< Hosea 6 >

1 saying, ‘Come let us return to the Lord, for he has torn us but he will heal us, he has injured us but he will bandage our wounds,
“Njoo, turudi kwa Bwana. Kwa maana ametuvunja vipande vipande, lakini atatuponya; ametujeruhi, lakini atatufunga majeraha yetu.
2 he will revive in a couple of days, on the third day he will raise us up again, to live in his presence.
Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, na tutaishi mbele yake.
3 Let us know, let us eagerly seek to know the Lord. His coming is as sure as the sunrise. He will come to us like the winter rain, as the spring rain that waters the earth.’
Nasi tumjue Bwana; tukaendelee kumjua Bwana. Kuja kwake ni hakika kama asubuhi; atakuja kwetu kama mvua, kama mvua ya vuli ambayo huinyeshea ardhi.”
4 What can I make of you, Ephraim! What can I make of you, Judah! Your love is like a morning cloud, like the dew which early goes away.
Efuraimu, nikufanyie nini? Yuda, nikufanyie nini? Uaminifu wako ni kama wingu la asubuhi, kama umande unaoondoka mapema.
5 That is why I have hewn them by the prophets, I have slain them by the words of my mouth. My judgment is like the light that goes forth,
Kwa hiyo nimewavunja vipande vipande kwa vinywa vya manabii, nimewaua kwa maneno ya kinywa changu. Maagizo yako ni kama nuru inayoangaza.
6 for it is love that I delight in and not sacrifice, and knowledge of God and not burnt offerings.
Kwa maana natamani uaminifu wala si dhabihu, na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.
7 But they after the manner of men have transgressed the covenant, there they have played me false.
Kama Adamu wamevunja agano; hawakuwa waaminifu kwangu.
8 Gilead is a city of evildoers, tracked with bloody footprints,
Gileadi ni jiji la wahalifu wenye miguu ya damu.
9 and as bandits lie in wait for a man, so a band of priests murder on the way to Shechem. How terrible is the evil they do!
Kama makundi ya wanyang'anyi wanaomngojea mtu, hivyo makuhani hujiunga pamoja kufanya mauaji kwa njia ya Shekemu; wamefanya uhalifu wa aibu.
10 In Bethel I have seen a horrible thing. There Ephraim plays the prostitute, Israel is defiled.
Katika nyumba ya Israeli nimeona jambo baya; Uzinzi wa Efraimu ukopale, na Israeli ametiwa unajisi.
11 Judah for you also a harvest is set. When I would restore the fortunes of my people,
Kwa maana wewe, Yuda, mavuno yameteuliwa, nitakaporudisha urithi wa watu wangu.

< Hosea 6 >