< Luke 3 >

1 In the fifteenth year of the reign of the Emperor Tiberius, when Pontius Pilate was governor of Judea, Herod ruler of Galilee, his brother Philip ruler of the territory comprising Ituraea and Trachonitis, and Lysanias ruler of Abilene,
Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2 and when Annas and Caiaphas were high priests, a command from God came to John, the son of Zechariah, while he was in the wilderness.
na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
3 And John went through the whole district of the Jordan, proclaiming a baptism of repentance, for the forgiveness of sins.
Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
4 This was in fulfilment of what is said in the writings of the prophet Isaiah – “The voice of one crying aloud in the wilderness: ‘Make ready the way of the Lord, make his paths straight.
Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
5 Every chasm will be filled, every mountain and hill will be levelled. The winding ways will be straightened, the rough roads made smooth,
Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
6 and everyone will see the salvation of God.’”
Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu.”
7 And John said to the crowds that went to be baptized by him, ‘You children of snakes! Who has prompted you to seek refuge from the coming judgment?
Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: “Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
8 Let your lives, then, prove your repentance; and do not begin to say among yourselves “Abraham is our ancestor,” for I tell you that out of these stones God is able to raise descendants for Abraham!
Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
9 Already, indeed, the axe is lying at the root of the trees. Therefore every tree that fails to bear good fruit will be cut down and thrown into the fire.’
Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.”
10 ‘What are we to do then?’ the people asked.
Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi?”
11 ‘Let anyone who has two coats,’ answered John, ‘share with the person who has none; and anyone who has food do the same.’
Akawajibu, “Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo.”
12 Even tax collectors came to be baptized, and said to John, ‘Teacher, what are we to do?’
Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, “Mwalimu, tufanye nini?”
13 ‘Do not collect more than you have authority to demand,’ John answered.
Naye akawaambia, “Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa.”
14 And when some soldiers on active service asked ‘And we – what are we to do?’ he said, ‘Never use violence, or exact anything by false accusation; and be content with your pay.’
Nao askari wakamwuliza, “Na sisi tufanye nini?” Naye akawajibu, “Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu.”
15 Then, while the people were in suspense, and were all debating with themselves whether John could be the Christ,
Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
16 John, addressing them all, said, ‘I, indeed, baptize you with water; but there is coming one more powerful than I, and I am not fit even to unfasten his sandals. He will baptize you with the Holy Spirit and with fire.
Hapo Yohane akawaambia wote, “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 His winnowing-fan is in his hand so that he may clear his threshing-floor, and store the grain in his barn, but the chaff he will burn with a fire that cannot be put out.’
Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika.”
18 And so with many different appeals John told his good news to the people.
Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
19 But when John rebuked Herod the ruler, for Herodia his brother’s wife, and for all the evil things that he had done,
Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
20 Herod crowned them all by shutting John up in prison.
Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
21 Now after the baptism of all the people, and when Jesus had been baptized and was still praying, the heavens opened,
Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
22 and the Holy Spirit came down on him in the form of a dove, and from the heavens came a voice – ‘You are my dearly loved son; you bring me great joy.’
na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
23 When beginning his work, Jesus was about thirty years old. He was regarded as the son of Joseph, whose ancestors were – Eli,
Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
24 Mattith, Levi, Melchiah, Janna, Joseph,
Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
25 Mattithiah, Amos, Nahum, Azaliah, Nogah,
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
26 Mattith, Mattithiah, Shimei, Joseph, Josheh,
mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
27 Johanan, Rhesa, Zerubbabel, Salathiel, Neriah,
mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 Melchiah, Addi, Cosam, Elmodam, Er,
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 Joshua, Eliezer, Joram, Mattith, Levi,
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
30 Simeon, Judah, Joseph, Jonam, Eliakim,
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
31 Meleah, Menan, Mattithiah, Nathan, David,
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 Jesse, Obed, Boaz, Salah, Nahshon,
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 Aminadab, Arni, Hezron, Perez, Judah,
mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
34 Jacob, Isaac, Abraham, Terah, Nahor,
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 Serug, Reu, Peleg, Eber, Shelah,
mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 Kenan, Arpachshad, Shem, Noah, Lamech,
mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
37 Methuselah, Enoch, Jared, Mahalalel, Kenan,
mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
38 Enosh, Seth, son of Adam, and Adam, son of God.
mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.

< Luke 3 >