< Joshua 16 >

1 And the lot for the children of Joseph went out from the Jordan at Jericho, at the waters of Jericho on the east, even the wilderness, going up from Jericho through the hill country to Beth-el;
Mgawanyo wa Yosefu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli.
2 and it went out from Beth-el to Luz, and passed along unto the border of the Archites to Ataroth;
Ukaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waariki huko Atarothi,
3 and it went down westward to the border of the Japhletites, unto the border of Beth-horon the nether, even unto Gezer: and the goings out thereof were at the sea.
ukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
4 And the children of Joseph, Manasseh and Ephraim, took their inheritance.
Kwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yosefu, walipokea urithi wao.
5 And the border of the children of Ephraim according to their families was [thus]: even the border of their inheritance eastward was Ataroth-addar, unto Beth-horon the upper;
Hili ndilo lilikuwa eneo la Efraimu, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao ulianzia Ataroth-Adari upande wa mashariki hadi Beth-Horoni ya Juu,
6 and the border went out westward at Michmethath on the north; and the border turned about eastward unto Taanath-shiloh, and passed along it on the east of Janoah;
na kuendelea mpaka baharini. Kutoka Mikmeta upande wa kaskazini ulipinda kuelekea mashariki hadi Taanath-Shilo, ukiupita hadi Yanoa upande wa mashariki.
7 and it went down from Janoah to Ataroth, and to Naarah, and reached unto Jericho, and went out at Jordan.
Kisha uliteremka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara, ukagusa Yeriko na kutokea katika Mto Yordani.
8 From Tappuah the border went along westward to the brook of Kanah; and the goings out thereof were at the sea. This is the inheritance of the tribe of the children of Ephraim according to their families;
Kutoka Tapua mpaka ulikwenda magharibi hadi Bonde la Kana na kuishia baharini. Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Waefraimu, ukoo kwa ukoo.
9 together with the cities which were separated for the children of Ephraim in the midst of the inheritance of the children of Manasseh, all the cities with their villages.
Pia ulijumuisha miji yote na vijiji vyake ambavyo vilitengwa kwa ajili ya Waefraimu ndani ya urithi wa kabila la Manase.
10 And they drave not out the Canaanites that dwelt in Gezer: but the Canaanites dwelt in the midst of Ephraim, unto this day, and became servants to do taskwork.
Hawakuwatoa Wakanaani waishio Gezeri; mpaka leo Wakanaani wanaishi miongoni mwa watu wa Efraimu lakini wanatakiwa kufanya kazi ngumu za kulazimishwa.

< Joshua 16 >