< Deuteronomy 1 >

1 These be the words which Moses spake unto all Israel beyond Jordan in the wilderness, in the Arabah over against Suph, between Paran, and Tophel, and Laban, and Hazeroth, and Di-zahab.
Haya ni maneno Mose aliyoyasema kwa Israeli yote jangwani mashariki ya Yordani, ambayo iko Araba, inayokabiliana na Sufu, kati ya Parani na Tofeli, Labani, Haserothi na Dizahabu.
2 It is eleven days’ [journey] from Horeb by the way of mount Seir unto Kadesh-barnea.
(Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka Horebu kwa njia ya Mlima Seiri mpaka Kadesh-Barnea.)
3 And it came to pass in the fortieth year, in the eleventh month, on the first day of the month, that Moses spake unto the children of Israel, according unto all that the LORD had given him in commandment unto them;
Katika mwaka wa arobaini, siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, Mose aliwatangazia Waisraeli yale yote Bwana aliyomwamuru kuwahusu.
4 after he had smitten Sihon the king of the Amorites, which dwelt in Heshbon, and Og the king of Bashan, which dwelt in Ashtaroth, at Edrei:
Hii ilikuwa baada ya kumshinda Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, na pia huko Edrei alikuwa amemshinda Ogu mfalme wa Bashani, ambaye alitawala huko Ashtarothi.
5 beyond Jordan, in the land of Moab, began Moses to declare this law, saying,
Huko mashariki ya Yordani katika nchi ya Moabu, Mose alianza kuielezea sheria hii, akisema:
6 The LORD our God spake unto us in Horeb, saying, Ye have dwelt long enough in this mountain:
Bwana Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, “Mmekaa vya kutosha katika mlima huu.
7 turn you, and take your journey, and go to the hill country of the Amorites, and unto all [the places] nigh thereunto, in the Arabah, in the hill country, and in the lowland, and in the South, and by the sea shore, the land of the Canaanites, and Lebanon, as far as the great river, the river Euphrates.
Vunjeni kambi, msonge mbele kuelekea nchi ya vilima ya Waamori; nendeni kwa watu wote ambao ni majirani wa Araba, katika milima, upande wa magharibi chini ya vilima, katika Negebu na kandokando ya pwani, mpaka nchi ya Wakanaani hadi Lebanoni, na kufika mto mkubwa Frati.
8 Behold, I have set the land before you: go in and possess the land which the LORD sware unto your fathers, to Abraham, to Isaac, and to Jacob, to give unto them and to their seed after them.
Tazama, nimewapa ninyi nchi hii. Ingieni mkaimiliki nchi ambayo Bwana aliapa kuwa angaliwapa baba zenu, Abrahamu, Isaki na Yakobo, pamoja na vizazi vyao baada yao.”
9 And I spake unto you at that time, saying, I am not able to bear you myself alone:
Wakati ule niliwaambia, “Ninyi mmekuwa mzigo mzito sana kwangu kuwachukua peke yangu.
10 The LORD your God hath multiplied you, and, behold, ye are this day as the stars of heaven for multitude.
Bwana Mungu wenu ameongeza hesabu yenu, hivi kwamba leo ninyi ni wengi kama nyota za angani.
11 The LORD, the God of your fathers, make you a thousand times so many more as ye are, and bless you, as he hath promised you!
Naye Bwana, Mungu wa baba zenu na awaongeze mara elfu na kuwabariki kama alivyoahidi!
12 How can I myself alone bear your cumbrance, and your burden, and your strife?
Lakini mimi nitawezaje kubeba matatizo yenu, na mizigo yenu, na magomvi yenu peke yangu?
13 Take you wise men, and understanding, and known, according to your tribes, and I will make them heads over you.
Chagueni baadhi ya watu wenye hekima, wenye ufahamu na wanaoheshimika kutoka kila kabila lenu, nami nitawaweka juu yenu.”
14 And ye answered me, and said, The thing which thou hast spoken is good [for us] to do.
Mlinijibu, “Shauri ulilolitoa ni zuri.”
15 So I took the heads of your tribes, wise men, and known, and made them heads over you, captains of thousands, and captains of hundreds, and captains of fifties, and captains of tens, and officers, according to your tribes.
Kwa hiyo niliwachukua wanaume viongozi wa makabila yenu, wenye hekima na wanaoheshimika, nami nikawateua wawe na mamlaka juu yenu kama majemadari wa maelfu, wa mamia, wa hamsini, na wa makumi, na kama maafisa wa makabila.
