< Hosea 11 >

1 When Israel was a child, then I loved him, and called my son out of Egypt.
“Wakati Israeli alipokuwa mtoto, nilimpenda, nilimwita mwanangu kutoka Misri.
2 As they called them, so they went from them: they sacrificed unto the Baalim, and burned incense to graven images.
Lakini kadiri nilivyomwita Israeli, ndivyo walivyokwenda mbali nami. Walitoa dhabihu kwa Mabaali na kufukiza uvumba kwa vinyago.
3 Yet I taught Ephraim to go; I took them on my arms; but they knew not that I healed them.
Mimi ndiye niliyemfundisha Efraimu kutembea, nikiwashika mikono; lakini hawakutambua kuwa ni mimi niliyewaponya.
4 I drew them with cords of a man, with bands of love; and I was to them as they that take off the yoke on their jaws, and I laid meat before them.
Niliwaongoza kwa kamba za huruma ya kibinadamu, kwa vifungo vya upendo; niliondoa nira shingoni mwao nami nikainama kuwalisha.
5 He shall not return into the land of Egypt; but the Assyrian shall be his king, because they refused to return.
“Je, hawatarudi Misri, nayo Ashuru haitawatawala kwa sababu wamekataa kutubu?
6 And the sword shall fall upon his cities, and shall consume his bars, and devour [them], because of their own counsels.
Panga zitametameta katika miji yao, zitaharibu makomeo ya malango yao na kukomesha mipango yao.
7 And my people are bent to backsliding from me: though they call them to [him that is] on high, none at all will exalt [him].
Watu wangu wamedhamiria kuniacha. Hata kama wakimwita Yeye Aliye Juu Sana, kwa vyovyote hatawainua.
8 How shall I give thee up, Ephraim? [how] shall I deliver thee, Israel? how shall I make thee as Admah? [how] shall I set thee as Zeboim? mine heart is turned within me, my compassions are kindled together.
“Efraimu, ninawezaje kukuacha? Ee Israeli, ninawezaje kukutoa? Nitawezaje kukutendea kama Adma? Nitawezaje kukufanya kama Seboimu? Moyo wangu umegeuka ndani yangu, huruma zangu zote zimeamshwa.
9 I will not execute the fierceness of mine anger, I will not return to destroy Ephraim: for I am God, and not man; the Holy One in the midst of thee: and I will not enter into the city.
Sitatimiza hasira yangu kali, wala sitageuka na kumharibu Efraimu. Kwa kuwa mimi ndimi Mungu, wala si mwanadamu, Aliye Mtakatifu miongoni mwenu. Sitakuja kwa ghadhabu.
10 They shall walk after the LORD, who shall roar like a lion: for he shall roar, and the children shall come trembling from the west.
Watamfuata Bwana; atanguruma kama simba. Wakati angurumapo, watoto wake watakuja wakitetemeka kutoka magharibi.
11 They shall come trembling as a bird out of Egypt, and as a dove out of the land of Assyria: and I will make them to dwell in their houses, saith the LORD.
Watakuja wakitetemeka kama ndege wakitoka Misri, kama hua wakitoka Ashuru. Nitawakalisha katika nyumba zao,” asema Bwana.
12 Ephraim compasseth me about with falsehood, and the house of Israel with deceit: but Judah yet ruleth with God, and is faithful with the Holy One.
Efraimu amenizunguka kwa uongo, nyumba ya Israeli kwa udanganyifu. Naye Yuda ni mkaidi dhidi ya Mungu, hata kinyume cha yule mwaminifu Aliye Mtakatifu.

< Hosea 11 >