< 1 Kings 6 >

1 And it came to pass in the four hundred and eightieth year after the children of Israel were come out of the land of Egypt, in the fourth year of Solomon’s reign over Israel, in the month Ziv, which is the second month, that he began to build the house of the LORD.
Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Solomoni katika Israeli, katika mwezi wa Zivu, ambao ndio mwezi wa pili, alianza kujenga Hekalu la Bwana.
2 And the house which king Solomon built for the LORD, the length thereof was threescore cubits, and the breadth thereof twenty [cubits], and the height thereof thirty cubits.
Hekalu hilo Mfalme Solomoni alilojenga kwa ajili ya Bwana lilikuwa na urefu wa dhiraa sitini, upana wa dhiraa ishirini na kimo cha dhiraa thelathini kwenda juu.
3 And the porch before the temple of the house, twenty cubits was the length thereof, according to the breadth of the house; [and] ten cubits was the breadth thereof before the house.
Baraza ya mbele ya Hekalu ilienea dhiraa ishirini kulingana na upana wa Hekalu na kujitokeza dhiraa kumi mbele ya Hekalu.
4 And for the house he made windows of fixed lattice-work.
Akatengeneza madirisha membamba yenye vidirisha vidogo vya juu katika Hekalu.
5 And against the wall of the house he built stories round about, against the walls of the house round about, both of the temple and of the oracle: and he made side-chambers round about:
Akafanyiza vyumba vya pembeni kulizunguka Hekalu lote vikishikamana na kuta za Hekalu na za Patakatifu pa Patakatifu.
6 The nethermost story was five cubits broad, and the middle was six cubits broad, and the third was seven cubits broad: for on the outside he made rebatements [in the wall] of the house round about, that [the beams] should not have hold in the walls of the house.
Ghorofa ya chini kabisa ilikuwa na upana wa dhiraa tano, ya kati ilikuwa dhiraa sita na ya tatu ilikuwa dhiraa saba. Kuzunguka ukuta wa nje wa Hekalu akapunguza ukuta pande zote ili boriti zisishikane kwenye kuta za Hekalu.
7 And the house, when it was in building, was built of stone made ready at the quarry: and there was neither hammer nor axe nor any tool of iron heard in the house, while it was in building.
Katika kujenga Hekalu, yalitumika tu mawe yaliyochongwa huko machimboni, wala hakuna nyundo, patasi au chombo kingine chochote cha chuma kilichosikika sauti yake katika eneo la ujenzi wa Hekalu wakati lilipokuwa likijengwa.
8 The door for the middle side-chambers was in the right side of the house: and they went up by winding stairs into the middle [chambers], and out of the middle into the third.
Ingilio la ghorofa ya chini kabisa lilikuwa upande wa kusini wa Hekalu, ngazi ilielekea ghorofa ya kati na kutokea hapo ilielekea hadi ghorofa ya tatu.
9 So he built the house, and finished it; and he covered the house with beams and planks of cedar.
Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha, akiliweka paa za boriti na mbao za mierezi.
10 And he built the stories against all the house, each five cubits high: and they rested on the house with timber of cedar.
Mfalme Solomoni akajenga vyumba vya pembeni kuzunguka Hekalu lote. Kimo cha kila kimoja kilikuwa dhiraa tano. Navyo vilikuwa vimeunganishwa na Hekalu kwa boriti za mierezi.
11 And the word of the LORD came to Solomon, saying,
Neno la Bwana likamjia Solomoni kusema:
12 Concerning this house which thou art in building, if thou wilt walk in my statutes, and execute my judgments, and keep all my commandments to walk in them; then will I establish my word with thee, which I spake unto David thy father.
“Kwa habari ya Hekalu hili unalojenga, kama ukifuata amri zangu, ukatunza masharti yangu na kushika maagizo yangu yote na kuyatii, kwa kupitia wewe nitatimiza ahadi niliyomwahidi Daudi baba yako.
13 And I will dwell among the children of Israel, and will not forsake my people Israel.
Nami nitakaa miongoni mwa Waisraeli, nami sitawaacha watu wangu Israeli.”
14 So Solomon built the house, and finished it.
Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha.
15 And he built the walls of the house within with boards of cedar; from the floor of the house unto the walls of the cieling, he covered them on the inside with wood: and he covered the floor of the house with boards of fir.
Akazifunika kuta zake za ndani kwa mbao za mierezi, akizipigilia ukutani kuanzia sakafuni mwa Hekalu hadi kwenye dari na kufunika sakafu ya Hekalu kwa mbao za misunobari.
16 And he built twenty cubits on the hinder part of the house with boards of cedar from the floor unto the walls: he even built [them] for it within, for an oracle, even for the most holy place.
Akagawa dhiraa ishirini sehemu ya nyuma ya Hekalu kwa mbao za mierezi kuanzia kwenye sakafu hadi darini ili kufanya sehemu takatifu ya ndani, yaani Patakatifu pa Patakatifu.
17 And the house, that is, the temple before [the oracle], was forty cubits [long].
Ukumbi mkubwa uliokuwa mbele ya chumba hiki ndio ulikuwa na urefu wa dhiraa arobaini.
18 And there was cedar on the house within, carved with knops and open flowers: all was cedar; there was no stone seen.
Hekalu ndani ilikuwa ya mierezi iliyonakshiwa mifano ya maboga na maua yaliyochanua. Kila kitu kilikuwa cha mwerezi, hakuna jiwe ambalo lilionekana.
