< Leviticus 1 >

1 And the LORD called unto Moses, and spake unto him out of the tent of meeting, saying,
Bwana akamwita Mose na kusema naye kutoka kwenye Hema la Kukutania, akamwambia,
2 Speak unto the children of Israel, and say unto them, When any man of you offereth an oblation unto the LORD, ye shall offer your oblation of the cattle, [even] of the herd and of the flock.
“Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Yeyote miongoni mwenu aletapo sadaka ya mnyama kwa Bwana, alete mnyama kama sadaka yake kutoka kundi lake la ngʼombe au la kondoo na mbuzi.
3 If his oblation be a burnt offering of the herd, he shall offer it a male without blemish: he shall offer it at the door of the tent of meeting, that he may be accepted before the LORD.
“‘Kama sadaka hiyo ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la ngʼombe, atamtoa ngʼombe dume asiye na dosari. Ni lazima amlete kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili aweze kukubalika kwa Bwana.
4 And he shall lay his hand upon the head of the burnt offering; and it shall be accepted for him to make atonement for him.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya kuteketezwa, nayo itakubaliwa kwa niaba yake ili kufanya upatanisho kwa ajili yake.
5 And he shall kill the bullock before the LORD: and Aaron’s sons, the priests, shall present the blood, and sprinkle the blood round about upon the altar that is at the door of the tent of meeting.
Atamchinja yule fahali mchanga mbele za Bwana, kisha wana wa Aroni walio makuhani wataleta damu na kuinyunyiza pande zote za madhabahu yaliyo penye ingilio la Hema la Kukutania.
6 And he shall flay the burnt offering, and cut it into its pieces.
Ataichuna hiyo sadaka ya kuteketezwa na kuikata vipande vipande.
7 And the sons of Aaron the priest shall put fire upon the altar, and lay wood in order upon the fire:
Wana wa Aroni kuhani wataweka moto juu ya madhabahu na kupanga kuni juu ya huo moto.
8 and Aaron’s sons, the priests, shall lay the pieces, the head, and the fat, in order upon the wood that is on the fire which is upon the altar:
Kisha wana wa Aroni walio makuhani watapanga vile vipande vya nyama, pamoja na kichwa na mafuta ya huyo mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
9 but its inwards and its legs shall he wash with water: and the priest shall burn the whole on the altar, for a burnt offering, an offering made by fire, of a sweet savour unto the LORD.
Ataziosha sehemu za ndani na miguu yake kwa maji, naye kuhani atavichoma vyote juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, yenye harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
10 And if his oblation be of the flock, of the sheep, or of the goats, for a burnt offering; he shall offer it a male without blemish.
“‘Kama sadaka ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la kondoo au mbuzi, atamtoa mnyama dume asiye na dosari.
11 And he shall kill it on the side of the altar northward before the LORD: and Aaron’s sons, the priests, shall sprinkle its blood upon the altar round about.
Atamchinjia upande wa kaskazini wa madhabahu mbele za Bwana, nao wana wa Aroni walio makuhani watanyunyizia damu yake pande zote za madhabahu.
12 And he shall cut it into its pieces, with its head and its fat: and the priest shall lay them in order on the wood that is on the fire which is upon the altar:
Atamkata vipande vipande, naye kuhani atavipanga, pamoja na kichwa na mafuta ya mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
13 but the inwards and the legs shall he wash with water: and the priest shall offer the whole, and burn it upon the altar: it is a burnt offering, an offering made by fire, of a sweet savour unto the LORD.
Ataosha sehemu za ndani na miguu kwa maji, naye kuhani atavileta vyote na kuvichoma juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
14 And if his oblation to the LORD be a burnt offering of fowls, then he shall offer his oblation of turtledoves, or of young pigeons.
“‘Kama sadaka ya kuteketezwa inayotolewa kwa Bwana ni ndege, atamtoa hua au kinda la njiwa.
15 And the priest shall bring it unto the altar, and wring off its head, and burn it on the altar; and the blood thereof shall be drained out on the side of the altar:
Kuhani atamleta kwenye madhabahu, naye atamvunja shingo na kumnyofoa kichwa na kumchoma juu ya madhabahu. Damu yake itachuruzishwa ubavuni mwa madhabahu.
16 and he shall take away its crop with the filth thereof, and cast it beside the altar on the east part, in the place of the ashes:
Ataondoa kifuko cha chakula pamoja na uchafu wake na kuvitupa upande wa mashariki wa madhabahu, mahali pale penye majivu.
17 and he shall rend it by the wings thereof, [but] shall not divide it asunder: and the priest shall burn it upon the altar, upon the wood that is upon the fire: it is a burnt offering, an offering made by fire, of a sweet savour unto the LORD.
Atampasua na kumweka wazi katika mabawa yake, lakini asimwachanishe kabisa, kisha kuhani ataichoma juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.

< Leviticus 1 >