< Micah 5 >

1 ‘Now cut yourself in bitter grief, daughter besieged by soldiers. They have set a wall around you. They strike the ruler of Israel, in the face with a rod.
Sasa njoni pamoja katika safu ya kupigana, binti wa maaskari; maaskari wameuzingira mji, kwa ufito watampiga mwamuzi wa Israeli kwenye shavu.
2 ‘Bethlehem in Ephrathah, small among the tribes of Judah, from you will come a king who will rule for me over Israel, whose family line goes back to the distant past.’
Lakini wewe, Bethlehemu Efrata, hata kama uko mdogo miongoni mwa koo za Yuda, kutoka kweko mmoja atakuja kwangu kutawala Israeli, ambaye mwanzo wake ni kutoka nyakati za kale, toka milele.
3 So the Lord will only abandon Israel to its enemies until the woman in labour gives birth. Then the survivors will be reunited with their own people.
Kwa hiyo Mungu atawapa, hata mda wa yeye aliye katika uchungu kuzaa mtoto, na mabaki ya ndugu zake yatawarudia wana wa Israeli.
4 And he will stand and shepherd by the strength of the Lord, In the exalted name of the Lord his God; And they will live in security, for now he will be great, even to the ends of the earth.
Atasimama na kuchunga kundi lake kwa nguvu za Yahwe, kwa ukuu wa enzi ya jina la Yahwe Mungu wake. Watabaki, kwa kuwa atakuwa mashuhuri hata mwisho wa dunia.
5 This will be our peace: when Assyria comes into our land and treads on our soil, we will raise up against him seven shepherds, eight leaders of men.
Atakuwa amani yetu. Wakati Waashuru watakapokuja kwenye nchi yetu, wakati wakitembea dhidi ya boma yetu, kisha kisha tutainuka juu yao wachungaji saba na viongozi nane juu ya watu.
6 They will shepherd Assyria with a sword, and the land of Nimrod with bared blades. They will deliver us from Assyria, when they come into our land, and tread within our borders.
Watachunga nchi ya Ashuru kwa upanga, na nchi ya Nimrodi katika malango yake. Atatuokoa kutoka kwa Waashuru, watakapokuja kwenye nchi yetu, watakapoingia kwenye mipaka yetu.
7 And the survivors of Jacob will be disbursed among the nations, in the midst of many peoples, like dew from the Lord, like showers on the grass, which don’t wait for people to come or linger for mortals.
Mabaki ya Yakobo yatakuwa katika kabila za watu wengi, kama umande utokao kwa Yahwe, kama manyunyu kwenye majani, ambayo hayamsubiri mtu, na hayawasubiri watoto wa mwanadamu.
8 And the survivors of Jacob will be disbursed among the nations, in the midst of many peoples, like a lion among the beasts of the forest, like a young lion among the sheep-folds, who, when he passes through, pounces. He savages his prey. There is no rescuer.
Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa, miongoni mwa watu wengi, kama simba katikati ya kundi la kondoo. wakati akipita katikati yao, atawakanyaga juu yao na kuwachachana kuwa vipande vipande, na hakutakuwa na mtu wa kuwaokoa.
9 Let your hand triumph over your adversaries, let all your enemies be cut off.
Mkono wako utainuliwa dhidi ya maadui zako, na utawaharibu.
10 On that day, says the Lord: ‘I will slaughter your horses from your midst, and destroy your chariots.
“Itatokea siku hiyo,” asema Yahwe, “kwamba nitawaharibu farasi wako kutoka miongoni mwenu na nitayavunja magari yako ya farasi.
11 I will devastate the cities in your land, and tear down your fortresses.
Nitaiharibu miji katika nchi yako na kuzingusha ngome zako zote.
12 I will destroy your magic charms, and you will have no soothsayers.
Nitauharibu uchawi kwenye mkono wako, na hakutakuwa na waaguzi tena.
13 I will cut down your idols and sacred pillars, and you will not worship any more the work of your hands.
Nitaziaharibu sanamu zako za pango na nguzo za mawe kutoka miongoni mwako. Hautaabudu tena ustadi wa mikono yako.
14 I will uproot your sacred poles, and destroy your idols.
Nitazin'goa nguzo zako za Ashera kutoka miongoni mwenu, na nitaiharibu miji yenu.
15 In my wrath and my anger I will seek vengeance on the nations that ignore me.’
Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu juu ya mataifa ambayo hayakusikiliza.”

< Micah 5 >