< Psalms 146 >

1 My soul, praise the Lord.
Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
2 I will praise the Lord, while I live; I will sing to my God, while I am.
Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
3 Put not your trust in princes mortals, in whom is no help.
Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
4 When their breath goes out, they go back to the dust: on that very day their purposes perish.
Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
5 Happy those whose help is the God of Jacob: whose hope is set on the Lord their God,
Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
6 the Creator of heaven and earth, the sea, and all that is in them. He remains eternally loyal.
Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
7 For the wronged he executes justice; he gives bread to the hungry; the Lord releases the prisoners.
Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
8 The Lord gives sight to the blind: the Lord raises those who are bowed. The Lord loves the righteous.
Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
9 The Lord preserves the stranger, upholds the widow and orphan, but the wicked he leads to disaster.
Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
10 The Lord shall reign forever, your God, O Zion, to all generations. Hallelujah.
Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.

< Psalms 146 >