+ Psalms 1 >

1 Happy are those who do not follow the counsel of the wicked, not halting in ways frequented by sinners, nor taking a seat in a gathering of scoffers.
Amebarikiwa mtu yule asiye enenda katika ushauri wa waovu, au kusimama katika njia ya wenye dhambi, au kukaa katika kusanyiko la wenye mizaha.
2 But the law of the Lord is their joy, they study it day and night.
Bali yeye huifurahia sheria ya Yahwe, na huitafakari sheria yake mchana na usiku.
3 They are like trees planted by runlets of water, yielding fruit in due season, leaves never fading. In all that they do, they prosper.
Atakuwa kama mti uliopandwa karibu na mkondo wa maji ambao huzaa matunda yake kwa majira yake, ambao majani yake hayakauki; lolote afanyalo litafanikiwa.
4 Not so fare the wicked, not so; like chaff are they, blown by the wind.
Waovu hawako hivyo, wao badala yake ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 So the wicked will not stand firm in the judgment, nor sinners appear, when the righteous are gathered.
Kwa hivyo waovu hawatasimama katika hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 For the way of the righteous is dear to the Lord, but the way of the wicked will end in ruin.
Kwa kuwa Yahweh huikubali njia ya wenye haki, njia ya waovu itaangamizwa.

+ Psalms 1 >