< Exodus 25 >

1 And the LORD spake unto Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
2 Speak unto the children of Israel, that they take for me an offering: of every man whose heart maketh him willing ye shall take my offering.
“Waambie Waisraeli waniletee sadaka. Utapokea sadaka kwa niaba yangu kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake wapenda kutoa.
3 And this is the offering which ye shall take of them; gold, and silver, and brass;
Hizi ndizo sadaka utakazozipokea kutoka kwao: dhahabu, fedha na shaba;
4 and blue, and purple, and scarlet, and fine linen, and goats’ [hair];
nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu, pamoja na kitani safi; singa za mbuzi;
5 and rams’ skins dyed red, and sealskins, and acacia wood;
ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
6 oil for the light, spices for the anointing oil, and for the sweet incense;
mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
7 onyx stones, and stones to be set, for the ephod, and for the breastplate.
na vito vya shohamu na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
8 And let them make me a sanctuary; that I may dwell among them.
“Kisha uwaamuru wanitengenezee mahali patakatifu, nami nitakaa miongoni mwao.
9 According to all that I shew thee, the pattern of the tabernacle, and the pattern of all the furniture thereof, even so shall ye make it.
Tengeneza hema hili na vyombo vyake vyote sawasawa na kielelezo nitakachokuonyesha.
10 And they shall make an ark of acacia wood: two cubits and a half shall be the length thereof, and a cubit and a half the breadth thereof, and a cubit and a half the height thereof.
“Nao watatengeneza Sanduku la mbao za mshita, lenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, upana wa dhiraa moja na nusu, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
11 And thou shalt overlay it with pure gold, within and without shalt thou overlay it, and shalt make upon it a crown of gold round about.
Utalifunika hilo Sanduku kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu juu yake kulizunguka.
12 And thou shalt cast four rings of gold for it, and put them in the four feet thereof; and two rings shall be on the one side of it, and two rings on the other side of it.
Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
13 And thou shalt make staves of acacia wood, and overlay them with gold.
Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
14 And thou shalt put the staves into the rings on the sides of the ark, to bear the ark withal.
Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
15 The staves shall be in the rings of the ark: they shall not be taken from it.
Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa.
16 And thou shalt put into the ark the testimony which I shall give thee.
Kisha weka ndani ya hilo Sanduku ule Ushuhuda nitakaokupa.
17 And thou shalt make a mercy-seat of pure gold: two cubits and a half [shall be] the length thereof, and a cubit and a half the breadth thereof.
“Tengeneza kifuniko cha upatanisho cha dhahabu safi, chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, na upana wa dhiraa moja na nusu.
18 And thou shalt make two cherubim of gold; of beaten work shalt thou make them, at the two ends of the mercy-seat.
Tengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
19 And make one cherub at the one end, and one cherub at the other end: of one piece with the mercy-seat shall ye make the cherubim on the two ends thereof.
Tengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; watengeneze makerubi hao wawe kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
20 And the cherubim shall spread out their wings on high, covering the mercy-seat with their wings, with their faces one to another; toward the mercy-seat shall the faces of the cherubim be.
Makerubi hao watakuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, yakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao wataelekeana, wakitazama hicho kifuniko.
21 And thou shalt put the mercy-seat above upon the ark; and in the ark thou shalt put the testimony that I shall give thee.
Weka huo Ushuhuda nitakaokupa ndani ya hilo Sanduku la Agano, na uweke hicho kifuniko juu ya hilo Sanduku.
22 And there I will meet with thee, and I will commune with thee from above the mercy-seat, from between the two cherubim which are upon the ark of the testimony, of all things which I will give thee in commandment unto the children of Israel.
Hapo juu ya hicho kifuniko, kati ya hao makerubi wawili walioko juu ya hilo Sanduku la Ushuhuda, hapo ndipo nitakapokutana nawe na kukupa maagizo yangu kwa ajili ya Waisraeli.
23 And thou shalt make a table of acacia wood: two cubits [shall be] the length thereof, and a cubit the breadth thereof, and a cubit and a half the height thereof.
“Tengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
24 And thou shalt overlay it with pure gold, and make thereto a crown of gold round about.
Ifunike kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
25 And thou shalt make unto it a border of an handbreadth round about, and thou shalt make a golden crown to the border thereof round about.
Kisha tengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na ufanyie ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
26 And thou shalt make for it four rings of gold, and put the rings in the four corners that are on the four feet thereof.
Tengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na uzifungie kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
27 Close by the border shall the rings be, for places for the staves to bear the table.
Pete hizo zitakuwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko itakayotumika kuibebea hiyo meza.
28 And thou shalt make the staves of acacia wood, and overlay them with gold, that the table may be borne with them.
Tengeneza mipiko hiyo kwa mbao za mshita, uifunike na dhahabu, uitumie kubeba hiyo meza.
29 And thou shalt make the dishes thereof, and the spoons thereof, and the flagons thereof, and the bowls thereof, to pour out withal: of pure gold shalt thou make them.
Tengeneza sahani zake na masinia yake kwa dhahabu safi, pamoja na bilauri na bakuli zake kwa ajili ya kumiminia sadaka.
30 And thou shalt set upon the table shewbread before me alway.
Utaweka mikate ya Wonyesho juu ya meza hii iwe mbele yangu daima.
31 And thou shalt make a candlestick of pure gold: of beaten work shall the candlestick be made, even its base, and its shaft; its cups, its knops, and its flowers, shall be of one piece with it:
“Tengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vinavyofanana na ua, matovu yake na maua yake viwe kitu kimoja.
32 and there shall be six branches going out of the sides thereof; three branches of the candlestick out of the one side thereof, and three branches of the candlestick out of the other side thereof:
Matawi sita yatatokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
33 three cups made like almond-blossoms in one branch, a knop and a flower; and three cups made like almond-blossoms in the other branch, a knop and a flower: so for the six branches going out of the candlestick:
Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vitakuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yanayotokeza kwenye kile kinara cha taa.
34 and in the candlestick four cups made like almond-blossoms, the knops thereof, and the flowers thereof:
Juu ya kinara chenyewe vitakuwepo vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
35 and a knop under two branches of one piece with it, and a knop under two branches of one piece with it, and a knop under two branches of one piece with it, for the six branches going out of the candlestick.
Tovu moja litakuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani matawi sita kwa jumla.
36 Their knops and their branches shall be of one piece with it: the whole of it one beaten work of pure gold.
Matovu na matawi yote yatakuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakifuliwa kwa dhahabu safi.
37 And thou shalt make the lamps thereof, seven: and they shall light the lamps thereof, to give light over against it.
“Kisha tengeneza taa zake saba na uziweke juu ya kinara hicho ili ziangaze mbele yake.
38 And the tongs thereof, and the snuffdishes thereof, shall be of pure gold.
Mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote zitakuwa za dhahabu safi.
39 Of a talent of pure gold shall it be made, with all these vessels.
Utatumia talanta moja ya dhahabu safi kutengeneza hicho kinara na vifaa vyake vyote.
40 And see that thou make them after their pattern, which hath been shewed thee in the mount.
Hakikisha kuwa umevitengeneza sawasawa na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani.

< Exodus 25 >