16 And I charged your judges at that time, saying, Hear [the causes] between your brethren, and judge righteously between a man and his brother, and the stranger that is with him.
Nami wakati ule nikawaagiza waamuzi wenu: Sikilizeni magomvi kati ya ndugu zenu na mwamue kwa haki, hata kama shauri ni kati ya ndugu wa Kiisraeli, au kati ya mmoja wa ndugu wa Kiisraeli na mgeni.
17 Ye shall not respect persons in judgment; ye shall hear the small and the great alike; ye shall not be afraid of the face of man; for the judgment is God’s: and the cause that is too hard for you ye shall bring unto me, and I will hear it.
Msionyeshe upendeleo katika maamuzi; wasikilizeni wote sawasawa, wadogo kwa wakubwa. Msimwogope mtu yeyote, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Mniletee mimi shauri lolote lililo gumu sana kwenu, nami nitalisikiliza.
18 And I commanded you at that time all the things which ye should do.
Nami wakati ule niliwaambia kila kitu ambacho mngefanya.
19 And we journeyed from Horeb, and went through all that great and terrible wilderness which ye saw, by the way to the hill country of the Amorites, as the LORD our God commanded us; and we came to Kadesh-barnea.
Kisha, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru, tuliondoka kutoka Horebu na kwenda kuelekea nchi ya vilima ya Waamori, kupitia jangwa lile kubwa lote la kutisha, lile mliloliona, nasi tukafika Kadesh-Barnea.
20 And I said unto you, Ye are come unto the hill country of the Amorites, which the LORD our God giveth unto us.
Kisha niliwaambia, “Mmefika katika nchi ya vilima ya Waamori, ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.
21 Behold, the LORD thy God hath set the land before thee: go up, take possession, as the LORD, the God of thy fathers, hath spoken unto thee; fear not, neither be dismayed.
Tazama, Bwana Mungu wenu amewapa nchi. Pandeni mkaimiliki kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaambia. Msiogope, wala msikate tamaa.”
22 And ye came near unto me every one of you, and said, Let us send men before us, that they may search the land for us, and bring us word again of the way by which we must go up, and the cities unto which we shall come.
Ndipo ninyi nyote mkanijia na kusema, “Tupeleke watu watutangulie kuipeleleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea taarifa kuhusu njia tutakayopita, na miji tutakayoiendea.”
23 And the thing pleased me well: and I took twelve men of you, one man for every tribe:
Wazo hilo lilionekana zuri kwangu; kwa hiyo niliwachagua watu wenu kumi na wawili, mwanaume mmoja kutoka kila kabila.
24 and they turned and went up into the mountain, and came unto the valley of Eshcol, and spied it out.
Waliondoka na kukwea katika nchi ya vilima, wakafika katika Bonde la Eshkoli na kuipeleleza.
25 And they took of the fruit of the land in their hands, and brought it down unto us, and brought us word again, and said, It is a good land which the LORD our God giveth unto us.
Wakachukua baadhi ya matunda ya nchi, wakatuletea na kutuarifu, “Ni nchi nzuri ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.”
26 Yet ye would not go up, but rebelled against the commandment of the LORD your God:
Lakini hamkuwa tayari kukwea, mkaasi dhidi ya amri ya Bwana Mungu wenu.
27 and ye murmured in your tents, and said, Because the LORD hated us, he hath brought us forth out of the land of Egypt, to deliver us into the hand of the Amorites, to destroy us.
Mkanungʼunika ndani ya mahema yenu na kusema, “Bwana anatuchukia, kwa hiyo alitutoa Misri ili kututia mikononi mwa Waamori kutuangamiza.
28 Whither are we going up? our brethren have made our heart to melt, saying, The people is greater and taller than we; the cities are great and fenced up to heaven; and moreover we have seen the sons of the Anakim there.
Twende wapi? Ndugu zetu wametufanya kufa moyo. Wanasema, ‘Watu wa huko wana nguvu zaidi na ni warefu kuliko sisi tulivyo; miji ni mikubwa, yenye kuta zilizofika juu angani. Zaidi ya hayo, tumewaona Waanaki huko.’”
29 Then I said unto you, Dread not, neither be afraid of them.
Ndipo nikawaambia, “Msihofu, wala msiwaogope.
