< Job 6 >

1 Then Job answered and said,
Kisha Ayubu akajibu:
2 Oh that my vexation were but weighed, and my calamity laid in the balances together!
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 For now it would be heavier than the sand of the seas: therefore have my words been rash.
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 For the arrows of the Almighty are within me, the poison whereof my spirit drinketh up: the terrors of God do set themselves in array against me.
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 Doth the wild ass bray when he hath grass? or loweth the ox over his fodder?
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 Can that which hath no savour be eaten without salt? or is there any taste in the white of an egg?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 My soul refuseth to touch [them]; they are as loathsome meat to me.
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 Oh that I might have my request; and that God would grant [me] the thing that I long for.
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 Even that it would please God to crush me; that he would let loose his hand, and cut me off!
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 Then should I yet have comfort; yea, I would exult in pain that spareth not: for I have not denied the words of the Holy One.
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 What is my strength, that I should wait? and what is mine end, at I should be patient?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 Is my strength the strength of stones? or is my flesh of brass?
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 Is it not that I have no help in me, and that effectual working is driven quite from me?
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 To him that is ready to faint kindness [should be shewed] from his friend; even to him that forsaketh the fear of the Almighty.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 My brethren have dealt deceitfully as a brook, as the channel of brooks that pass away;
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 Which are black by reason of the ice, [and] wherein the snow hideth itself:
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 What time they wax warm, they vanish: when it is hot, they are consumed out of their place.
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 The caravans [that travel] by the way of them turn aside; they go up into the waste, and perish.
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 The caravans of Tema looked, the companies of Sheba waited for them.
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 They were ashamed because they had hoped; they came thither, and were confounded.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 For now ye are nothing; ye see a terror, and are afraid.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 Did I say, Give unto me? or, offer a present for me of your substance?
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 Or, Deliver me from the adversary’s hand? or, Redeem me from the hand of the oppressors?
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Teach me, and I will hold my peace: and cause me to understand wherein I have erred.
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 How forcible are words of uprightness! but what doth your arguing reprove?
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 Do ye imagine to reprove words? seeing that the speeches of one that is desperate are as wind.
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 Yea, ye would cast [lots] upon the fatherless, and make merchandise of your friend.
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 Now therefore be pleased to look upon me; for surely I shall not lie to your face.
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Return, I pray you, let there be no injustice; yea, return again, my cause is righteous.
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 Is there injustice on my tongue? cannot my taste discern mischievous things?
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?

< Job 6 >