< 1 Chronicles 14 >

1 And Hiram king of Tyre sent messengers to David, and cedar trees, and masons, and carpenters, to build him an house.
Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme.
2 And David perceived that the LORD had established him king over Israel, for his kingdom was exalted on high, for his people Israel’s sake.
Naye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.
3 And David took more wives at Jerusalem: and David begat more sons and daughters.
Huko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi.
4 And these are the names of the children which he had in Jerusalem; Shammua, and Shobab, Nathan, and Solomon;
Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
5 and Ibhar, and Elishua, and Elpelet;
Ibihari, Elishua, Elpeleti,
6 and Nogah, and Nepheg, and Japhia;
Noga, Nefegi, Yafia,
7 and Elishama, and Beeliada, and Eliphelet.
Elishama, Beeliada na Elifeleti.
8 And when the Philistines heard that David was anointed king over all Israel, all the Philistines went up to seek David: and David heard of it, and went out against them.
Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli yote, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akatoka ili kwenda kukabiliana nao.
9 Now the Philistines had come and made a raid in the valley of Rephaim.
Basi Wafilisti walikuwa wameingia na kushambulia Bonde la Warefai,
10 And David inquired of God, saying, Shall I go up against the Philistines? and wilt thou deliver them into mine hand? And the LORD said unto him, Go up; for I will deliver them into thine hand.
Hivyo Daudi akamuuliza Mungu: “Je, niende kuwashambulia hao Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”
11 So they came up to Baal-perazim, and David smote them there; and David said, God hath broken mine enemies by mine hand, like the breach of waters. Therefore they called the name of that place Baal-perazim.
Hivyo Daudi pamoja na watu wake wakakwea mpaka Baal-Perasimu, akawashinda huko. Akasema, “Kama maji yafurikavyo, Mungu amewafurikia adui zangu kwa kutumia mkono wangu.” Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Baal-Perasimu.
12 And they left their gods there; and David gave commandment, and they were burned with fire.
Wafilisti walikuwa wameacha miungu yao huko, Daudi akaamuru iteketezwe kwa moto.
13 And the Philistines yet again made a raid in the valley.
Kwa mara nyingine Wafilisti wakavamia lile bonde;
14 And David inquired again of God; and God said unto him, Thou shalt not go up after them: turn away from them, and come upon them over against the mulberry trees.
hivyo Daudi akamuuliza Mungu tena, naye Mungu akamjibu, “Usiwapandie moja kwa moja, bali wazungukie na uwashambulie kutoka mbele ya hiyo miti ya miforosadi.
15 And it shall be, when thou hearest the sound of marching in the tops of the mulberry trees, that then thou shalt go out to battle: for God is gone out before thee to smite the host of the Philistines;
Mara usikiapo sauti ya kwenda juu ya hiyo miti ya miforosadi, hapo ndipo utoke upigane vita, kwa sababu hiyo itaonyesha kwamba Mungu amekutangulia ili kupiga jeshi la Wafilisti.”
16 And David did as God commanded him: and they smote the host of the Philistines from Gibeon even to Gezer.
Kwa hiyo Daudi akafanya kama alivyoagizwa na Mungu, wakalipiga jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni hadi Gezeri.
17 And the fame of David went out unto all lands; and the LORD brought the fear of him upon all nations.
Hivyo umaarufu wa Daudi ukaenea katika kila nchi, naye Bwana akayafanya mataifa yote kumwogopa Daudi.

< 1 Chronicles 14 >