< Deuteronomy 3 >

1 Then we turned, and went up the way to Bashan: and Og the king of Bashan came out against us, he and all his people, unto battle at Edrei.
Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
2 And the LORD said unto me, Fear him not: for I have delivered him, and all his people, and his land, into thy hand; and thou shalt do unto him as thou didst unto Sihon king of the Amorites, which dwelt at Heshbon.
Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
3 So the LORD our God delivered into our hand Og also, the king of Bashan, and all his people: and we smote him until none was left to him remaining.
Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
4 And we took all his cities at that time; there was not a city which we took not from them; threescore cities, all the region of Argob, the kingdom of Og in Bashan.
Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
5 All these were cities fenced with high walls, gates, and bars; beside the unwalled towns a great many.
Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
6 And we utterly destroyed them, as we did unto Sihon king of Heshbon, utterly destroying every inhabited city, with the women and the little ones.
Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
7 But all the cattle, and the spoil of the cities, we took for a prey unto ourselves.
Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
8 And we took the land at that time out of the hand of the two kings of the Amorites that were beyond Jordan, from the valley of Arnon unto mount Hermon;
Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
9 ([which] Hermon the Sidonians call Sirion, and the Amorites call it Senir; )
(Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
10 all the cities of the plain, and all Gilead, and all Bashan, unto Salecah and Edrei, cities of the kingdom of Og in Bashan.
Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
11 (For only Og king of Bashan remained of the remnant of the Rephaim; behold, his bedstead was a bedstead of iron; is it not in Rabbah of the children of Ammon? nine cubits was the length thereof, and four cubits the breadth of it, after the cubit of a man.)
(Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
12 And this land we took in possession at that time: from Aroer, which is by the valley of Arnon, and half the hill country of Gilead, and the cities thereof, gave I unto the Reubenites and to the Gadites:
Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
13 and the rest of Gilead, and all Bashan, the kingdom of Og, gave I unto the half tribe of Manasseh; all the region of Argob, even all Bashan. (The same is called the land of Rephaim.
Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
14 Jair the son of Manasseh took all the region of Argob, unto the border of the Geshurites and the Maacathites; and called them, even Bashan, after his own name, Havvoth-jair, unto this day.)
Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
15 And I gave Gilead unto Machir.
Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
16 And unto the Reubenites and unto the Gadites I gave from Gilead even unto the valley of Arnon, the middle of the valley, and the border [thereof]; even unto the river Jabbok, which is the border of the children of Ammon;
Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
17 the Arabah also, and Jordan and the border [thereof], from Chinnereth even unto the sea of the Arabah, the Salt Sea, under the slopes of Pisgah eastward.
Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
18 And I commanded you at that time, saying, The LORD your God hath given you this land to possess it: ye shall pass over armed before your brethren the children of Israel, all the men of valour.
Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
19 But your wives, and your little ones, and your cattle, (I know that ye have much cattle, ) shall abide in your cities which I have given you;
Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
20 until the LORD give rest unto your brethren, as unto you, and they also possess the land which the LORD your God giveth them beyond Jordan: then shall ye return every man unto his possession, which I have given you.
mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
21 And I commanded Joshua at that time, saying, Thine eyes have seen all that the LORD your God hath done unto these two kings: so shall the LORD do unto all the kingdoms whither thou goest over.
Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
22 Ye shall not fear them: for the LORD your God, he it is that fighteth for you.
Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
23 And I besought the LORD at that time, saying,
Wakati huo nilimsihi Bwana:
24 O Lord GOD, thou hast begun to shew thy servant thy greatness, and thy strong hand: for what god is there in heaven or in earth, that can do according to thy works, and according to thy mighty acts?
“Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
25 Let me go over, I pray thee, and see the good land that is beyond Jordan, that goodly mountain, and Lebanon.
Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
26 But the LORD was wroth with me for your sakes, and hearkened not unto me: and the LORD said unto me, Let it suffice thee; speak no more unto me of this matter.
Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
27 Get thee up into the top of Pisgah, and lift up thine eyes westward, and northward, and southward, and eastward, and behold with thine eyes: for thou shalt not go over this Jordan.
Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
28 But charge Joshua, and encourage him, and strengthen him: for he shall go over before this people, and he shall cause them to inherit the land which thou shalt see.
Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
29 So we abode in the valley over against Beth-peor.
Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.

< Deuteronomy 3 >