< Matthew 8 >

1 When Jesus had come down from the hill, great crowds followed him.
Wakati Yesu aliposhuka chini kutoka mlimani, umati mkubwa ulimfuata.
2 He saw a leper who came up, and bowed to the ground before him, and said, ‘Master, if only you are willing, you are able to make me clean.’
Tazama, mkoma alikuja na kusujudu mbele yake, akasema, “Bwana, ikiwa uko tayari, unaweza kunifanya niwe safi”.
3 Stretching out his hand, Jesus touched him, saying as he did so, ‘I am willing; become clean.’ Instantly he was made clean from his leprosy;
Yesu akanyoosha mkono wake na kumgusa, akasema, “Niko tayari. Uwe msafi.” Hapo hapo alitakaswa ukoma wake.
4 and then Jesus said to him, ‘Be careful not to say a word to anyone, but go and show yourself to the priest, and offer the gift directed by Moses, as evidence of your cure.’
Yesu akamwambia, “Angalia kwamba usiseme kwa mtu yeyote. Shika njia yako, na jioneshe mwenyewe kwa kuhani na utoe zawadi ambayo Musa aliagiza, kwa ajili ya ushuhuda kwao”
5 After Jesus had entered Capernaum, a centurion in the Roman army came up to him, entreating his help.
Wakati Yesu alipofika Kapernaumu, Jemedari akaja kwake akamuuliza
6 ‘Sir,’ he said, ‘my manservant is lying ill at my house with a stroke of paralysis, and is suffering terribly.’
akisema, “Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani amepooza na ana maumivu ya kutisha.”
7 ‘I will come and cure him,’ answered Jesus.
Yesu akamwambia, “Nitakuja na kumponya”.
8 ‘Sir,’ the centurion went on, ‘I am unworthy to receive you under my roof; but only speak, and my manservant will be cured.
Jemedari akajibu na kumwambia, “Bwana, mimi si wathamani hata uje na kuingia ndani ya dari yangu, sema neno tu na mtumishi wangu ataponywa.
9 For I myself am a man under the orders of others, with soldiers under me; and, if I say to one of them “Go,” he goes, and to another “Come,” he comes, and to my slave “Do this,” he does it.’
Kwa kuwa mimi pia ni mtu niliye na mamlaka, na ninao askari walio chini yangu. Nikisema kwa huyu “Nenda' na huenda, na kwa mwingine 'Njoo' na yeye huja, na kwa mtumishi wangu, 'Fanya hivi,' na yeye anafanya hivyo”
10 Jesus was surprised to hear this, and said to those who were following him, ‘Never I tell you, in any Israelite have I met with such faith as this!
Wakati Yesu aliposikia haya, alishangazwa na kuwaambia wale waliokuwa wakimfuata, “Kweli ninawaambia, Sijapata kuona mtu mwenye imani kama huyu katika Israel.
11 Yes, and many will come in from East and West and take their places beside Abraham, Isaac, and Jacob, in the kingdom of heaven;
Ninawambieni, wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, wataketi katika meza pamoja na Abrahimu, Isaka, na Yakobo, katika ufame wa mbinguni.
12 while the heirs to the kingdom will be banished into the darkness outside; there, there will be weeping and grinding of teeth.’
Lakini watoto wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ambapo kutakuwa na kilio na kusaga meno.”
13 Then Jesus said to the centurion, ‘Go now, and it will be according to your faith.’ And the man was cured that very hour.
Yesu akamwambia Jemadari, “Nenda! Kama ulivyokwisha amini, na itendeke hivyo kwako”. Na mtumishi aliponywa katika saa hiyo.
14 When Jesus went into Peter’s house, he saw Peter’s mother-in-law prostrated with fever.
Wakati Yesu alipofika kwenye nyumba ya Petro, alimwona mama mkwe wake na Petro amelala akiwa mgonjwa wa homa.
15 On his taking her hand, the fever left her, and she rose and began to take care of him.
Yesu akamgusa mkono wake, na homa yake ikamwacha. kisha akaamka akaanza kumhudumia.
16 In the evening the people brought to Jesus many who were possessed by demons; and he drove out the spirits with a word, and cured all who were ill,
Na ilipofika jioni, watu wakamletea Yesu wengi waliotawaliwa na pepo. Akawafukuza pepo na wale walio wagonjwa akawaponya.
17 in fulfilment of these words in the prophet Isaiah – “He took our infirmities on himself, and bore the burden of our diseases.”
