< Leviticus 11 >

1 And the LORD spake unto Moses and to Aaron, saying unto them,
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
2 Speak unto the children of Israel, saying, These are the living things which ye shall eat among all the beasts that are on the earth.
“Waambieni Waisraeli: ‘Kati ya wanyama wote waishio juu ya nchi, hawa ndio mtakaowala:
3 Whatsoever parteth the hoof, and is clovenfooted, [and] cheweth the cud, among the beasts, that shall ye eat.
Mwaweza kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua.
4 Nevertheless these shall ye not eat of them that chew the cud, or of them that part the hoof: the camel, because he cheweth the cud but parteth not the hoof, he is unclean unto you.
“‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.
5 And the coney, because he cheweth the cud but parteth not the hoof, he is unclean unto you.
Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
6 And the hare, because she cheweth the cud but parteth not the hoof, she is unclean unto you.
Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
7 And the swine, because he parteth the hoof, and is clovenfooted, but cheweth not the cud, he is unclean unto you.
Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.
8 Of their flesh ye shall not eat, and their carcases ye shall not touch; they are unclean unto you.
Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.
9 These shall ye eat of all that are in the waters: whatsoever hath fins and scales in the waters, in the seas, and in the rivers, them shall ye eat.
“‘Kuhusu viumbe wote wanaoishi ndani ya maji ya bahari na vijito, mtakula wale wote wenye mapezi na magamba.
10 And all that have not fins and scales in the seas, and in the rivers, of all that move in the waters, and of all the living creatures that are in the waters, they are an abomination unto you,
Lakini viumbe wote ndani ya bahari au vijito wasio na mapezi na magamba, wakiwa miongoni mwa makundi au viumbe wote ndani ya maji, hao ni machukizo kwenu.
11 and they shall be an abomination unto you; ye shall not eat of their flesh, and their carcases ye shall have in abomination.
Nao watakuwa machukizo kwenu. Msile nyama yao, nayo mizoga yao itakuwa machukizo.
12 Whatsoever hath no fins nor scales in the waters, that is an abomination unto you.
Chochote kinachoishi ndani ya maji ambacho hakina mapezi na magamba kitakuwa chukizo kwenu.
13 And these ye shall have in abomination among the fowls; they shall not be eaten, they are an abomination: the eagle, and the gier eagle, and the ospray;
“‘Wafuatao ndio ndege watakaokuwa machukizo kwenu, hivyo msiwale kwa sababu ni chukizo: tai, furukombe, kipungu,
14 and the kite, and the falcon after its kind;
mwewe mwekundu, aina zote za mwewe mweusi,
15 every raven after its kind;
aina zote za kunguru,
16 and the ostrich, and the night hawk, and the seamew, and the hawk after its kind;
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga, shakwe, aina zote za kipanga,
17 and the little owl, and the cormorant, and the great owl;
bundi, mnandi, bundi mkubwa,
18 and the horned owl, and the pelican, and the vulture;
mumbi, mwari, nderi,
19 and the stork, the heron after its kind, and the hoopoe, and the bat.
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
20 All winged creeping things that go upon all four are an abomination unto you.
“‘Wadudu wote warukao ambao hutembea kwa miguu minne watakuwa chukizo kwenu.
21 Yet these may ye eat of all winged creeping things that go upon all four, which have legs above their feet, to leap withal upon the earth;
Lakini wako viumbe wenye mabawa ambao hutembea kwa miguu minne mtakaowala: wale wenye vifundo katika miguu yao ya kurukaruka juu ya ardhi.
22 even these of them ye may eat; the locust after its kind, and the bald locust after its kind, and the cricket after its kind, and the grasshopper after its kind.
Miongoni mwa hawa, mtakula nzige wa aina zote, senene, parare au panzi.
23 But all winged creeping things, which have four feet, are an abomination unto you.
Lakini viumbe wengine wote wenye mabawa na wenye miguu minne ni machukizo kwenu.
24 And by these ye shall become unclean: whosoever toucheth the carcase of them shall be unclean until the even:
“‘Mtajinajisi kwa wanyama hawa. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
25 And whosoever beareth [aught] of the carcase of them shall wash his clothes, and be unclean until the even.
Yeyote atakayebeba mizoga ya viumbe hawa ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
26 Every beast which parteth the hoof, and is not clovenfooted, nor cheweth the cud, is unclean unto you: every one that toucheth them shall be unclean.
“‘Kila mnyama mwenye ukwato ulioachana lakini haukugawanyika kabisa, au yule asiyecheua, huyo ni najisi kwenu; yeyote agusaye mzoga wowote wa hao atakuwa najisi.
27 And whatsoever goeth upon its paws, among all beasts that go on all four, they are unclean unto you: whoso toucheth their carcase shall be unclean until the even.
Miongoni mwa wanyama wote watembeao kwa miguu minne, wale watembeao kwa vitanga vyao ni najisi kwenu; yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
28 And he that beareth the carcase of them shall wash his clothes, and be unclean until the even: they are unclean unto you.
Yeyote atakayebeba mizoga yao ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Wanyama hawa ni najisi kwenu.