30 The LORD your God who goeth before you, he shall fight for you, according to all that he did for you in Egypt before your eyes;
Bwana Mungu wenu anayewatangulia, atawapigania, kama alivyofanya kwa ajili yenu huko Misri, mbele ya macho yenu hasa,
31 and in the wilderness, where thou hast seen how that the LORD thy God bare thee, as a man doth bear his son, in all the way that ye went, until ye came unto this place.
na pia huko jangwani. Huko mliona jinsi Bwana Mungu wenu alivyowachukua, kama baba amchukuavyo mwanawe, katika njia yote mliyoiendea mpaka mkafika mahali hapa.”
32 Yet in this thing ye did not believe the LORD your God,
Pamoja na hili, hamkumtegemea Bwana Mungu wenu,
33 who went before you in the way, to seek you out a place to pitch your tents in, in fire by night, to shew you by what way ye should go, and in the cloud by day.
ambaye aliwatangulia katika safari yenu, kwa moto usiku na kwa wingu mchana, kuwatafutia mahali penu pa kupiga kambi na kuwaonyesha njia mtakayoiendea.
34 And the LORD heard the voice of your words, and was wroth, and sware, saying,
Wakati Bwana aliposikia lile mlilosema, alikasirika, akaapa, akasema:
35 Surely there shall not one of these men of this evil generation see the good land, which I sware to give unto your fathers,
“Hakuna mtu wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kuwapa baba zenu,
36 save Caleb the son of Jephunneh, he shall see it; and to him will I give the land that he hath trodden upon, and to his children: because he hath wholly followed the LORD.
isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wazao wake nchi aliyoikanyaga kwa miguu, kwa sababu alimfuata Bwana kwa moyo wote.”
37 Also the LORD was angry with me for your sakes, saying, Thou also shalt not go in thither:
Kwa sababu yenu Bwana pia alinikasirikia mimi, akasema, “Hutaingia hiyo nchi pia.
38 Joshua the son of Nun, which standeth before thee, he shall go in thither: encourage thou him; for he shall cause Israel to inherit it.
Lakini msaidizi wako, Yoshua mwana wa Nuni, ataingia. Mtie moyo, kwa sababu atawaongoza Waisraeli kuirithi hiyo nchi.
39 Moreover your little ones, which ye said should be a prey, and your children, which this day have no knowledge of good or evil, they shall go in thither, and unto them will I give it, and they shall possess it.
Wale watoto ambao mliwasema wangelichukuliwa mateka, yaani watoto wenu ambao bado hawajui jema na baya, wataingia katika nchi. Nitawapa hiyo nchi, nao wataimiliki.
40 But as for you, turn you, and take your journey into the wilderness by the way to the Red Sea.
Bali ninyi geukeni, mwondoke kuelekea jangwani kwa kufuata njia ya Bahari ya Shamu.”
41 Then ye answered and said unto me, We have sinned against the LORD, we will go up and fight, according to all that the LORD our God commanded us. And ye girded on every man his weapons of war, and were forward to go up into the mountain.
Ndipo mkanijibu, “Tumemtenda Bwana dhambi. Tutakwenda kupigana, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru.” Hivyo kila mmoja wenu akachukua silaha zake, huku mkifikiri kuwa ni rahisi kukwea katika nchi ya vilima.
42 And the LORD said unto me, Say unto them, Go not up, neither fight; for I am not among you; lest ye be smitten before your enemies.
Lakini Bwana aliniambia, “Waambie, ‘Msipande kupigana, kwa sababu sitakuwa pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu.’”
43 So I spake unto you, and ye hearkened not; but ye rebelled against the commandment of the LORD, and were presumptuous, and went up into the mountain.
Hivyo niliwaambia, lakini hamkutaka kusikia. Mliasi dhidi ya amri ya Bwana, na katika kiburi chenu mlienda katika nchi ya vilima.
44 And the Amorites, which dwelt in that mountain, came out against you, and chased you, as bees do, and beat you down in Seir, even unto Hormah.
Waamori ambao waliishi katika vilima hivyo waliinuka dhidi yenu, wakawafukuza kama kundi la nyuki wakiwapiga njia yote ya Seiri mpaka Horma.
45 And ye returned and wept before the LORD; but the LORD hearkened not to your voice, nor gave ear unto you.
Mlirudi na kulia mbele za Bwana, lakini Mungu hakusikiliza kilio chenu, wala hakuwajali.
46 So ye abode in Kadesh many days, according unto the days that ye abode [there].
Hivyo mlikaa Kadeshi kwa siku nyingi, kwa muda ule wote mliokaa huko.

< Deuteronomy 1 >