Kwa jinsi hii yalitimia yale yaliyo kwisha kunenwa na Isaya nabii, “Yeye mwenyewe alichukua magonjwa yetu na alibeba maradhi yetu”
18 Seeing a crowd round him, Jesus gave orders to go across.
Kisha Yesu alipoliona kusanyiko limemzunguka, alitoa maelekezo ya kwenda upande mwingine wa Bahari ya Galilaya.
19 A teacher of the Law came up to him, and said, ‘Teacher, I will follow you wherever you go.’
Kisha mwandishi akaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, nitakufuata popote utakapoenda.”
20 ‘Foxes have holes,’ answered Jesus, ‘and wild birds their nests, but the Son of Man has nowhere to lay his head.’
Yesu akamwambia, “Mbweha wana mashimo, na ndege wa angani wana viota, lakini mwana wa Adamu hana sehemu ya kulaza kichwa chake.”
21 ‘Master,’ said another, who was a disciple, ‘let me first go and bury my father.’
Mwanafunzi mwingine akamwambia, “Bwana, niruhusu kwanza niende kumzika baba yangu.”
22 But Jesus answered, ‘Follow me, and leave the dead to bury their dead.’
Lakini Yesu akamwambia, “Nifuate, na uwaache wafu wazike wafu wao.”
23 Then he got into the boat, followed by his disciples.
Yesu alipoingia kwenye mtumbwi, wanafunzi wake wakamfuata mtumbwini.
24 Suddenly so great a storm came up on the sea, that the waves broke right over the boat. But Jesus was asleep;
Tazama, ikainuka dhoruba kuu juu ya bahari, kiasi kwamba mtumbwi ulifunikwa na mawimbi. Lakini Yesu alikuwa amelala.
25 and the disciples came and roused him. ‘Master,’ they cried, ‘save us; we are lost!’
Wanafunzi wakaja kwake na kumwamsha wakisema, “Bwana, tuokoe sisi, tunaelekea kufa!”
26 ‘Why are you so timid?’ he said. ‘You of little faith!’ Then Jesus rose and rebuked the winds and the sea, and a great calm followed.
Yesu akawaambia, “kwa nini mnaogopa, ninyi wenye imani ndogo?” Ndipo akaamka na kuukemea upepo na bahari. Kisha kukawa na utulivu mkuu,
27 The men were amazed, and exclaimed, ‘What kind of man is this, that even the winds and the sea obey him!’
wanaume wakashikwa na mshangao wakasema, “Huyu mtu niwa namna gani, kwamba hata pepo na bahari vinamtii yeye?”
28 On getting to the other side – the region of the Gadarenes – Jesus met two men who were possessed by demons, coming out of the tombs. They were so violent that no one was able to pass that way.
Wakati Yesu alipokuwa amekuja upande mwingine wa nchi ya Magadala, wanaume wawili waliotawaliwa na pepo walikutana naye. Walikuwa wakitokea makaburini na walikuwa wakifanya vurugu sana, kiasi kwamba hakuna msafiri angeweza kupita njia ile.
29 Suddenly they shrieked out, ‘What do you want with us, Son of God? Have you come here to torment us before our time?’
Tazama, walipaza sauti na kusema, “Tuna nini cha kufanya kwako, mwana wa Mungu? Umekuja hapa kututesa kabla ya wakati kufika?”
30 A long way off, there was a herd of many pigs, feeding;
Sasa kundi kubwa la nguruwe lilikuwa likichunga, hapakuwa mbali sana walipokuwa,
31 and the foul spirits began begging Jesus, ‘If you drive us out, send us into the herd of pigs.’
pepo waliendelea kulalamika kwa Yesu na kusema. “Ikiwa utatuamuru kutoka, tupeleke kwenye kundi la nguruwe.”
32 ‘Go,’ he said. The spirits came out, and entered the pigs; and the whole herd rushed down the steep slope into the sea, and died in the water.
Yesu akawaambia, “Nendeni!” Pepo wakawatoka na kwenda kwa nguruwe. Na tazama, kundi lote likashuka kutoka mlimani kuteremkia baharini na lote likafia majini.
33 At this the men who tended them ran away and went to the town, carrying the news of all that had occurred, and of what had happened to the possessed men.
Wanaume waliokuwa wakichunga nguruwe walikimbia. Na walipoenda mjini wakaelezea kila kitu, hususani kilichotokea kwa wanaume waliotawaliwa na mapepo.
34 At the news the whole town went out to meet Jesus, and, when they saw him, they entreated him to go away from their region.
Tazama, mji mzima ukaja kukutana na Yesu. Walipomwona, walimsihi aondoke kwenye mkoa wao.

< Matthew 8 >