< 2 Samuel 6 >

1 And David again gathered together all the chosen men of Israel, thirty thousand.
Tena Daudi akakusanya watu 30,000 wa Israeli waliochaguliwa.
2 And David arose, and went with all the people that were with him, from Baale Judah, to bring up from thence the ark of God, which is called by the Name, even the name of the LORD of hosts that sitteth upon the cherubim.
Yeye na watu wake wote wakatoka Baala ya Yuda kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka huko, linaloitwa kwa Jina, naam, jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, ambaye anaketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi walioko juu ya hilo Sanduku.
3 And they set the ark of God upon a new cart, and brought it out of the house of Abinadab that was in the hill: and Uzzah and Ahio, the sons of Abinadab, drave the new cart.
Wakaweka hilo Sanduku la Mungu juu ya gari jipya la kukokotwa na kulileta kutoka nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wana wa Abinadabu, walikuwa wakiongoza hilo gari jipya la kukokotwa
4 And they brought it out of the house of Abinadab, which was in the hill, with the ark of God: and Ahio went before the ark.
likiwa na Sanduku la Mungu juu yake, naye Ahio alikuwa anatembea akiwa mbele yake.
5 And David and all the house of Israel played before the LORD with all manner of [instruments made of] fir wood, and with harps, and with psalteries, and with timbrels, and with castanets, and with cymbals.
Daudi na nyumba yote ya Israeli walikuwa wanacheza mbele za Bwana kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, vinubi, zeze, matari, kayamba na matoazi.
6 And when they came to the threshing-floor of Nacon, Uzzah put forth [his hand] to the ark of God, and took hold of it; for the oxen stumbled.
Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Nakoni, Uza akanyoosha mkono na kulishika Sanduku la Mungu kwa sababu maksai walijikwaa.
7 And the anger of the LORD was kindled against Uzzah; and God smote him there for his error; and there he died by the ark of God.
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza kwa sababu ya kitendo chake cha kukosa heshima, kwa hiyo Mungu akampiga akafia papo hapo kando ya Sanduku la Mungu.
8 And David was displeased, because the LORD had broken forth upon Uzzah: and he called that place Perez-uzzah, unto this day.
Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, hivyo hadi leo mahali hapo panaitwa Peres-Uza.
9 And David was afraid of the LORD that day; and he said, How shall the ark of the LORD come unto me?
Daudi akamwogopa Bwana siku ile, akasema, “Ni jinsi gani Sanduku la Bwana litakavyoweza kunijia?”
10 So David would not remove the ark of the LORD unto him into the city of David; but David carried it aside into the house of Obed-edom the Gittite.
Hakuwa radhi kulichukua Sanduku la Bwana kwake katika Mji wa Daudi. Badala yake akalipeleka kwenye nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti.
11 And the ark of the LORD remained in the house of Obed-edom the Gittite three months: and the LORD blessed Obed-edom, and all his house.
Sanduku la Bwana likabaki katika nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti, kwa miezi mitatu, naye Bwana akambariki pamoja na nyumba yake yote.
12 And it was told king David, saying, The LORD hath blessed the house of Obed-edom, and all that pertaineth to him, because of the ark of God. And David went and brought up the ark of God from the house of Obed-edom into the city of David with joy.
Kisha Mfalme Daudi akaambiwa, “Bwana ameibariki nyumba ya Obed-Edomu pamoja na kila alicho nacho, kwa sababu ya Sanduku la Mungu.” Basi Daudi akateremka na kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka nyumba ya Obed-Edomu hadi Mji wa Daudi kwa shangwe.
13 And it was so, that when they that bare the ark of the LORD had gone six paces, he sacrificed an ox and a fatling.
Wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Bwana walipokuwa wametembea hatua sita, Daudi alitoa dhabihu fahali na ndama aliyenoneshwa.
14 And David danced before the LORD with all his might; and David was girded with a linen ephod.
Daudi, akiwa amevaa kisibau cha kitani, alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote,
15 So David and all the house of Israel brought up the ark of the LORD with shouting, and with the sound of the trumpet.
wakati yeye na nyumba yote ya Israeli walipopandisha Sanduku la Bwana kwa shangwe na sauti za tarumbeta.
16 And it was so, as the ark of the LORD came into the city of David, that Michal the daughter of Saul looked out at the window, and saw king David leaping and dancing before the LORD; and she despised him in her heart.
Ikawa Sanduku la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele za Bwana, akamdharau moyoni mwake.
17 And they brought in the ark of the LORD, and set it in its place, in the midst of the tent that David had pitched for it: and David offered burnt offerings and peace offerings before the LORD.
Wakaleta Sanduku la Bwana na kuliweka mahali pake ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.
18 And when David had made an end of offering the burnt offering and the peace offerings, he blessed the people in the name of the LORD of hosts.
Baada ya kumaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, Daudi akawabariki watu katika jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
19 And he dealt among all the people, even among the whole multitude of Israel, both to men and women, to every one a cake of bread, and a portion [of flesh], and a cake of raisins. So all the people departed every one to his house.
Kisha akatoa mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu kwa kila mtu katika mkutano wote wa Waisraeli, wanaume kwa wanawake. Nao watu wote wakaenda nyumbani kwao.
20 Then David returned to bless his household. And Michal the daughter of Saul came out to meet David, and said, How glorious was the king of Israel today, who uncovered himself today in the eyes of the handmaids of his servants, as one of the vain fellows shamelessly uncovereth himself!
Daudi aliporudi ili kuwabariki watu wa nyumbani mwake, Mikali binti Sauli akatoka nje kumlaki, akamwambia, “Tazama jinsi mfalme wa Israeli alivyojibainisha mwenyewe leo kwa kuvua mavazi yake machoni pa vijakazi wa watumishi wake, kama vile ambavyo mtu asiye na adabu angelifanya!”
21 And David said unto Michal, [It was] before the LORD, which chose me above thy father, and above all his house, to appoint me prince over the people of the LORD, over Israel: therefore will I play before the LORD.
Daudi akamwambia Mikali, “Nilifanya hivyo mbele za Bwana ambaye alinichagua mimi badala ya baba yako au mwingine yeyote kutoka nyumba yake wakati aliponiweka niwe mtawala juu ya Israeli, watu wa Bwana. Kwa hiyo nitacheza mbele za Bwana.
22 And I will be yet more vile than thus, and will be base in mine own sight: but of the handmaids which thou hast spoken of, of them shall I be had in honour.
Nitakuwa asiye na heshima zaidi kuliko sasa, nami nitajishusha machoni pangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliosema habari zao nitaheshimiwa.”
23 And Michal the daughter of Saul had no child unto the day of her death.
Naye Mikali binti Sauli hakuwa na watoto mpaka siku ya kufa kwake.

< 2 Samuel 6 >