< Genesis 33 >

1 And Jacob lifted up his eyes, and looked, and, behold, Esau came, and with him four hundred men. And he divided the children unto Leah, and unto Rachel, and unto the two handmaids.
Yakobo akainua macho akamwona Esau akija na watu wake 400, kwa hiyo akawagawanya watoto kati ya Lea, Raheli na wale watumishi wake wawili wa kike.
2 And he put the handmaids and their children foremost, and Leah and her children after, and Rachel and Joseph hindermost.
Akawaweka wale watumishi wa kike na watoto wao mbele, Lea na watoto wake wakafuata, Raheli na Yosefu wakaja nyuma.
3 And he himself passed over before them, and bowed himself to the ground seven times, until he came near to his brother.
Yeye mwenyewe akatangulia mbele na kusujudu mara saba alipomkaribia ndugu yake.
4 And Esau ran to meet him, and embraced him, and fell on his neck, and kissed him: and they wept.
Lakini Esau akamkimbilia Yakobo kumlaki na kumkumbatia, akamwangukia shingoni na kumbusu. Nao wakalia.
5 And he lifted up his eyes, and saw the women and the children; and said, Who are these with thee? And he said, The children which God hath graciously given thy servant.
Esau akainua macho akawaona wale wanawake na watoto. Akauliza, “Hawa uliofuatana nao ni nani?” Yakobo akamjibu, “Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako kwa neema.”
6 Then the handmaids came near, they and their children, and they bowed themselves.
Kisha wale watumishi wa kike na watoto wao wakakaribia na kusujudu.
7 And Leah also and her children came near, and bowed themselves: and after came Joseph near and Rachel, and they bowed themselves.
Kisha Lea na watoto wake wakaja na kusujudu. Mwisho wa wote wakaja Yosefu na Raheli, nao pia wakasujudu.
8 And he said, What meanest thou by all this company which I met? And he said, To find grace in the sight of my lord.
Esau akauliza, “Una maana gani kuhusu makundi hayo yote niliyokutana nayo?” Akasema, “Ni ili kupata kibali machoni pako, bwana wangu.”
9 And Esau said, I have enough; my brother, let that thou hast be thine.
Lakini Esau akamwambia, “Ndugu yangu, tayari nina wingi wa mali. Ulivyo navyo viwe vyako mwenyewe.”
10 And Jacob said, Nay, I pray thee, if now I have found grace in thy sight, then receive my present at my hand: forasmuch as I have seen thy face, as one seeth the face of God, and thou wast pleased with me.
Yakobo akasema, “La hasha! Tafadhali, kama nimepata kibali machoni pako, upokee zawadi hii kutoka kwangu. Kwa maana kuuona uso wako, ni kama kuuona uso wa Mungu, kwa kuwa umenipokea kwa takabali kubwa.
11 Take, I pray thee, my gift that is brought to thee; because God hath dealt graciously with me, and because I have enough. And he urged him, and he took it.
Tafadhali ukubali zawadi iliyoletwa kwako, kwa kuwa Mungu amenineemesha na ninavyo vyote ninavyohitaji.” Kwa sababu Yakobo alisisitiza, Esau akapokea.
12 And he said, Let us take our journey, and let us go, and I will go before thee.
Ndipo Esau akasema, “Na tuendelee na safari, nitakuwa pamoja nawe.”
13 And he said unto him, My lord knoweth that the children are tender, and that the flocks and herds with me give suck: and if they overdrive them one day, all the flocks will die.
Lakini Yakobo akamwambia, “Bwana wangu unajua kwamba watoto ni wachanga na kwamba ni lazima nitunze hawa kondoo wake na ngʼombe wanaonyonyesha. Wakipelekwa kwa haraka hata kama ni kwa siku moja tu, wanyama wote watakufa.
14 Let my lord, I pray thee, pass over before his servant: and I will lead on softly, according to the pace of the cattle that is before me and according to the pace of the children, until I come unto my lord unto Seir.
Hivyo bwana wangu umtangulie mtumishi wako, wakati mimi nikija polepole kwa mwendo wa makundi yaliyo mbele yangu na mwendo wa watoto, mpaka nifike kwa bwana wangu huko Seiri.”
15 And Esau said, Let me now leave with thee some of the folk that are with me. And he said, What needeth it? let me find grace in the sight of my lord.
Esau akamwambia, “Basi na niwaache baadhi ya watu wangu pamoja nawe.” Yakobo akauliza, “Lakini kwa nini ufanye hivyo, niache tu nipate kibali machoni pa bwana wangu.”
16 So Esau returned that day on his way unto Seir.
Hivyo siku hiyo Esau akashika njia akarudi Seiri.
17 And Jacob journeyed to Succoth, and built him an house, and made booths for his cattle: therefore the name of the place is called Succoth.
Pamoja na hayo, Yakobo akaenda Sukothi, mahali alipojijengea makazi kwa ajili yake na mabanda kwa ajili ya mifugo yake. Hii ndiyo sababu sehemu ile inaitwa Sukothi.
18 And Jacob came in peace to the city of Shechem, which is in the land of Canaan, when he came from Paddan-aram; and encamped before the city.
Baada ya Yakobo kutoka Padan-Aramu, alifika salama katika mji wa Shekemu huko Kanaani na kuweka kambi yake karibu na mji.
19 And he bought the parcel of ground, where he had spread his tent, at the hand of the children of Hamor, Shechem’s father, for an hundred pieces of money.
Akanunua kiwanja kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa bei ya vipande mia vya fedha, ambapo alipiga hema lake.
20 And he erected there an altar, and called it El-elohe-Israel.
Pale akajenga madhabahu na kupaita El-Elohe-Israeli.

< Genesis 33 >