< Ecclesiastes 11 >

1 Cast thy bread upon the waters: for thou shalt find it after many days.
Tupa mkate wako juu ya maji, kwa maana baada ya siku nyingi utaupata tena.
2 Give a portion to seven, yea, even unto eight; for thou knowest not what evil shall be upon the earth.
Wape sehemu watu saba, naam hata wanane, kwa maana hujui ni baa gani litakalokuwa juu ya nchi.
3 If the clouds be full of rain, they empty themselves upon the earth: and if a tree fall toward the south, or toward the north, in the place where the tree falleth, there shall it be.
Kama mawingu yamejaa maji, hunyesha mvua juu ya nchi. Kama mti ukianguka kuelekea kusini au kuelekea kaskazini, mahali ulipoangukia, hapo ndipo utakapolala.
4 He that observeth the wind shall not sow; and he that regardeth the clouds shall not reap.
Yeyote atazamaye upepo hatapanda, yeyote aangaliaye mawingu hatavuna.
5 As thou knowest not what is the way of the wind, [nor] how the bones [do grow] in the womb of her that is with child; even so thou knowest not the work of God who doeth all.
Kama vile usivyofahamu njia ya upepo, au jinsi mwili uumbwavyo ndani ya tumbo la mama, vivyo hivyo huwezi kufahamu kazi ya Mungu, Muumba wa vitu vyote.
6 In the morning sow thy seed, and in the evening withhold not thine hand: for thou knowest not which shall prosper, whether this or that, or whether they both shall be alike good.
Panda mbegu yako asubuhi, nako jioni usiruhusu mikono yako ilegee, kwa maana hujui ni ipi itakayofanikiwa, kwamba ni hii au ni ile, au kwamba zote zitafanikiwa sawasawa.
7 Truly the light is sweet, and a pleasant thing it is for the eyes to behold the sun.
Nuru ni tamu, tena inafurahisha macho kuona jua.
8 Yea, if a man live many years, let him rejoice in them all; but let him remember the days of darkness, for they shall be many. All that cometh is vanity.
Hata kama mtu ataishi miaka mingi kiasi gani, na aifurahie yote. Lakini na akumbuke siku za giza, kwa maana zitakuwa nyingi. Kila kitu kitakachokuja ni ubatili.
9 Rejoice, O young man, in thy youth; and let thy heart cheer thee in the days of thy youth, and walk in the ways of thine heart, and in the sight of thine eyes: but know thou, that for all these things God will bring thee into judgment.
Furahi ewe kijana, wakati ungali kijana, moyo wako na ukupe furaha katika siku za ujana wako. Fuata njia za moyo wako na chochote macho yako yaonayo, lakini ujue kwamba kwa ajili ya haya yote Mungu atakuleta hukumuni.
10 Therefore remove sorrow from thy heart, and put away evil from thy flesh: for youth and the prime of life are vanity.
Kwa hiyo basi, ondoa wasiwasi moyoni mwako na utupilie mbali masumbufu ya mwili wako, kwa kuwa ujana na nguvu ni ubatili.

< Ecclesiastes 11 >