< Deuteronomy 8 >

1 All the commandment which I command thee this day shall ye observe to do, that ye may live, and multiply, and go in and possess the land which the LORD sware unto your fathers.
Uwe mwangalifu kufuata kila agizo ninalokupa wewe leo, ili mweze kuishi, kuongezeka na mweze kuingia mkamiliki nchi ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zenu.
2 And thou shalt remember all the way which the LORD thy God hath led thee these forty years in the wilderness, that he might humble thee, to prove thee, to know what was in thine heart, whether thou wouldest keep his commandments, or no.
Kumbuka jinsi Bwana Mungu wenu alivyowaongoza katika njia yote katika jangwa kwa miaka hii arobaini, kukunyenyekeza na kukujaribu ili ajue lililoko moyoni mwako, kwamba utayashika maagizo yake au la.
3 And he humbled thee, and suffered thee to hunger, and fed thee with manna, which thou knewest not, neither did thy fathers know; that he might make thee know that man doth not live by bread only, but by every thing that proceedeth out of the mouth of the LORD doth man live.
Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Bwana.
4 Thy raiment waxed not old upon thee, neither did thy foot swell, these forty years.
Nguo zenu hazikuchakaa wala miguu yenu haikuvimba kwa miaka hii arobaini.
5 And thou shalt consider in thine heart, that, as a man chasteneth his son, so the LORD thy God chasteneth thee.
Mjue basi ndani ya mioyo yenu kama mtu anavyomwadibisha mwanawe, ndivyo Bwana Mungu wako atawaadibisha ninyi.
6 And thou shalt keep the commandments of the LORD thy God, to walk in his ways, and to fear him.
Shikeni maagizo ya Bwana Mungu wenu mtembee katika njia zake na kumheshimu.
7 For the LORD thy God bringeth thee into a good land, a land of brooks of water, of fountains and depths, springing forth in valleys and hills;
Kwa kuwa Bwana Mungu wenu anawaleta katika nchi nzuri, nchi yenye vijito na mabwawa ya maji, yenye chemchemi zinazotiririka mabondeni na katika vilima;
8 a land of wheat and barley, and vines and fig trees and pomegranates; a land of oil olives and honey;
nchi yenye ngano na shayiri, mizabibu na mitini, mikomamanga, mafuta ya zeituni na asali;
9 a land wherein thou shalt eat bread without scarceness, thou shalt not lack any thing in it; a land whose stones are iron, and out of whose hills thou mayest dig brass.
nchi ambayo chakula hakitapungua na hamtakosa chochote; nchi ambayo miamba yake ni chuma na mnaweza kuchimba shaba kutoka kwenye vilima.
10 And thou shalt eat and be full, and thou shalt bless the LORD thy God for the good land which he hath given thee.
Wakati mtakapokwisha kula na kushiba, msifuni Bwana Mungu wenu kwa ajili ya nchi nzuri aliyowapa.
11 Beware lest thou forget the LORD thy God, in not keeping his commandments, and his judgments, and his statutes, which I command thee this day:
Jihadharini msimsahau Bwana Mungu wenu, mkashindwa kushika maagizo yake, sheria na amri zake ambazo ninawapa leo.
12 lest when thou hast eaten and art full, and hast built goodly houses, and dwelt therein;
Angalia wakati mtakapokuwa mmekula na kushiba, mkajenga nyumba nzuri na kukaa humo,
13 and when thy herds and thy flocks multiply, and thy silver and thy gold is multiplied, and all that thou hast is multiplied;
na wakati makundi yenu ya ngʼombe na mbuzi na kondoo yatakapoongezeka na fedha na dhahabu yenu itakapoongezeka na vyote mlivyo navyo vitakapozidishwa,
14 then thine heart be lifted up, and thou forget the LORD thy God, which brought thee forth out of the land of Egypt, out of the house of bondage;
basi mioyo yenu isiwe na kiburi mkamsahau Bwana Mungu wenu aliyewatoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
15 who led thee through the great and terrible wilderness, [wherein were] fiery serpents and scorpions, and thirsty ground where was no water; who brought thee forth water out of the rock of flint;
Aliwaongoza kupitia jangwa lile kubwa na la kutisha, nchi ile ya kiu isiyo na maji, yenye nyoka wa sumu na nge. Aliwatolea maji kutoka kwenye mwamba mgumu.
16 who fed thee in the wilderness with manna, which thy fathers knew not; that he might humble thee, and that he might prove thee, to do thee good at thy latter end:
Aliwapa mana ya kula jangwani, kitu ambacho baba zenu hawakukijua, ili kuwanyenyekesha na kuwajaribu ninyi ili mwishoni apate kuwatendea mema.
17 and thou say in thine heart, My power and the might of mine hand hath gotten me this wealth.
Mnaweza kusema, “Uwezo wangu na nguvu za mikono yangu ndizo zilizonipatia utajiri huu.”
18 But thou shalt remember the LORD thy God, for it is he that giveth thee power to get wealth; that he may establish his covenant which he sware unto thy fathers, as at this day.
Lakini kumbukeni Bwana Mungu wenu, ndiye ambaye huwapa uwezo wa kupata utajiri, na hivyo kulithibitisha Agano lake, ambalo aliwaapia baba zenu, kama ilivyo leo.
19 And it shall be, if thou shalt forget the LORD thy God, and walk after other gods, and serve them, and worship them, I testify against you this day that ye shall surely perish.
Ikiwa mtamsahau Bwana Mungu wenu, mkaifuata miungu mingine, mkaiabudu na kuisujudia, ninashuhudia dhidi yenu leo kwamba hakika mtaangamizwa.
20 As the nations which the LORD maketh to perish before you, so shall ye perish; because ye would not hearken unto the voice of the LORD your God.
Kama mataifa Bwana aliyoyaangamiza mbele yenu, ndivyo ninyi mtakavyoangamizwa kwa kutokumtii Bwana Mungu wenu.

< Deuteronomy 8 >