< Numbers 10 >

1 And the LORD spake unto Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose:
2 Make thee two trumpets of silver; of beaten work shalt thou make them: and thou shalt use them for the calling of the congregation, and for the journeying of the camps.
“Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
3 And when they shall blow with them, all the congregation shall gather themselves unto thee at the door of the tent of meeting.
Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
4 And if they blow but with one, then the princes, the heads of the thousands of Israel, shall gather themselves unto thee.
Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
5 And when ye blow an alarm, the camps that lie on the east side shall take their journey.
Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
6 And when ye blow an alarm the second time, the camps that lie on the south side shall take their journey: they shall blow an alarm for their journeys.
Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
7 But when the assembly is to be gathered together, ye shall blow, but ye shall not sound an alarm.
Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
8 And the sons of Aaron, the priests, shall blow with the trumpets; and they shall be to you for a statute for ever throughout your generations.
“Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
9 And when ye go to war in your land against the adversary that oppresseth you, then ye shall sound an alarm with the trumpets; and ye shall be remembered before the LORD your God, and ye shall be saved from your enemies.
Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
10 Also in the day of your gladness, and in your set feasts, and in the beginnings of your months, ye shall blow with the trumpets over your burnt offerings, and over the sacrifices of your peace offerings; and they shall be to you for a memorial before your God: I am the LORD your God.
Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
11 And it came to pass in the second year, in the second month, on the twentieth day of the month, that the cloud was taken up from over the tabernacle of the testimony.
Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
12 And the children of Israel set forward according to their journeys out of the wilderness of Sinai; and the cloud abode in the wilderness of Paran.
Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
13 And they first took their journey according to the commandment of the LORD by the hand of Moses.
Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
14 And in the first [place] the standard of the camp of the children of Judah set forward according to their hosts: and over his host was Nahshon the son of Amminadab.
Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
15 And over the host of the tribe of the children of Issachar was Nethanel the son of Zuar.
Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
16 And over the host of the tribe of the children of Zebulun was Eliab the son of Helon.
naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
17 And the tabernacle was taken down; and the sons of Gershon and the sons of Merari, who bare the tabernacle, set forward.
Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
18 And the standard of the camp of Reuben set forward according to their hosts: and over his host was Elizur the son of Shedeur.
Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
19 And over the host of the tribe of the children of Simeon was Shelumiel the son of Zurishaddai.
Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
20 And over the host of the tribe of the children of Gad was Eliasaph the son of Deuel.
naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
21 And the Kohathites set forward, bearing the sanctuary: and [the other] did set up the tabernacle against they came.
Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
22 And the standard of the camp of the children of Ephraim set forward according to their hosts: and over his host was Elishama the son of Ammihud.
Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
23 And over the host of the tribe of the children of Manasseh was Gamaliel the son of Pedahzur.
Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
24 And over the host of the tribe of the children of Benjamin was Abidan the son of Gideoni.
naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
25 And the standard of the camp of the children of Dan, which was the rearward of all the camps, set forward according to their hosts: and over his host was Ahiezer the son of Ammishaddai.
Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
26 And over the host of the tribe of the children of Asher was Pagiel the son of Ochran.
Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
27 And over the host of the tribe of the children of Naphtali was Ahira the son of Enan.
naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
28 Thus were the journeyings of the children of Israel according to their hosts; and they set forward.
Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
29 And Moses said unto Hobab, the son of Reuel the Midianite, Moses’ father in law, We are journeying unto the place of which the LORD said, I will give it you: come thou with us, and we will do thee good: for the LORD hath spoken good concerning Israel.
Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
30 And he said unto him, I will not go; but I will depart to mine own land, and to my kindred.
Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
31 And he said, Leave us not, I pray thee; forasmuch as thou knowest how we are to encamp in the wilderness, and thou shalt be to us instead of eyes.
Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
32 And it shall be, if thou go with us, yea, it shall be, that what good soever the LORD shall do unto us, the same will we do unto thee.
Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
33 And they set forward from the mount of the LORD three days’ journey; and the ark of the covenant of the LORD went before them three days’ journey, to seek out a resting place for them.
Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
34 And the cloud of the LORD was over them by day, when they set forward from the camp.
Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
35 And it came to pass, when the ark set forward, that Moses said, Rise up, O LORD, and let thine enemies be scattered; and let them that hate thee flee before thee.
Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
36 And when it rested, he said, Return, O LORD, unto the ten thousands of the thousands of Israel.
Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”

< Numbers 10 >