19 And he prepared an oracle in the midst of the house within, to set there the ark of the covenant of the LORD.
Ndani ya Hekalu akatengeneza sehemu takatifu ya ndani, kwa ajili ya kuweka Sanduku la Agano la Bwana.
20 And within the oracle was [a space of] twenty cubits in length, and twenty cubits in breadth, and twenty cubits in the height thereof; and he overlaid it with pure gold: and he covered the altar with cedar.
Sehemu takatifu ya ndani ilikuwa na upana, urefu na kimo cha dhiraa ishirini ndani kwa ndani. Akaifunika ndani kwa dhahabu safi, pia akaifunika madhabahu ya mierezi vivyo hivyo.
21 So Solomon overlaid the house within with pure gold: and he drew chains of gold across before the oracle; and he overlaid it with gold.
Solomoni akaifunika sehemu ya ndani ya Hekalu kwa dhahabu safi, naye akaitandaza mikufu ya dhahabu kutoka upande moja hadi ule mwingine mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, ambako palifunikwa kwa dhahabu.
22 And the whole house he overlaid with gold, until all the house was finished: also the whole altar that belonged to the oracle he overlaid with gold.
Basi akafunika sehemu yote ya ndani kwa dhahabu. Pia akafunika madhabahu yale yaliyokuwa ndani ya Patakatifu pa Patakatifu kwa dhahabu.
23 And in the oracle he made two cherubim of olive wood, each ten cubits high.
Katika Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza makerubi wawili kwa mzeituni, kila moja likiwa na dhiraa kumi kwenda juu.
24 And five cubits was the one wing of the cherub, and five cubits the other wing of the cherub: from the uttermost part of the one wing unto the uttermost part of the other were ten cubits.
Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na bawa jingine dhiraa tano, hivyo urefu kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa jingine ulikuwa dhiraa kumi.
25 And the other cherub was ten cubits: both the cherubim were of one measure and one form.
Kerubi wa pili alikuwa na urefu wa dhiraa kumi pia, hivyo makerubi hao wawili walifanana kwa vipimo na kwa umbo.
26 The height of the one cherub was ten cubits, and so was it of the other cherub.
Kimo cha kila kerubi kilikuwa dhiraa kumi.
27 And he set the cherubim within the inner house: and the wings of the cherubim were stretched forth, so that the wing of the one touched the one wall, and the wing of the other cherub touched the other wall; and their wings touched one another in the midst of the house.
Aliwaweka makerubi hao ndani ya Patakatifu pa Patakatifu pa Hekalu, mabawa yake yakiwa yamekunjuliwa. Bawa la kerubi mmoja liligusa ukuta mmoja, wakati bawa la yule mwingine liligusa ukuta mwingine, nayo mabawa yao mengine yaligusana katikati ya chumba.
28 And he overlaid the cherubim with gold.
Akafunika wale makerubi kwa dhahabu.
29 And he carved all the walls of the house round about with carved figures of cherubim and palm trees and open flowers, within and without.
Juu ya kuta zote zilizozunguka Hekalu, za vyumba vya ndani na vya nje, zilipambwa kwa nakshi zilizokatwa za makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua.
30 And the floor of the house he overlaid with gold, within and without.
Pia alifunika sakafu zote za vyumba vya ndani na vya nje vya Hekalu kwa dhahabu.
31 And for the entering of the oracle he made doors of olive wood: the lintel [and] door posts were a fifth part [of the wall].
Kwa ingilio la Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza milango ya mbao za mzeituni, zikiwa na miimo na vizingiti vyenye umbo la pembe tano.
32 So [he made] two doors of olive wood; and he carved upon them carvings of cherubim and palm trees and open flowers, and overlaid them with gold; and he spread the gold upon the cherubim, and upon the palm trees.
Juu ya milango miwili ya mbao za mzeituni alinakshi makerubi, miti ya mitende pamoja na maua yaliyochanua na kufunika makerubi na miti ya mitende kwa dhahabu iliyofuliwa.
33 So also made he for the entering of the temple door posts of olive wood, out of a fourth part [of the wall];
Kwa njia iyo hiyo akatengeneza miimo yenye pande nne ya miti ya mizeituni, kwa ajili ya ingilio la ukumbi mkubwa.
34 and two doors of fir wood; the two leaves of the one door were folding, and the two leaves of the other door were folding.
Kulikuwa na milango miwili iliyoweza kukunjuka iliyotengenezwa kwa mbao za msunobari na kila mmoja ulikuwa na bawaba ambazo zingeuwezesha kujikunja kila kipande juu ya kingine.
35 And he carved [thereon] cherubim and palm trees and open flowers: and he overlaid them with gold fitted upon the graven work.
Akanakshi makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua juu yake na kufunika kwa dhahabu iliyonyooshwa vizuri juu ya michoro.
36 And he built the inner court with three rows of hewn stone, and a row of cedar beams.
Tena akajenga ua wa ndani safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa.
37 In the fourth year was the foundation of the house of the LORD laid, in the month Ziv.
Msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa katika mwaka wa nne, katika mwezi wa Zivu, ndio mwezi wa tano.
38 And in the eleventh year, in the month Bul, which is the eighth month, was the house finished throughout all the parts thereof, and according to all the fashion of it. So was he seven years in building it.
Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa Buli, ndio mwezi wa nane, Hekalu lilikamilika katika hatua zake zote kwa kufuatana na maelekezo yake Solomoni. Alilijenga kwa miaka saba.

< 1 Kings 6 >