< Job 3 >

1 After this opened Job his mouth, and cursed his day.
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
2 And Job answered and said:
Kisha akasema:
3 Let the day perish wherein I was born, and the night which said, There is a man child conceived.
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 Let that day be darkness; let not God regard it from above, neither let the light shine upon it.
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
5 Let darkness and the shadow of death claim it for their own; let a cloud dwell upon it; let all that maketh black the day terrify it.
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
6 As for that night, let thick darkness seize upon it: let it not rejoice among the days of the year; let it not come into the number of the months.
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
7 Lo, let that night be barren; let no joyful voice come therein.
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
8 Let them curse it that curse the day, who are ready to rouse up leviathan.
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
9 Let the stars of the twilight thereof be dark: let it look for light, but have none; neither let it behold the eyelids of the morning:
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
10 Because it shut not up the doors of my [mother’s] womb, nor hid trouble from mine eyes.
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
11 Why died I not from the womb? why did I not give up the ghost when I came out of the belly?
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
12 Why did the knees receive me? or why the breasts, that I should suck?
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
13 For now should I have lain down and been quiet; I should have slept; then had I been at rest:
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
14 With kings and counsellors of the earth, which built up waste places for themselves;
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
15 Or with princes that had gold, who filled their houses with silver:
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
16 Or as an hidden untimely birth I had not been; as infants which never saw light.
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 There the wicked cease from troubling; and there the weary be at rest.
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
18 There the prisoners are at ease together; they hear not the voice of the taskmaster.
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 The small and great are there; and the servant is free from his master.
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
20 Wherefore is light given to him that is in misery, and life unto the bitter in soul;
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 Which long for death, but it cometh not; and dig for it more than for hid treasures;
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 Which rejoice exceedingly, and are glad, when they can find the grave?
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
23 [Why is light given] to a man whose way is hid, and whom God hath hedged in?
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
24 For my sighing cometh before I eat, and my roarings are poured out like water.
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
25 For the thing which I fear cometh upon me, and that which I am afraid of cometh unto me.
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
26 I am not at ease, neither am I quiet, neither have I rest; but trouble cometh.
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”

< Job 3 >