< Deuteronomy 33 >

1 And this is the blessing, wherewith Moses the man of God blessed the children of Israel before his death.
Hii ndiyo baraka Mose mtu wa Mungu aliyotamka kwa Waisraeli kabla ya kifo chake.
2 And he said, The LORD came from Sinai, And rose from Seir unto them; He shined forth from mount Paran, And he came from the ten thousands of holy ones: At his right hand was a fiery law unto them.
Alisema: “Bwana alikuja kutoka Mlima Sinai, akachomoza kama jua juu yao kutoka Mlima Seiri, akaangaza kutoka Mlima Parani. Alikuja pamoja na watakatifu makumi elfu kutoka kusini, kutoka materemko ya mlima wake.
3 Yea, he loveth the peoples; All his saints are in thy hand: And they sat down at thy feet; [Every one] shall receive of thy words.
Hakika ni wewe ambaye huwapenda watu, watakatifu wako wote wamo mkononi mwako. Miguuni pako wote wanasujudu na kutoka kwako wanapokea mafundisho,
4 Moses commanded us a law, An inheritance for the assembly of Jacob.
sheria ile Mose aliyotupa sisi, tulio milki ya kusanyiko la Yakobo.
5 And he was king in Jeshurun, When the heads of the people were gathered, All the tribes of Israel together.
Alikuwa mfalme juu ya Yeshuruni wakati viongozi wa watu walipokusanyika, pamoja na makabila ya Israeli.
6 Let Reuben live, and not die; Yet let his men be few.
“Reubeni na aishi, asife, wala watu wake wasiwe wachache.”
7 And this is [the blessing] of Judah: and he said, Hear, LORD, the voice of Judah, And bring him in unto his people: With his hands he contended for himself; And thou shalt be an help against his adversaries.
Akasema hili kuhusu Yuda: “Ee Bwana, sikia kilio cha Yuda, mlete kwa watu wake. Kwa mikono yake mwenyewe hujitetea. Naam, uwe msaada wake dhidi ya adui zake!”
8 And of Levi he said, Thy Thummim and thy Urim are with thy godly one, Whom thou didst prove at Massah, With whom thou didst strive at the waters of Meribah;
Kuhusu Lawi alisema: “Thumimu yako na Urimu yako ulimpa, mtu yule uliyemfadhili. Ulimjaribu huko Masa na kushindana naye kwenye maji ya Meriba.
9 Who said of his father, and of his mother, I have not seen him; Neither did he acknowledge his brethren, Nor knew he his own children: For they have observed thy word, And keep thy covenant.
Alinena hivi kuhusu baba yake na mama yake, ‘Mimi siwahitaji kamwe.’ Akawasahau jamaa zake, asiwatambue hata watoto wake, lakini akaliangalia neno lako na kulilinda Agano lako.
10 They shall teach Jacob thy judgments, And Israel thy law: They shall put incense before thee, And whole burnt offering upon thine altar.
Humfundisha Yakobo mausia yako na Israeli sheria yako. Hufukiza uvumba mbele zako na sadaka nzima za kuteketezwa juu ya madhabahu yako.
11 Bless, LORD, his substance, And accept the work of his hands: Smite through the loins of them that rise up against him, And of them that hate him, that they rise not again.
Ee Bwana, bariki ustadi wake wote, nawe upendezwe na kazi ya mikono yake. Vipige viuno vya wale wainukao dhidi yake; wapige adui zake hata wasiinuke tena.”
12 Of Benjamin he said, The beloved of the LORD shall dwell in safety by him; He covereth him all the day long, And he dwelleth between his shoulders.
Kuhusu Benyamini akasema: “Mwache mpenzi wa Bwana apumzike salama kwake, kwa maana humkinga mchana kutwa, na yule Bwana ampendaye hupumzika kati ya mabega yake.”
13 And of Joseph he said, Blessed of the LORD be his land; For the precious things of heaven, for the dew, And for the deep that coucheth beneath,
Kuhusu Yosefu akasema: “Bwana na aibariki nchi yake kwa umande wa thamani kutoka mbinguni juu, na vilindi vya maji vilivyotulia chini;
14 And for the precious things of the fruits of the sun, And for the precious things of the growth of the moons,
pamoja na vitu vilivyo bora sana viletwavyo na jua, na vitu vizuri sana vinavyoweza kutolewa na mwezi;
15 And for the chief things of the ancient mountains, And for the precious things of the everlasting hills,
pamoja na zawadi bora sana za milima ya zamani na kwa wingi wa baraka za vilima vya milele;
16 And for the precious things of the earth and the fulness thereof, And the good will of him that dwelt in the bush: Let [the blessing] come upon the head of Joseph, And upon the crown of the head of him that was separate from his brethren.
pamoja na baraka nzuri mno za ardhi na ukamilifu wake, na upendeleo wake yeye aliyeishi kwenye kichaka kilichokuwa kinawaka moto. Hivi vyote na vikae juu ya kichwa cha Yosefu, juu ya paji la uso la aliye mkuu miongoni mwa ndugu zake.
