< Exodus 39 >

1 And of the blue, and purple, and scarlet, they made finely wrought garments, for ministering in the holy place, and made the holy garments for Aaron; as the LORD commanded Moses.
Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
2 And he made the ephod of gold, blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen.
Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
3 And they did beat the gold into thin plates, and cut it into wires, to work it in the blue, and in the purple, and in the scarlet, and in the fine linen, the work of the cunning workman.
Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
4 They made shoulderpieces for it, joined together: at the two ends was it joined together.
Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
5 And the cunningly woven band, that was upon it, to gird it on withal, was of the same piece [and] like the work thereof; of gold, of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen; as the LORD commanded Moses.
Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
6 And they wrought the onyx stones, enclosed in ouches of gold, graven with the engravings of a signet, according to the names of the children of Israel.
Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
7 And he put them on the shoulderpieces of the ephod, to be stones of memorial for the children of Israel; as the LORD commanded Moses.
Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
8 And he made the breastplate, the work of the cunning workman, like the work of the ephod; of gold, of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen.
Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
9 It was foursquare; they made the breastplate double: a span was the length thereof, and a span the breadth thereof, being double.
Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
10 And they set in it four rows of stones: a row of sardius, topaz, and carbuncle was the first row.
Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
11 And the second row, an emerald, a sapphire, and a diamond.
safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
12 And the third row, a jacinth, an agate, and an amethyst.
safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
13 And the fourth row, a beryl, an onyx, and a jasper: they were enclosed in ouches of gold in their settings.
katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
14 And the stones were according to the names of the children of Israel, twelve, according to their names; like the engravings of a signet, every one according to his name, for the twelve tribes.
Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
15 And they made upon the breastplate chains like cords, of wreathen work of pure gold.
Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
16 And they made two ouches of gold, and two gold rings; and put the two rings on the two ends of the breastplate.
Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
17 And they put the two wreathen chains of gold on the two rings at the ends of the breastplate.
Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
18 And the [other] two ends of the two wreathen chains they put on the two ouches, and put them on the shoulderpieces of the ephod, in the forepart thereof.
nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
19 And they made two rings of gold, and put them upon the two ends of the breastplate, upon the edge thereof, which was toward the side of the ephod inward.
Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
20 And they made two rings of gold, and put them on the two shoulderpieces of the ephod underneath, in the forepart thereof, close by the coupling thereof, above the cunningly woven band of the ephod.
Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
21 And they did bind the breastplate by the rings thereof unto the rings of the ephod with a lace of blue, that it might be upon the cunningly woven band of the ephod, and that the breastplate might not be loosed from the ephod; as the LORD commanded Moses.
Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
22 And he made the robe of the ephod of woven work, all of blue;
Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
23 and the hole of the robe in the midst thereof, as the hole of a coat of mail, with a binding round about the hole of it, that it should not be rent.
na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
24 And they made upon the skirts of the robe pomegranates of blue, and purple, and scarlet, [and] twined [linen].
Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
25 And they made bells of pure gold, and put the bells between the pomegranates upon the skirts of the robe round about, between the pomegranates;
Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
26 a bell and a pomegranate, a bell and a pomegranate, upon the skirts of the robe round about, to minister in; as the LORD commanded Moses.
Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
27 And they made the coats of fine linen of woven work for Aaron, and for his sons,
Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
28 and the mitre of fine linen, and the goodly headtires of fine linen, and the linen breeches of fine twined linen,
na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
29 and the girdle of fine twined linen, and blue, and purple, and scarlet, the work of the embroiderer; as the LORD commanded Moses.
Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
30 And they made the plate of the holy crown of pure gold, and wrote upon it a writing, like the engravings of a signet, HOLY TO THE LORD.
Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
31 And they tied unto it a lace of blue, to fasten it upon the mitre above; as the LORD commanded Moses.
Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
32 Thus was finished all the work of the tabernacle of the tent of meeting: and the children of Israel did according to all that the LORD commanded Moses, so did they.
Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
33 And they brought the tabernacle unto Moses, the Tent, and all its furniture, its clasps, its boards, its bars, and its pillars, and its sockets;
Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
34 and the covering of rams’ skins dyed red, and the covering of sealskins, and the veil of the screen;
kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
35 the ark of the testimony, and the staves thereof, and the mercy-seat;
Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
36 the table, all the vessels thereof, and the shewbread;
meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
37 the pure candlestick, the lamps thereof, even the lamps to be set in order, and all the vessels thereof, and the oil for the light;
kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
38 and the golden altar, and the anointing oil, and the sweet incense, and the screen for the door of the Tent;
madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
39 the brasen altar, and its grating of brass, its staves, and all its vessels, the laver and its base;
madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
40 the hangings of the court, its pillars, and its sockets, and the screen for the gate of the court, the cords thereof, and the pins thereof, and all the instruments of the service of the tabernacle, for the tent of meeting;
mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
41 the finely wrought garments for ministering in the holy place, and the holy garments for Aaron the priest, and the garments of his sons, to minister in the priest’s office.
na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
42 According to all that the LORD commanded Moses, so the children of Israel did all the work.
Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
43 And Moses saw all the work, and, behold, they had done it; as the LORD had commanded, even so had they done it: and Moses blessed them.
Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.

< Exodus 39 >