< Luke 19 >

1 Jesus entered Jericho and made his way through the town.
Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
2 There was a man there, known by the name of Zacchaeus, who was a senior tax collector and a rich man.
Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 He tried to see what Jesus was like; but, being short, he was unable to do so because of the crowd.
Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
4 So he ran on ahead and climbed into a mulberry tree to see Jesus, for he knew that he must pass that way.
Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
5 When Jesus came to the place, he looked up and said to him, “Zacchaeus, be quick and come down, for I must stop at your house today.”
Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
6 So Zacchaeus got down quickly, and joyfully welcomed him.
Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
7 On seeing this, everyone began to complain, “He has gone to stay with a man who is an outcast.”
Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
8 But Zacchaeus stood forward and said to the Master, “Listen, Master! I will give half my property to the poor, and, if I have defrauded anyone of anything, I will give him back four times as much.”
Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
9 “Salvation has come to this house today,” answered Jesus, “for even this man is a son of Abraham.
Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
10 The Son of Man has come to search for those who are lost and to save them.”
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
11 As the people were listening to this, Jesus went on to tell them a parable. He did so because he was near Jerusalem, and because they thought that the kingdom of God was going to be proclaimed at once.
Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
12 He said, “A nobleman once went to a distant country to receive his appointment to a kingdom and then return.
Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
13 He called ten of his servants and gave them ten pounds of silver each, and told them to trade with them during his absence.
Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
14 But his subjects hated him and sent envoys after him to say ‘We will not have this man as our king.’
Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
15 On his return, after having been appointed king, he directed that the servants to whom he had given his money should be summoned, so that he might learn what amount of trade they had done.
Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
16 The first came up, and said ‘Sir, your ten pounds have made a hundred.’
Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
17 ‘Well done, good servant!’ exclaimed the master. ‘As you have proved trustworthy in a very small matter, I appoint you governor over ten towns.’
Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
18 When the second came, he said ‘Your ten pounds, Sir, have produced fifty.’
Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
19 So the master said to him ‘And you I appoint over five towns.’
Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
20 Another servant also came and said ‘Sir, here are your ten pounds; I have kept them put away in a handkerchief.
Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
21 For I was afraid of you, because you are a stern man. You take what you have not planted, and reap what you have not sown.’
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
22 The master answered ‘Out of your own mouth I judge you, you worthless servant. You knew that I am a stern man, that I take what I have not planted, and reap what I have not sown?
Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
23 Then why didn’t you put my money into a bank? And I, on my return, could have claimed it with interest.
Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
24 Take away from him the ten pounds,’ he said to those standing by, ‘and give them to the one who has the hundred.’
Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
25 ‘But, Sir,’ they said, ‘he has a hundred pounds already!’
Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
26 ‘I tell you,’ he answered, ‘that, to him who has, more will be given, but, from him who has nothing, even what he has will be taken away.
'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 But as for my enemies, these men who would not have me as their king, bring them here and put them to death in my presence.’”
Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
28 After saying this, Jesus went on in front, going up to Jerusalem.
Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
29 It was when Jesus had almost reached Bethphage and Bethany, near the Mount of Olives, that he sent on two of the disciples.
Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 “Go to the village facing us,” he said, “and, when you get there, you will find a foal tethered, which no one has yet ridden; untie it and lead it here.
akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
31 And, if anybody asks you ‘Why are you untying it?’, you are to say this – ‘The Master wants it.’”
Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
32 So the two who were sent went and found it as Jesus had told them.
Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
33 While they were untying the foal, the owners asked them – “Why are you untying the foal?”
Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
34 And the two disciples answered – “The Master wants it.”
Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
35 Then they led it back to Jesus, and threw their cloaks on the foal and put Jesus on it.
Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
36 As he went along, the people kept spreading their cloaks in the road.
Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 When he had almost reached the place where the road led down the Mount of Olives, everyone of the many disciples began in their joy to praise God loudly for all the miracles that they had seen:
Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
38 “Blessed is He who comes – our king – in the name of the Lord! Peace in heaven, and glory on high.”
wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
39 Some of the Pharisees in the crowd said to him, “Teacher, restrain your disciples.”
Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
40 But Jesus answered, “I tell you that if they are silent, the stones will call out.”
Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
41 When he drew near, on seeing the city, he wept over it, and said,
Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
42 “If only you had known, while yet there was time – even you – the things that make for peace! But now they have been hidden from your sight.
akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 For a time is coming when your enemies will surround you with earthworks, and encircle you, and hem you in on all sides;
Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
44 they will trample you down and your children within you, and they will not leave in you one stone on another, because you did not know the time of your visitation.”
Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
45 Jesus went into the Temple Courts and began to drive out those who were selling,
Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
46 saying as he did so, “Scripture says – ‘My house will be a house of prayer’; but you have made it a den of robbers.”
akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
47 Jesus continued to teach each day in the Temple Courts; but the chief priests and teachers of the Law were eager to take his life, and so also were the leaders of the people.
Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
48 Yet they could not see what to do, for the people all hung on his words.
lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.

< Luke 19 >