< Mark 1 >

1 The beginning of the good news about Jesus Christ.
Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 It is said in the prophet Isaiah – “I am sending my messenger ahead of you; he will prepare your way.
Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
3 The voice of one crying aloud in the wilderness: ‘Prepare the road for the Lord, make a straight path for him.’”
Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
4 John the Baptizer appeared in the wilderness, proclaiming a baptism on repentance, for the forgiveness of sins.
Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
5 The whole of Judea, as well as all the inhabitants of Jerusalem, went out to him; and they were baptized by him in the Jordan River, confessing their sins.
Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
6 John wore clothes made of camels’ hair, with a leather strap round his waist, and lived on locusts and wild honey;
Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
7 and he proclaimed – ‘After me is coming someone more powerful than I am, and I am not fit even to stoop down and unfasten his sandals.
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
8 I have baptized you with water, but he will baptize you with the Holy Spirit.’
Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
9 Now about that time Jesus came from Nazareth in Galilee, and was baptized by John in the Jordan.
Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
10 Just as he was coming up out of the water, he saw the heavens split open and the Spirit coming down to him like a dove,
Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
11 and from the heavens came a voice – ‘You are my dearly loved son; you bring me great joy.’
Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
12 Immediately afterwards the Spirit drove Jesus out into the wilderness;
Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
13 and he was there in the wilderness forty days, tempted by Satan, and among the wild beasts, while the angels helped him.
akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
14 After John had been arrested, Jesus went to Galilee, proclaiming the good news of God –
Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
15 ‘The time has come, and the kingdom of God is at hand; repent, and believe the good news.’
“Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
16 As Jesus was going along the shore of the Sea of Galilee, he saw Simon and his brother Andrew casting a net in the sea, for they were fishermen.
Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
17 ‘Come and follow me,’ Jesus said, ‘and I will teach you to fish for people.’
Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
18 They left their nets at once, and followed him.
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
19 Going on a little further, he saw James, Zebedee’s son, and his brother John, who were in their boat mending the nets.
Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 Jesus called them at once, and they left their father Zebedee in the boat with the crew, and went after him.
Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
21 They walked to Capernaum. On the next Sabbath Jesus went into the synagogue and began to teach.
Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
22 The people were amazed at his teaching, for he taught them like one who had authority, and not like the teachers of the Law.
Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
23 Now there was in their synagogue at the time a man under the power of a foul spirit, who called out,
Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
24 ‘What do you want with us, Jesus the Nazarene? Have you come to destroy us? I know who you are – the Holy One of God!’
akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
25 But Jesus rebuked the spirit, ‘Be silent! Come out from him.’
Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
26 The foul spirit threw the man into a fit, and with a loud cry came out from him.
Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
27 They were all so amazed that they kept asking each other, ‘What is this? What is this, a new kind of teaching? He gives his commands with authority even to the foul spirits, and they obey him!’
Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 His fame spread at once in all directions, through the whole region of Galilee.
Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
29 As soon as they had left the synagogue, they went to the house of Simon and Andrew, along with James and John.
Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
30 Now Simon’s mother-in-law was lying ill with a fever, and they at once told Jesus about her.
Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
31 Jesus went up to her and, grasping her hand, raised her up; the fever left her, and she began to take care of them.
Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
32 In the evening, after sunset, the people brought to Jesus all who were ill or possessed by demons;
Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
33 and the whole city was gathered round the door.
Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
34 Jesus cured many who were ill with various diseases, and drove out many demons, and would not permit them to speak, because they knew him to be the Christ.
Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
35 In the morning, long before daylight, Jesus got up and went out to a lonely spot, where he began to pray.
Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36 But Simon and his companions went out searching for him;
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37 and, when they found him, they exclaimed, ‘Everyone is looking for you!’
Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
38 But Jesus said to them, ‘Let us go somewhere else, into the country towns nearby so that I can make my proclamation in them also; for that was why I came.’
Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
39 And he went about making his proclamation in their synagogues all through Galilee, and driving out the demons.
Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40 One day a leper came to Jesus and, falling on his knees, begged him for help. ‘If only you are willing,’ he said, ‘you are able to make me clean.’
Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
41 Moved with compassion, Jesus stretched out his hand and touched him, saying as he did so, ‘I am willing; become clean.’
Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
42 Instantly the leprosy left the man, and he became clean;
Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
43 and then Jesus, after sternly warning him, immediately sent him away,
Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
44 and said to him, ‘Be careful not to say anything to anyone; but go and show yourself to the priest, and make the offerings for your cleansing directed by Moses, as evidence of your cure.’
“Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
45 The man, however, went away, and began to speak about it publicly, and to spread the story so widely, that Jesus could no longer go openly into a town, but stayed outside in lonely places; and people came to him from every direction.
Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.

< Mark 1 >