< Psalms 22 >

1 For the leader; set to “Deer of the Dawn”. A psalm of David. My God, my God, why have you left me, my rescue so far from the words of my roaring?
Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
2 I cry in the day, you do not answer, I cry in the night but find no rest.
Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
3 You are the Holy One, throned on the praises of Israel.
Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
4 In you our ancestors trusted, they trusted and you delivered them.
Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
5 They cried to you, and found safety, in you did they trust and were not put to shame.
Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
6 But I am a worm, not a person; insulted by others, despised by the people.
Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
7 All who see me mock me, with mouths wide open and wagging heads:
Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
8 ‘He relies on the Lord; let him save him. Let him rescue the one he holds dear!’
Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
9 But you drew me from the womb, laid me safely on my mother’s breasts.
Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
10 On your care was I cast from my very birth, you are my God from my mother’s womb.
Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
11 Be not far from me, for trouble is nigh, and there is none to help.
Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
12 I am circled by many bulls, beset by the mighty of Bashan,
Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
13 who face me with gaping jaws, like ravening roaring lions.
Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
14 Poured out am I like water, and all my bones are loosened. My heart is become like wax, melted within me.
Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
15 My palate is dry as a sherd, my tongue sticks to my jaws; in the dust of death you lay me.
Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
16 For dogs are round about me, a band of knaves encircles me, gnawing my hands and my feet.
Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
17 I can count my bones, every one. As for them, they feast their eyes on me.
Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
18 They divide my garments among them, and over my raiment cast lots.
Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
19 But you, O Lord, be not far, O my strength, hasten to help me.
Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
20 Deliver my life from the sword my life from the power of the dogs.
Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
21 Save me from the jaws of the lion, from the horns of the wild oxen help me.
Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
22 I will tell of your fame to my kindred, and in the assembly will praise you.
Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
23 Praise the Lord, you who fear him. All Jacob’s seed, give him glory. All Israel’s seed, stand in awe of him.
Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
24 For he has not despised nor abhorred the sorrow of the sorrowful. He hid not his face from me, but he listened to my cry for help.
Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
25 Of you is my praise in the great congregation; my vows I will pay before those who fear him.
Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
26 The afflicted will eat to their heart’s desire, and those who seek after the Lord will praise him. Lift up your hearts forever.
Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
27 All will call it to mind, to the ends of the earth, and turn to the Lord; and all tribes of the nations will bow down before you.
Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
28 For the kingdom belongs to the Lord: he is the Lord of the nations.
Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
29 To him will bow down all who sleep in the earth, and before him bend all who go down to the dust, and those who could not preserve their lives.
Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
30 My descendants will tell of the Lord to the next generation;
Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
31 they will declare his righteousness to people yet to be born: He has done it.
Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!

< Psalms 22 >