< Hosea 7 >

1 When I would heal Israel, then is the iniquity of Ephraim discovered, and the wickedness of Samaria; for they commit falsehood: and the thief entereth in, [and] the troop of robbers spoileth without.
kila mara nilipotaka kumponya Israeli, dhambi za Efraimu zinafichuliwa na maovu ya Samaria yanafunuliwa. Wanafanya udanganyifu, wevi huvunja nyumba, maharamia hunyangʼanya barabarani,
2 And they consider not in their hearts that I remember all their wickedness: now have their own doings beset them about; they are before my face.
lakini hawafahamu kwamba ninakumbuka matendo yao yote mabaya. Dhambi zao zimewameza, ziko mbele zangu siku zote.
3 They make the king glad with their wickedness, and the princes with their lies.
“Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao, wakuu wao kwa uongo wao.
4 They are all adulterers; they are as an oven heated by the baker; he ceaseth to stir [the fire], from the kneading of the dough until it be leavened.
Wote ni wazinzi, wanawaka kama tanuru ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea kuanzia kukanda unga hadi umekwisha kuumuka.
5 On the day of our king the princes made themselves sick with the heat of wine; he stretched out his hand with scorners.
Katika sikukuu ya mfalme wetu wakuu wanawaka kwa mvinyo, naye anawaunga mkono wenye mizaha.
6 For they have made ready their heart like an oven, whiles they lie in wait: their baker sleepeth all the night; in the morning it burneth as a flaming fire.
Mioyo yao ni kama tanuru, wanamwendea kwa hila. Hasira yao inafoka moshi usiku kucha, wakati wa asubuhi inalipuka kama miali ya moto.
7 They are all hot as an oven, and devour their judges; all their kings are fallen: there is none among them that calleth unto me.
Wote ni moto kama tanuru; wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wake wote wanaanguka, wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.
8 Ephraim, he mixeth himself among the peoples; Ephraim is a cake not turned.
“Efraimu anajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate ambao haukuiva.
9 Strangers have devoured his strength, and he knoweth [it] not: yea, gray hairs are here and there upon him, and he knoweth [it] not.
Wageni wananyonya nguvu zake, lakini hafahamu hilo. Nywele zake zina mvi hapa na pale, lakini hana habari.
10 And the pride of Israel doth testify to his face: yet they have not returned unto the LORD their God, nor sought him, for all this.
Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake, lakini pamoja na haya yote harudi kwa Bwana Mungu wake wala kumtafuta.
11 And Ephraim is like a silly dove, without understanding: they call unto Egypt, they go to Assyria.
“Efraimu ni kama hua, hudanganywa kwa urahisi na hana akili: mara anaita Misri, mara anageukia Ashuru.
12 When they shall go, I will spread my net upon them; I will bring them down as the fowls of the heaven: I will chastise them, as their congregation hath heard.
Wakati watakapokwenda, nitatupa wavu wangu juu yao; nitawavuta chini waanguke kama ndege wa angani. Nitakaposikia wakikusanyika pamoja, nitawanasa.
13 Woe unto them! for they have wandered from me; destruction unto them! for they have trespassed against me: though I would redeem them, yet they have spoken lies against me.
Ole wao, kwa sababu wamepotoka kutoka kwangu! Maangamizi ni yao kwa sababu wameniasi! Ninatamani kuwakomboa, lakini wanasema uongo dhidi yangu.
14 And they have not cried unto me with their heart, but they howl upon their beds: they assemble themselves for corn and wine, they rebel against me.
Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao, bali wanaomboleza vitandani mwao. Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya, lakini hugeukia mbali nami.
15 Though I have taught and strengthened their arms, yet do they imagine mischief against me.
Niliwafundisha na kuwatia nguvu, lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.
16 They return, but not to [him that is] on high; they are like a deceitful bow: their princes shall fall by the sword for the rage of their tongue: this shall be their derision in the land of Egypt.
Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana, wako kama upinde wenye kasoro. Viongozi wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya maneno yao ya jeuri. Kwa ajili ya hili watadhihakiwa katika nchi ya Misri.

< Hosea 7 >