< Ezekiel 19 >

1 Moreover, take thou up a lamentation for the princes of Israel,
“Wewe fanya maombolezo kuhusu wakuu wa Israeli
2 and say, What was thy mother? A lioness: she couched among lions, in the midst of the young lions she nourished her whelps.
na useme: “‘Tazama jinsi gani mama yako alivyokuwa simba jike miongoni mwa simba! Alilala katikati ya wana simba na kulisha watoto wake.
3 And she brought up one of her whelps; he became a young lion: and he learned to catch the prey, he devoured men.
Alimlea mmoja wa watoto wake, naye akawa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
4 The nations also heard of him; he was taken in their pit: and they brought him with hooks unto the land of Egypt.
Mataifa wakasikia habari zake, naye akanaswa katika shimo lao. Wakamwongoza kwa ndoana mpaka nchi ya Misri.
5 Now when she saw that she had waited, and her hope was lost, then she took another of her whelps, and made him a young lion.
“‘Mama yake alipongoja na kuona tumaini lake halitimiziki, nayo matarajio yake yametoweka, akamchukua mwanawe mwingine na kumfanya simba mwenye nguvu.
6 And he went up and down among the lions, he became a young lion: and he learned to catch the prey, he devoured men.
Alizungukazunguka miongoni mwa simba, kwa kuwa sasa alikuwa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
7 And he knew their palaces, and laid waste their cities; and the land was desolate, and the fulness thereof, because of the noise of his roaring.
Akabomoa ngome zao na kuiharibu miji yao. Nchi na wote waliokuwa ndani yake wakatiwa hofu kwa kunguruma kwake.
8 Then the nations set against him on every side from the provinces: and they spread their net over him; he was taken in their pit.
Kisha mataifa wakaja dhidi yake kutoka sehemu zilizomzunguka. Wakatanda nyavu zao kwa ajili yake, naye akanaswa katika shimo lao.
9 And they put him in a cage with hooks, and brought him to the king of Babylon; they brought him into strong holds, that his voice should no more be heard upon the mountains of Israel.
Kwa kutumia ndoana wakamvutia kwenye tundu na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli. Wakamtia gerezani, hivyo kunguruma kwake hakukusikika tena katika milima ya Israeli.
10 Thy mother was like a vine, in thy blood, planted by the waters: she was fruitful and full of branches by reason of many waters.
“‘Mama yako alikuwa kama mzabibu katika shamba lako la mizabibu uliopandwa kando ya maji, ukiwa unazaa sana na wenye matawi mengi kwa sababu ya wingi wa maji.
11 And she had strong rods for the sceptres of them that bare rule, and their stature was exalted among the thick boughs, and they were seen in their height with the multitude of their branches.
Matawi yake yalikuwa na nguvu, yaliyofaa kuwa fimbo ya enzi ya mtawala. Ulikuwa mrefu kupita miti mingine katikati ya matawi manene; ulionekana kwa urahisi kwa ajili ya urefu wake na wingi wa matawi yake.
12 But she was plucked up in fury, she was cast down to the ground, and the east wind dried up her fruit: her strong rods were broken off and withered; the fire consumed them.
Lakini ulingʼolewa kwa hasira kali na kutupwa chini. Upepo wa mashariki uliufanya usinyae, matunda yake yakapukutika, matawi yake yenye nguvu yakanyauka na moto ukayateketeza.
13 And now she is planted in the wilderness, in a dry and thirsty land.
Sasa umepandwa jangwani katika nchi kame na ya kiu.
14 And fire is gone out of the rods of her branches, it hath devoured her fruit, so that there is in her no strong rod to be a sceptre to rule. This is a lamentation, and shall be for a lamentation.
Moto ulienea kuanzia katika mmojawapo ya matawi yake makubwa na kuteketeza matunda yake. Hakuna tawi lenye nguvu lililobaki juu yake lifaalo kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.’ Hili ndilo ombolezo, na litumike kama ombolezo.”

< Ezekiel 19 >