< Revelation 4 >

1 After this, in my vision, I saw an open door in the heavens, and the first voice that I heard was like the blast of a trumpet speaking to me. It said – “Come up here and I will show you what must take place.”
Baada ya mambo hayo nilitazama, nami nikaona mbele yangu mlango uliokuwa wazi mbinguni. Nayo ile sauti niliyokuwa nimeisikia hapo mwanzo ikisema nami kama tarumbeta ikasema, “Njoo, huku, nami nitakuonyesha yale ambayo hayana budi kutokea baada ya haya.”
2 Immediately after this I fell into a trance. There stood a throne in heaven, and on the throne was One seated.
Ghafula nilikuwa katika Roho, na hapo mbele yangu kilikuwepo kiti cha enzi mbinguni, kikiwa kimekaliwa na mtu.
3 He who was seated on it was in appearance like a jasper and a sardius; and round the throne there was a rainbow of the colour of an emerald.
Aliyekuwa amekikalia alikuwa anaonekana kama yaspi na akiki. Kukizunguka kile kiti cha enzi palikuwa na upinde wa mvua ulioonekana kama zumaridi.
4 And round the throne were twenty-four other thrones, and on these I saw twenty-four elders sitting clothed in white robes; and on their heads they had crowns of gold.
Kukizunguka hicho kiti cha enzi palikuwa na viti vingine vya enzi ishirini na vinne, na juu ya hivyo viti walikuwa wameketi wazee ishirini na wanne. Walivaa mavazi meupe, na walikuwa na taji za dhahabu vichwani mwao.
5 Out from the throne come flashes of lightning, cries, and peals of thunder! There are seven torches burning in front of the throne, which are the seven spirits of God;
Kwenye kile kiti cha enzi palikuwa panatoka miali ya umeme wa radi, ngurumo na sauti za radi. Mbele ya kiti cha enzi, taa saba zilikuwa zinawaka. Hizi ndizo roho saba za Mungu.
6 and in front of the throne is what seemed to be a sea of glass, resembling crystal, while within the space before the throne and round the throne are four creatures full of eyes in front and behind.
Pia mbele ya kiti cha enzi palikuwa na kile kilichoonekana kama bahari ya kioo, iliyokuwa angavu kama bilauri. Katikati, kukizunguka kile kiti cha enzi, kulikuwa na viumbe wanne wenye uhai, wakiwa wamejawa na macho mbele na nyuma.
7 The first creature is like a lion, the second creature like a calf, the third creature has a face like a man’s, and the fourth creature is like an eagle on the wing.
Kiumbe wa kwanza mwenye uhai alikuwa kama simba, wa pili alikuwa kama ngʼombe dume, wa tatu alikuwa na uso kama wa mwanadamu, na wa nne alikuwa kama tai anayeruka.
8 These four creatures have each of them six wings, and all round, and within, they are full of eyes; and day and night they never cease to say – “Holy, holy, holy is the Lord, our God, the Almighty, who was, and who is, and who will be.”
Kila mmoja wa hawa viumbe wanne wenye uhai alikuwa na mabawa sita, na kujawa na macho pande zote hadi chini ya mabawa. Usiku na mchana hawaachi kusema:
9 And, whenever these creatures give praise and honour and thanks to him who is seated on the throne, to him who lives for ever and ever, (aiōn g165)
Kila mara viumbe hao wanne wenye uhai wanapomtukuza, kumheshimu na kumshukuru yeye aketiye kwenye kile kiti cha enzi, tena aishiye milele na milele, (aiōn g165)
10 the twenty-four elders prostrate themselves before him who is seated on the throne, and worship him who lives for ever and ever, and throw down their crowns before the throne, saying – (aiōn g165)
wale wazee ishirini na wanne huanguka mbele zake aketiye kwenye kiti cha enzi na kumwabudu yeye aliye hai milele na milele. Huziweka taji zao mbele ya kiti cha enzi, wakisema: (aiōn g165)
11 “Worthy are you, our Lord and God, to receive all praise, and honour, and power, for you did create all things, and at your bidding they came into being and were created.”
“Bwana wetu na Mungu wetu, wewe unastahili kupokea utukufu na heshima na uweza, kwa maana ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa mapenzi yako viliumbwa na vimekuwako.”

< Revelation 4 >