17 The firstling of his bullock, majesty is his; And his horns are the horns of the wild-ox: With them he shall push the peoples all of them, [even] the ends of the earth: And they are the ten thousands of Ephraim, And they are the thousands of Manasseh.
Katika fahari yeye ni kama fahali mzaliwa wa kwanza; pembe zake ni pembe za nyati, na kwa pembe hizo atapiga mataifa, hata yaliyo miisho ya dunia. Hivyo ndivyo yalivyo makumi elfu ya Efraimu; hivyo ndivyo yalivyo maelfu ya Manase.”
18 And of Zebulun he said, Rejoice, Zebulun, in thy going out; And, Issachar, in thy tents.
Kuhusu Zabuloni akasema: “Shangilia, Zabuloni, wakati wa kutoka nje, nawe Isakari, katika mahema yako.
19 They shall call the peoples unto the mountain; There shall they offer sacrifices of righteousness: For they shall suck the abundance of the seas, And the hidden treasures of the sand.
Watawaita mataifa kwenye mlima, na huko mtatoa dhabihu za haki; watajifurahisha kwa wingi uliojaza bahari, kwa hazina zilizofichwa mchangani.”
20 And of Gad he said, Blessed be he that enlargeth Gad: He dwelleth as a lioness, And teareth the arm, yea, the crown of the head.
Kuhusu Gadi akasema: “Atabarikiwa yeye aongezaye milki ya Gadi! Gadi huishi huko kama simba, akirarua kwenye mkono au kichwa.
21 And he provided the first part for himself, For there was the lawgiver’s portion reserved; And he came [with] the heads of the people, He executed the justice of the LORD, And his judgments with Israel.
Alijichagulia nchi nzuri kuliko zote kwa ajili yake mwenyewe; fungu la kiongozi lilikuwa limehifadhiwa kwa ajili yake. Viongozi wa watu walipokusanyika, alitimiza haki ya mapenzi ya Bwana, na hukumu zake kuhusu Israeli.”
22 And of Dan he said, Dan is a lion’s whelp, That leapeth forth from Bashan.
Kuhusu Dani akasema: “Dani ni mwana simba, akiruka kutoka Bashani.”
23 And of Naphtali he said, O Naphtali, satisfied with favour, And full with the blessing of the LORD: Possess thou the west and the south.
Kuhusu Naftali akasema: “Naftali amejaa tele upendeleo wa Bwana, naye amejaa baraka yake; atarithi magharibi na kusini.”
24 And of Asher he said, Blessed be Asher with children; Let him be acceptable unto his brethren, And let him dip his foot in oil.
Kuhusu Asheri akasema: “Aliyebarikiwa zaidi sana katika wana ni Asheri; yeye na apate upendeleo kwa ndugu zake, yeye na anawe miguu yake kwenye mafuta.
25 Thy bars shall be iron and brass; And as thy days, so shall thy strength be.
Makomeo ya malango yako yawe chuma na shaba, nazo nguvu zako zitakuwa sawa na siku zako.
26 There is none like unto God, O Jeshurun, Who rideth upon the heaven for thy help, And in his excellency on the skies.
“Hakuna mwingine kama Mungu wa Yeshuruni, ambaye hupanda juu ya mbingu ili akusaidie, na juu ya mawingu katika utukufu wake.
27 The eternal God is [thy] dwelling place, And underneath are the everlasting arms: And he thrust out the enemy from before thee, And said, Destroy.
Mungu wa milele ni kimbilio lako, na chini kuna mikono ya milele. Atamfukuza adui yako mbele yako, akisema, ‘Mwangamize yeye!’
28 And Israel dwelleth in safety, The fountain of Jacob alone, In a land of corn and wine; Yea, his heavens drop down dew.
Hivyo Israeli ataishi salama peke yake. Mzao wa Yakobo ni salama katika nchi ya nafaka na divai mpya, mahali ambapo mbingu hudondosha umande.
29 Happy art thou, O Israel: Who is like unto thee, a people saved by the LORD, The shield of thy help, And that is the sword of thy excellency! And thine enemies shall submit themselves unto thee; And thou shalt tread upon their high places.
Ee Israeli, wewe umebarikiwa! Ni nani kama wewe, taifa lililookolewa na Bwana? Yeye ni ngao yako na msaada wako, na upanga wako uliotukuka. Adui zako watatetemeka mbele yako, nawe utapakanyaga mahali pao pa juu.”

< Deuteronomy 33 >