they shall not see the land which I sware unto their fathers, neither shall any of them that despised me see it:
hakuna hata mmoja wao atakayeona nchi niliyowaahidi baba zao kwa kiapo. Hakuna hata mmoja ambaye amenidharau atakayeiona.
24 but my servant Caleb, because he had another spirit with him, and hath followed me fully, him will I bring into the land whereinto he went; and his seed shall possess it.
Lakini kwa sababu mtumishi wangu Kalebu ana roho ya tofauti na ananifuata kwa moyo wote, nitamwingiza katika nchi aliyoiendea, nao wazao wake watairithi.
25 Now the Amalekite and the Canaanite dwell in the valley: tomorrow turn ye, and get you into the wilderness by the way to the Red Sea.
Kwa kuwa Waamaleki na Wakanaani wanaishi katika mabonde, kesho geukeni mwelekee jangwani kwa kufuata njia iendayo Bahari ya Shamu.”
26 And the LORD spake unto Moses and unto Aaron, saying,
Bwana akamwambia Mose na Aroni:
27 How long [shall I bear] with this evil congregation, which murmur against me? I have heard the murmurings of the children of Israel, which they murmur against me.
“Jumuiya hii ovu itanungʼunika dhidi yangu hadi lini? Nimesikia malalamiko ya hawa Waisraeli wanaonungʼunika.
28 Say unto them, As I live, saith the LORD, surely as ye have spoken in mine ears, so will I do to you:
Hivyo waambie, ‘Hakika kama niishivyo, asema Bwana, nitawafanyia vitu vilevile nilivyosikia mkisema:
29 your carcases shall fall in this wilderness; and all that were numbered of you, according to your whole number, from twenty years old and upward, which have murmured against me,
Kila mmoja wenu mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi ambaye alihesabiwa na amenungʼunika dhidi yangu, miili yenu itaanguka katika jangwa hili.
30 surely ye shall not come into the land, concerning which I lifted up my hand that I would make you dwell therein, save Caleb the son of Jephunneh, and Joshua the son of Nun.
Hakuna hata mmoja wenu atakayeingia katika nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kuwa makao yenu, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.
31 But your little ones, which ye said should be a prey, them will I bring in, and they shall know the land which ye have rejected.
Lakini watoto wenu ambao mlisema watachukuliwa kama mateka, nitawaingiza humo ili waifurahie nchi ambayo ninyi mmeikataa.
32 But as for you, your carcases shall fall in this wilderness.
Lakini ninyi, miili yenu itaanguka katika jangwa hili.
33 And your children shall be wanderers in the wilderness forty years, and shall bear your whoredoms, until your carcases be consumed in the wilderness.
Watoto wenu watakuwa wachungaji wa mifugo hapa kwa miaka arobaini, wakiteseka kwa ajili ya kukosa uaminifu kwenu, hadi mwili wa mtu wenu wa mwisho ulale katika jangwa hili.
34 After the number of the days in which ye spied out the land, even forty days, for every day a year, shall ye bear your iniquities, even forty years, and ye shall know my alienation.
Kwa miaka arobaini, mwaka mmoja kwa kila siku katika zile siku arobaini mlizoipeleleza nchi, mtateseka kwa ajili ya dhambi zenu, na kujua jinsi ilivyo vibaya kunifanya mimi kuwa adui yenu.’
35 I the LORD have spoken, surely this will I do unto all this evil congregation, that are gathered together against me: in this wilderness they shall be consumed, and there they shall die.
Mimi Bwana nimesema, na hakika nitafanya mambo haya kwa jumuiya hii yote ovu, ambayo imefungamana pamoja dhidi yangu. Watakutana na mwisho wao katika jangwa hili; hapa ndipo watafia.”
36 And the men, which Moses sent to spy out the land, who returned, and made all the congregation to murmur against him, by bringing up an evil report against the land,
Hivyo watu wale ambao Mose alikuwa amewatuma kuipeleleza nchi, waliorudi na kuifanya jumuiya nzima kunungʼunika dhidi ya Mose kwa kueneza taarifa mbaya kuhusu hiyo nchi:
37 even those men that did bring up an evil report of the land, died by the plague before the LORD.
watu hawa waliohusika kueneza taarifa mbaya kuhusu hiyo nchi walipigwa na kuanguka kwa tauni mbele za Bwana.
38 But Joshua the son of Nun, and Caleb the son of Jephunneh, remained alive of those men that went to spy out the land.
Miongoni mwa watu waliokwenda kuipeleleza hiyo nchi, ni Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune peke yao waliosalia.
39 And Moses told these words unto all the children of Israel: and the people mourned greatly.
Mose alipotoa taarifa hii kwa Waisraeli wote, waliomboleza kwa uchungu.
40 And they rose up early in the morning, and gat them up to the top of the mountain, saying, Lo, we be here, and will go up unto the place which the LORD hath promised: for we have sinned.
Mapema asubuhi siku iliyofuata walipanda juu kuelekea kwenye nchi ya vilima virefu, wakasema, “Tumetenda dhambi. Tutakwea mpaka mahali Bwana alipotuahidi.”
41 And Moses said, Wherefore now do ye transgress the commandment of the LORD, seeing it shall not prosper?
Lakini Mose akasema, “Kwa nini hamtii amri ya Bwana? Jambo hili halitafanikiwa!
42 Go not up, for the LORD is not among you; that ye be not smitten down before your enemies.
Msipande juu, kwa kuwa Bwana hayupo pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu,
43 For there the Amalekite and the Canaanite are before you, and ye shall fall by the sword: because ye are turned back from following the LORD, therefore the LORD will not be with you.
kwa kuwa Waamaleki na Wakanaani watapambana nanyi huko. Kwa sababu mmemwacha Bwana, hatakuwa pamoja nanyi, ninyi mtaanguka kwa upanga.”
44 But they presumed to go up to the top of the mountain: nevertheless the ark of the covenant of the LORD, and Moses, departed not out of the camp.
Hata hivyo, kwa kiburi chao walipanda juu kuelekea nchi ya vilima virefu, ijapokuwa Mose hakutoka kambini wala Sanduku la Agano la Bwana.
45 Then the Amalekite came down, and the Canaanite which dwelt in that mountain, and smote them and beat them down, even unto Hormah.
Ndipo Waamaleki na Wakanaani walioishi katika hiyo nchi ya vilima wakateremka na kuwashambulia, wakawapiga njia yote hadi Horma.

< Numbers 14 >