< Romans 6 >

1 What are we to say, then? Are we to continue to sin, in order that God’s loving kindness may be multiplied?
Tuseme nini basi? Je, twendelee kubaki katika dhambi ili neema ya Mungu iongezeke?
2 Heaven forbid! We became dead to sin, so how can we go on living in it?
Hata kidogo! Kuhusu dhambi sisi tumekufa—tutaendeleaje kuishi tena katika dhambi?
3 Or can it be that you do not know that all of us, who were baptized into union with Christ Jesus, in our baptism shared his death?
Maana, mnajua kwamba sisi tuliobatizwa tukaungana na Kristo Yesu, tulibatizwa na kuungana na kifo chake.
4 Consequently, through sharing his death in our baptism, we were buried with him; so that, just as Christ was raised from the dead by a manifestation of the Father’s power, so we also may live a new life.
Tulipobatizwa tuliungana na kifo chake, tukazikwa pamoja naye, ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka wafu kwa kitendo kitukufu cha Baba, sisi pia tuweze kuishi maisha mapya.
5 If we have become united with him by the act symbolic of his death, surely we will also become united with him by the act symbolic of his resurrection.
Maana, kama sisi tumeungana naye katika kufa kama yeye, vivyo hivyo tutaungana naye kwa kufufuliwa kutoka wafu kama yeye.
6 We recognise the truth that our old self was crucified with Christ, in order that the body, the stronghold of sin, might be rendered powerless, so that we should no longer be slaves to sin.
Tunajua kwamba utu wetu wa kale ulisulubiwa pamoja na Kristo, ili hali ya dhambi iharibiwe, tusiwe tena watumwa wa dhambi.
7 For the man who has so died has been pronounced righteous and released from sin.
Kwa maana, mtu aliyekufa, amenasuliwa kutoka katika nguvu ya dhambi.
8 And our belief is, that, as we have shared Christ’s death, we will also share his life.
Basi, ikiwa tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pia pamoja naye.
9 We know, indeed, that Christ, having once risen from the dead, will not die again. Death has power over him no longer.
Maana, tunajua kwamba Kristo amekwisha fufuliwa kutoka wafu na hafi tena; kifo hakimtawali tena.
10 For the death that he died was a death to sin, once and for all. But the life that he now lives, he lives for God.
Hivyo, kwa kuwa alikufa—mara moja tu—dhambi haina nguvu tena juu yake; na sasa anaishi maisha yake katika umoja na Mungu.
11 So let it be with you – regard yourselves as dead to sin, but as living for God, through union with Christ Jesus.
Hali kadhalika nanyi lazima mjione kuwa mmekufa kuhusu dhambi, lakini kama mnaoishi katika umoja na Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
12 Therefore do not let sin reign in your mortal bodies and compel you to obey its cravings.
Kwa hiyo, dhambi isiitawale tena miili yenu ambayo hufa, na hivyo kuzitii tamaa zake.
13 Do not offer any part of your bodies to sin, in the cause of unrighteousness, but once for all offer yourselves to God (as those who, though once dead, now have life), and devote every part of your bodies to the cause of righteousness.
Wala msitoe hata sehemu moja ya miili yenu iwe chombo cha kutenda uovu na dhambi. Badala yake, jitoleeni ninyi wenyewe kwa Mungu kama watu waliofufuliwa kutoka wafu; toeni nafsi zenu zote kwa Mungu kwa ajili ya uadilifu.
14 For sin will not lord it over you. You are living under the reign, not of Law, but of love.
Maana, dhambi haitawatawala ninyi tena, kwani hamko chini ya Sheria, bali chini ya neema.
15 What follows, then? Are we to sin because we are living under the reign of love and not of Law? Heaven forbid!
Basi, tuseme nini? Je, tutende dhambi ati kwa sababu hatuko chini ya Sheria bali chini ya neema? Hata kidogo!
16 Surely you know that when you offer yourselves as servants, to obey anyone, you are the servants of the person whom you obey, whether the service be a service to sin which leads to death, or a service to duty which leads to righteousness.
Mnajua kwamba mkijitolea ninyi wenyewe kama watumwa na kumtii fulani, mnakuwa kweli watumwa wake mtu huyo—au watumwa wa dhambi, na matokeo yake ni kifo, au wa utii, na matokeo yake ni kukubaliwa kuwa waadilifu.
17 God be thanked that, though you were once servants of sin, yet you learned to give hearty obedience to that form of doctrine under which you were placed.
Ingawa mlikuwa watumwa wa dhambi zamani, sasa lakini—namshukuru Mungu—mmetii kwa moyo wote yale maazimio na mafundisho mliyopokea.
18 Set free from the control of sin, you became servants to righteousness.
Mlikombolewa kutoka utumwa wa dhambi, mkawa watumwa wa uadilifu.
19 I can but speak as people do because of the weakness of your earthly nature. Once you offered every part of your bodies to the service of impurity, and of wickedness, which leads to further wickedness. Now, in the same way, offer them to the service of righteousness, which leads to holiness.
(Hapa natumia lugha ya kawaida ya watu kwa sababu ya udhaifu wenu wenyewe.) Kama vile wakati fulani mlivyojitolea ninyi wenyewe kutumikia uchafu na uhalifu kwa ajili ya uovu, vivyo hivyo sasa jitoleeni nafsi zenu wenyewe kutumikia uadilifu kwa ajili ya utakatifu.
20 While you were still servants of sin, you were free as regards righteousness.
Mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na uadilifu.
21 But what were the fruits that you reaped from those things of which you are now ashamed? For the end of such things is death.
Sasa, mlipata faida gani siku zile kutokana na mambo yale ambayo mnayaonea aibu sasa? Maana, matokeo ya mambo haya ni kifo!
22 But now that you have been set free from the control of sin, and have become servants to God, the fruit that you reap is an ever increasing holiness, and the end eternal life. (aiōnios g166)
Lakini sasa, mmekwisha kombolewa kutoka utumwa wa dhambi na mmekuwa watumishi wa Mungu; faida mliyo nayo sasa ni utakatifu, na matokeo yake ni uzima wa milele. (aiōnios g166)
23 The wages of sin are death, but the gift of God is eternal life, through union with Christ Jesus, our Lord. (aiōnios g166)
Kwa maana mshahara wa dhambi ni kifo; lakini zawadi anayotoa Mungu ni uzima wa milele katika kuungana na Kristo Yesu, Bwana wetu. (aiōnios g166)

< Romans 6 >