< Psalms 76 >

1 For the leader. With instrumental music. A psalm of Asaph, a song. God has made himself known in Judah, his name is great in Israel.
Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
2 His tent is in Salem, his dwelling in Zion.
Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
3 There he broke the lightning arrows, shield, sword, and weapons of war. (Selah)
Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
4 Terrible is your splendour on the everlasting mountains.
Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
5 Despoiled were the stout of heart; in the sleep into which they had fallen, none of the warriors could lift a hand.
Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
6 At your rebuke, God of Jacob, sank chariot and horse to sleep.
Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
7 Awful are you: who can stand before you, when once you are angry?
Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
8 The judgment you gave from heaven frightened the earth into silence,
Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
9 when God arose to judgment to save the oppressed of the earth. (Selah)
wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
10 The fiercest will praise you, to you will the remnant hold festival.
Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
11 Vow and pay to Lord your God, and let all who are round him bring presents.
Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
12 He lops off the courage of princes, and with terror fills kings of the earth.
Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.

< Psalms 76 >