< Psalms 109 >

1 For the leader. Of David, a psalm. O God whom I praise, keep not silence;
Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
2 for their wicked mouths they have opened against me, they speak to me with tongues that are false,
Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
3 they beset me with words of hatred, and fight without cause against me.
Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
4 My love they requite with hostility, while for them I lift up my prayer.
Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
5 Evil for good they reward me, and hatred for my love.
Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
6 ‘Set over him one who is godless,’ they say, ‘an opponent at his right hand.
Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
7 From his trial let him come forth guilty, may his prayer be counted as sin.
Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
8 Grant that his days may be few, that his office be seized by another.
Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
9 Grant that his children be fatherless, and that his wife be a widow.
Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
10 Up and down may his children go begging, expelled from their desolate home.
Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
11 May all that he owns be seized by the creditor may strangers plunder the fruits of his toil.
Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
12 ‘May none extend to him kindness, or pity his fatherless children.
Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
13 His descendants be doomed to destruction! Blotted out be his name in one generation!
Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
14 May his father’s guilt be remembered, and his mother’s sin not blotted out:
Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
15 on record always before the Lord, and his memory root from the earth;
Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
16 for he gave no thought to show kindness, but pursued the poor and the needy, drove the downhearted to death.
Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
17 ‘May the curses he loved light upon him, may the blessings he loathed be afar.
Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
18 Like a garment he clothed him with curses; may they pierce to his inwards like water, and cling to his bones like oil.
Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
19 Let them be like the robe he wraps round him, like the belt he wears every day.’
Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
20 Be this the reward of my adversaries, of those who speak evil against me.
Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
21 But you, Lord my God, be true to your name, deal kindly with me; in your gracious kindness save me.
Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
22 For I am poor and needy, and my heart is wounded within me.
Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 I am gone like a lengthening shadow, I am shaken off like a locust.
Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
24 My knees totter from fasting, my flesh is shrivelled and spare.
Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
25 They heap insults upon me: when they see me, they shake their head.
Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
26 Help me, O Lord my God, and save me in your kindness.
Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
27 Teach them that this is your hand, and your own doing, O Lord.
Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
28 Let them curse, if only you bless. Put my assailants to shame, and make your servant glad.
Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
29 My opponents be clothed with dishonour, and wrapped in a robe of shame.
Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
30 I give thanks to you, Lord, with loud voice, I give praise in the midst of the throng;
Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
31 for he stands by the poor, at his right hand, to save them from those who condemn them.
Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.

< Psalms 109 >