< Job 14 >

1 Man that is born of a woman is of few days, and full of trouble.
“Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
2 He cometh forth like a flower, and is cut down: he fleeth also as a shadow, and continueth not.
Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
3 And dost thou open thine eyes upon such an one, and bringest me into judgment with thee?
Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
4 Who can bring a clean thing out of an unclean? not one.
Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
5 Seeing his days are determined, the number of his months is with thee, and thou hast appointed his bounds that he cannot pass;
Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
6 Look away from him, that he may rest, till he shall accomplish, as an hireling, his day.
Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
7 For there is hope of a tree, if it be cut down, that it will sprout again, and that the tender branch thereof will not cease.
“Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
8 Though the root thereof wax old in the earth, and the stock thereof die in the ground;
Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
9 Yet through the scent of water it will bud, and put forth boughs like a plant.
lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
10 But man dieth, and wasteth away: yea, man giveth up the ghost, and where is he?
Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
11 [As] the waters fail from the sea, and the river decayeth and drieth up;
Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
12 So man lieth down and riseth not: till the heavens be no more, they shall not awake, nor be roused out of their sleep.
ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
13 Oh that thou wouldest hide me in Sheol, that thou wouldest keep me secret, until thy wrath be past, that thou wouldest appoint me a set time, and remember me! (Sheol h7585)
“Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol h7585)
14 If a man die, shall he live [again]? all the days of my warfare would I wait, till my release should come.
Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
15 Thou shouldest call, and I would answer thee: thou wouldest have a desire to the work of thine hands.
Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
16 But now thou numberest my steps: dost thou not watch over my sin?
Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
17 My transgression is sealed up in a bag, and thou fastenest up mine iniquity.
Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
18 And surely the mountain falling cometh to nought, and the rock is removed out of its place;
“Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
19 The waters wear the stones; the overflowings thereof wash away the dust of the earth: and thou destroyest the hope of man.
kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
20 Thou prevailest for ever against him, and he passeth; thou changest his countenance, and sendest him away.
Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
21 His sons come to honour, and he knoweth it not; and they are brought low, but he perceiveth it not of them.
Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wakidharauliwa, yeye haoni.
22 But his flesh upon him hath pain, and his soul within him mourneth.
Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”

< Job 14 >