< Psalms 107 >

1 Give thanks to the Lord for his goodness for his kindness endures forever.
Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Let this be the song of the ransomed, whom the Lord has redeemed from distress,
Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
3 gathering them from all lands, east, west, north, and south.
Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 In the wastes of the desert some wandered, finding no way to a city inhabited.
Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
5 Full of hunger and thirst, their spirit failed.
Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
6 Then they cried to the Lord in their trouble, and he saved them from their distresses,
Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
7 guiding them straight on the way, till they reached an inhabited city.
Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
8 Let them thank the Lord for his kindness, for his wonderful deeds for people;
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
9 for the thirsty he satisfies, and the hungry he fills with good things.
Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
10 Some sat in darkness and gloom prisoners in irons and misery,
Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
11 for rebelling against God’s word, and spurning the Most High’s counsel.
Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
12 Their heart was bowed with toil; there was no one to help when they stumbled.
Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
13 Then they cried to the Lord in their trouble, and he saved them from their distresses.
Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
14 Out of darkness and gloom he brought them, and burst their chains.
Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
15 Let them praise the Lord for his kindness, for his wonderful deeds for people.
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
16 For he shattered the gates of bronze, and broke bars of iron.
Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Some were sick from their wicked ways, and suffering because of their sins.
Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
18 All manner of food they hated; they had come to the gates of death.
Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
19 Then they cried to the Lord in their trouble, and he saved them from their distresses.
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
20 He sent his word and healed them, and delivered their life from the pit.
Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
21 Let them praise the Lord for his kindness, for his wonderful deeds for people.
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
22 Let them offer to him thankofferings, and with joy tell what things he has done.
Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
23 Some crossed the sea in ships, doing business in great waters.
Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
24 They have seen what the Lord can do, and his wonderful deeds on the deep.
Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
25 At his command rose a tempest, which lifted the waves on high.
Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
26 Up to heaven they went, down to the depths; their courage failed them.
Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
27 They staggered and reeled like drunkards; all their skills useless.
Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
28 Then they cried to the Lord in their trouble, and he saved them from their distresses.
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
29 He stilled the storm to a whisper, and the waves of the sea were hushed.
Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
30 They were glad, because it was quiet; they were led to the haven they longed for.
Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
31 Let them praise the Lord, for his kindness, for his wonderful deeds for people.
Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
32 Where the people assemble, extol him, and praise him in council of elders.
Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
33 He turns streams into a wilderness, springs of water into thirsty land,
Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
34 fruitful land into a salt waste, because of the sin of the people.
na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
35 A desert he makes pools of water, a land of drought into springs of water.
Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
36 He settles the hungry therein, they establish a city to live in.
Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
37 They sow fields and plant vineyards, which furnish a fruitful yield.
Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
38 By his blessing they multiply greatly, and he lets not their cattle decrease.
Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
39 Yet when they are bowed and diminished by oppression, misfortune, or sorrow,
Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
40 he pours contempt upon princes, and on trackless wastes leads them astray
Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
41 He lifts the poor out of misery, and makes families fruitful as flocks.
Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
42 At this sight shall the upright be glad, and all wicked mouths shall be stopped.
Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
43 Let those who are wise observe this, and consider the love of the Lord
Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.

< Psalms 107 >