< Psalms 50 >

1 A psalm of Asaph. The Lord God has spoken: He summons the earth from sunrise to sunset.
Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
2 From Zion, perfection of beauty, God’s glory shines forth.
Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
3 Our God comes, he cannot keep silence, devouring fire is before him, and furious tempest around him.
Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
4 He summons the heavens above and the earth to judge his people.
Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5 Gather to him his saints by covenant-sacrifice bound to him;
Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6 that the heavens may declare his justice, for a God of justice is he. (Selah)
Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7 ‘Hear, O my people, and I will speak, and protest to you, O Israel: I am the Lord, your God.
Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8 Not for your sacrifices will I reprove you your burnt-offerings are ever before me
Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9 Not a bullock will I take from your house, nor male goats out of your folds;
Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10 for all beasts of the forest are mine, and the kine on a thousand hills.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11 I know all the birds of the air, all that moves on the fields is mine.
Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
12 Were I hungry, I would not tell you, for the world and its fulness are mine.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13 Am I such as to eat bulls’ flesh, or drink the blood of goats?
Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
14 Offer to God a thank-offering, pay the Most High your vows.
Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
15 Summon me in the day of distress, I will rescue you, so will you honour me.’
Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
16 But to the wicked God says: ‘What right have you to talk of my statutes, or take my covenant into your mouth
Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
17 while you yourself hate correction, and cast my words behind you?
wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
18 When you see a thief, you run with them; with adulterers you keep company.
Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
19 You let your mouth loose for evil, your tongue contrives deceit.
Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
20 You shamefully speak of your kin, and slander your own mother’s son.
Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
21 And because I kept silence at this, you did take me for one like yourself. But I will convict you and show you plainly.
Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
22 ‘Now you who forget God, mark this, lest I rend you, past hope of deliverance.
Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
23 Those who bring a thank-offering honour me; but to those: who follows my way, I will show the salvation of God.’
Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”

< Psalms 50 >