< Luke 4 >

1 On returning from the Jordan, full of the Holy Spirit, Jesus was led by the power of the Spirit through the wilderness for forty days, tempted by the devil.
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 All that time he ate nothing; and, when it was over, he became hungry.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 So the devil said to him, ‘If you are God’s Son, tell this stone to become a loaf of bread.’
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 And Jesus answered him, ‘Scripture says – “It is not on bread alone that a person is to live.”’
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 And the devil led Jesus up, and showing him in a single moment all the kingdoms of the earth, said to him,
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 ‘I will give you all this power, and the splendour of them; for it has been given into my hands and I give it to whom I wish.
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 If you worship me, it will all be yours.’
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 And Jesus answered him, ‘Scripture says – “You should worship the Lord your God, and worship him only.”’
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 The devil next led him into Jerusalem, and, placing him on the parapet of the Temple, said, ‘If you are God’s Son throw yourself down from here,
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 for scripture says – “He will give his angels commands about you, to guard you safely,”
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 And “On their hands they will lift you up, otherwise you might strike your foot against a stone.”’
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 But Jesus answered him, ‘It is said – “You must not tempt the Lord your God.”’
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 When he had tried every kind of temptation, the devil left Jesus, until another opportunity.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 Moved by the power of the Spirit, Jesus returned to Galilee. Reports about him spread through all that region;
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 and he began to teach in their synagogues, and was honoured by everyone.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 Coming to Nazareth, where he had been brought up, Jesus, as was his custom, went on the Sabbath into the synagogue, and stood up to read the scriptures.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 He was given the book of the prophet Isaiah; and Jesus opened the book and found the place where it says –
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 “The Spirit of the Lord is on me, for he has consecrated me to bring good news to the poor, he has sent me to proclaim release to captives and restoration of sight to the blind, to set the oppressed at liberty,
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 to proclaim the year of the Lord’s favour.”
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 Then, closing the book and returning it to the attendant, he sat down. The eyes of all in the synagogue were fixed on him,
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 and Jesus began, ‘This very day this passage has been fulfilled in your hearing.’
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 All who were present spoke well of him, and were astonished at the beautiful words that fell from his lips. ‘Isn’t Joseph’s son?’ they asked.
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 ‘Doubtless,’ said Jesus, ‘you will remind me of the saying – “Doctor, cure yourself;” and you will say “Do here in your own country all that we have heard that has been done at Capernaum.”
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 I tell you,’ he continued, ‘that no prophet is acceptable in his own country.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 There were, doubtless, many widows in Israel in Elijah’s days, when the heavens were closed for three years and six months, and a severe famine prevailed throughout the country;
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 and yet it was not to one of them that Elijah was sent, but to a widow at Zarephath in Sidonia.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 And there were many lepers in Israel in the time of the prophet Elisha, yet it was not one of them who was made clean, but Naaman the Syrian.’
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 All the people in the synagogue, as they listened to this, became enraged.
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 Starting up, they drove Jesus out of the town, and led him to the brow of the hill on which their town stood, intending to hurl him down.
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 But he passed through the middle of the crowd and went on his way.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 Then Jesus went down to Capernaum, a city in Galilee. On the Sabbath he taught the people.
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 They were amazed at his teaching, because his words were spoken with authority.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 In the synagogue there was a man with the spirit of a foul demon in him, who called out loudly,
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 ‘Stop! What do you want with us, Jesus of Nazareth? Have you come to destroy us? I know who you are – the Holy One of God!’
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 But Jesus rebuked the demon. ‘Be silent! Come out from him,’ he said. The demon flung the man down in the middle of the people, and then came out from him, without causing him further harm.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 And they were all lost in amazement, and kept saying to one another, ‘What words are these? For he gives his commands to the foul spirits with a marvellous authority, and they come out.’
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 And rumours about Jesus traveled through every place in the region.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 On leaving the synagogue, Jesus went into Simon’s house. Now Simon’s mother-in-law was suffering from a severe attack of fever, and they asked Jesus to cure her.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 Bending over her, he rebuked the fever; the fever left her, and she immediately got up and began to take care of them.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 At sunset, all who had friends suffering from various diseases took them to Jesus; and he placed his hands on everyone of them and cured them.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 And even demons came out from many people, screaming “You are the Son of God.” Jesus rebuked them, and would not allow them to speak, because they knew that he was the Christ.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 At daybreak, Jesus went out and walked to a lonely spot. But crowds of people began to look for him; and they came to where he was and tried to detain him and prevent his leaving them.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 Jesus, however, said to them, ‘I must take the good news of the kingdom of God to the other towns too, for that was why I was sent.’
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 And he continued to make his proclamation in the synagogues of Judea.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luke 4 >