29 And these are they which are unclean unto you among the creeping things that creep upon the earth; the weasel, and the mouse, and the great lizard after its kind,
“‘Kuhusu wanyama watambaao juu ya ardhi, hawa ni najisi kwenu: kicheche, panya, aina yoyote ya mijusi mikubwa,
30 and the gecko, and the land-crocodile, and the lizard, and the sand-lizard, and the chameleon.
guruguru, kenge, mijusi ya ukutani, goromoe na kinyonga.
31 These are they which are unclean to you among all that creep: whosoever doth touch them, when they are dead, shall be unclean until the even.
Hao wote watambaao juu ya ardhi ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
32 And upon whatsoever any of them, when they are dead, doth fall, it shall be unclean; whether it be any vessel of wood, or raiment, or skin, or sack, whatsoever vessel it be, wherewith any work is done, it must be put into water, and it shall be unclean until the even; then shall it be clean.
Ikiwa mmoja wao atakufa na kuangukia juu ya kitu fulani, chombo hicho, hata kikiwa cha matumizi gani, kitakuwa najisi, kiwe kimetengenezwa kwa mti, nguo, ngozi au gunia. Kiweke ndani ya maji; kitakuwa najisi mpaka jioni, kisha kitakuwa safi tena.
33 And every earthen vessel, whereinto any of them falleth, whatsoever is in it shall be unclean, and it ye shall break.
Ikiwa mmoja wa wanyama aliyekufa ataangukia ndani ya chungu, kila kilichomo katika chungu hicho kitakuwa najisi, nawe ni lazima uvunje chungu hicho.
34 All food [therein] which may be eaten, that on which water cometh, shall be unclean: and all drink that may be drunk in every [such] vessel shall be unclean.
Chakula chochote ambacho chaweza kuliwa lakini kikawa kimeingia maji kutoka kwenye chungu hicho ni najisi, na kitu chochote cha majimaji ambacho chaweza kunyweka kutoka kwenye chungu hicho ni najisi.
35 And every thing whereupon [any part] of their carcase falleth shall be unclean; whether oven, or range for pots, it shall be broken in pieces: they are unclean, and shall be unclean unto you.
Chochote ambacho mzoga wa mmojawapo utaangukia kitakuwa najisi. Jiko au chungu cha kupikia ni lazima kivunjwe. Ni najisi, nawe ni lazima uvihesabu kuwa najisi.
36 Nevertheless a fountain or a pit wherein is a gathering of water shall be clean: but that which toucheth their carcase shall be unclean.
Lakini chemchemi au kisima, mahali pa kuchota maji, patakuwa safi, lakini yeyote atakayegusa moja ya mizoga hii ni najisi.
37 And if [aught] of their carcase fall upon any sowing seed which is to be sown, it is clean.
Kama mzoga ukianguka juu ya mbegu zozote ambazo ni za kupanda, zinabaki safi.
38 But if water be put upon the seed, and [aught] of their carcase fall thereon, it is unclean unto you.
Lakini kama mbegu imetiwa maji na mzoga ukaanguka juu yake, hiyo mbegu ni najisi kwenu.
39 And if any beast, of which ye may eat, die; he that toucheth the carcase thereof shall be unclean until the even.
“‘Kama mnyama ambaye mnaruhusiwa kumla akifa, yeyote atakayeugusa mzoga wake atakuwa najisi mpaka jioni.
40 And he that eateth of the carcase of it shall wash his clothes, and be unclean until the even: he also that beareth the carcase of it shall wash his clothes, and be unclean until the even.
Yeyote atakayekula sehemu ya mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayebeba mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
41 And every creeping thing that creepeth upon the earth is an abomination; it shall not be eaten.
“‘Kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi ni chukizo; kisiliwe.
42 Whatsoever goeth upon the belly, and whatsoever goeth upon all four, or whatsoever hath many feet, even all creeping things that creep upon the earth, them ye shall not eat; for they are an abomination.
Msile kiumbe chochote kitambaacho juu ya ardhi, kiwe kitambaacho kwa tumbo lake, au kitambaacho kwa miguu minne au kwa miguu mingi; ni chukizo.
43 Ye shall not make yourselves abominable with any creeping thing that creepeth, neither shall ye make yourselves unclean with them, that ye should be defiled thereby.
Msijitie unajisi kwa chochote katika viumbe hivi. Msijitie unajisi kwa viumbe hivyo au kutiwa unajisi navyo.
44 For I am the LORD your God: sanctify yourselves therefore, and be ye holy; for I am holy: neither shall ye defile yourselves with any manner of creeping thing that moveth upon the earth.
Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; jitakaseni mwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu. Msijitie unajisi wenyewe kwa kiumbe chochote kile kiendacho juu ya ardhi.
45 For I am the LORD that brought you up out of the land of Egypt, to be your God: ye shall therefore be holy, for I am holy.
Mimi ndimi Bwana niliyewapandisha mtoke Misri ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo kuweni watakatifu kwa sababu Mimi ni mtakatifu.
46 This is the law of the beast, and of the fowl, and of every living creature that moveth in the waters, and of every creature that creepeth upon the earth:
“‘Haya ndiyo masharti kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho ndani ya maji, na kila kiumbe kiendacho juu ya ardhi.
47 to make a difference between the unclean and the clean, and between the living thing that may be eaten and the living thing that may not be eaten.
Ni lazima mpambanue kati ya kilicho najisi na kilicho safi, kati ya viumbe hai vinavyoweza kuliwa na vile visivyoweza kuliwa.’”

< Leviticus 11 >