< Hosea 4 >

1 Hear the Lord’s message, Israelites, for the Lord has brought charges against the inhabitants of the land, for there is no fidelity, nor true love, nor knowledge of God in the land,
Sikilizeni neno la Bwana, enyi watu wa Israeli. Bwana ana mashtaka dhidi ya wenyeji wa nchi, kwa sababu hakuna ukweli au uaminifu wa agano, hakuna ujuzi wa Mungu katika nchi.
2 but cursing, lying, and murder, stealing, committing adultery, and deeds of violence, and acts of bloodshed quickly follow each other.
Kuna laana, uongo, mauaji, wizi na uzinzi. Watu wamevunja mipaka yote, na damu inakuja baada ya damu.
3 Therefore the land mourns, all its inhabitants languish, the wild animals and the birds of the skies, even the fish of the sea are dying.
Kwa hiyo nchi inakauka, na kila mtu aliyeishi ndani yake anaangamia; wanyama katika mashamba na ndege angani, hata samaki katika bahari, wanaondolewa.
4 Yet let no one bring charges, let none accuse, for your people are like those, who bring charges against a priest.
Lakini usiruhusu mtu yeyote kuleta mashtaka; msiruhusu mtu yeyote ahukumu mtu mwingine. Kwa maana ninyi ndio makuhani, ninaowashtaki.
5 You stumble by day, and the prophet stumbles with you by night, and I will destroy your mother.
Ninyi makuhani mtajikwaa wakati wa mchana; manabii pia watajikwaa pamoja nanyi usiku, nami nitamwangamiza mama yako.
6 My people are being destroyed for lack of knowledge; because you have rejected knowledge I reject you from being priest to me. Since you have forgotten the teaching of your God, I also will forget your children.
Watu wangu wanaharibiwa kwa sababu ya ukosefu wa maarifa. Kwa sababu makuhani wamekataa maarifa, nami nitawakataa msiwe makuhani kwangu. Kwa sababu umesahau sheria yangu, ingawa mimi ni Mungu wako, nami pia nitasahau watoto wako.
7 The more priests there are, the more they sin against me. I will change their dignity to dishonour.
Makuhani wengi waliongezeka, zaidi walifanya dhambi dhidi yangu. Walibadilisha heshima zao kwa aibu.
8 They feed on the sin offerings of my people, so they hunger after their guilt.
Wanajilisha dhambi ya watu wangu; wao ni wenye tamaa zaidi ya uovu wao.
9 Thus it comes to be, like people, like priest: I will visit upon each punishment for their ways, and their deeds I will repay them.
Itakuwa sawa kwa watu kama kwa makuhani: nitawaadhibu wote kwa matendo yao; Nitawalipa kwa matendo yao.
10 They will eat and not be satisfied, they will sleep around but stay childless, because they have abandoned the Lord to give themselves to
Watakula lakini hawatashiba; watafanya uzinzi lakini hawataongezeka, kwa sababu wamekwenda mbali na Bwana.
11 prostitution. Old and new wine take away the understanding.
Wanapenda uasherati, divai, na divai mpya, ambayo imechukua uelewa wao.
12 My own people ask counsel of a piece of wood! A stick gives them advice! For a spirit of prostitution has led them astray, they commit adultery against their God.
Watu wangu hutaka shauri kwa sanamu zao za mbao, na fimbo zao za kutembelea huwapa unabii. Kwa maana mawazo ya uasherati yamewadanganya, na wamefanya kama makahaba badala ya kuwa mwaminifu kwa Mungu wao.
13 On the heights of the mountains they sacrifice, and on the hills they burn incense under oaks and poplars and terebinths, for their shade is so pleasant. Therefore your daughters become cult prostitutes, and your daughters-in-law commit adultery.
Wanatoa sadaka juu ya milima na kuteketeza uvumba kwenye milima, chini ya mialoni, milibua na miela, kwa sababu kivuli ni nzuri. Basi binti zenu hufanya uasherati, na binti zenu wanazini.
14 I will not punish your daughters for committing prostitution, nor your daughters-in-law for adultery. Your men visit prostitutes, sacrifice with cult prostitutes. So a people without understanding come to ruin!
Mimi siwaadhibu binti zako wakati wanachagua kutenda uasherati, wala binti zako wakati wazini. Kwa maana wanaume pia wanajitoa kwa makahaba, na hutoa dhabihu ili waweze kufanya vitendo vya uasherati na makahaba. Hivyo watu wasiofahamu wataangamizwa.
15 Though you commit adultery, Israel, let not Judah become guilty. Do not go to Gilgal, do not go up to Beth-aven, nor swear an oath, ‘As the Lord lives.’
Ingawa wewe, Israeli, umefanya uzinzi, lakini Yuda asiwe na hatia. Ninyi msiende Gilgali; msiende hadi Beth Aven. Wala msiape, “Aishivyo Bwana.”
16 Like a wilful heifer, Israel is stubborn. Can the Lord now feed them as he would a lamb in a broad pasture?
Kwa maana Israeli amefanya ukaidi, kama ndama mkaidi. Je! Bwana anaweza kuwaleta kwenye malisho kama kondoo mahali penye nafasi?
17 Ephraim is wedded to idols. Leave them alone!
Efraimu alijiunga na sanamu; mwache peke yake.
18 When their drinking is over they sleep with the cult prostitutes, their rulers love shameful ways.
Hata wakati kileo chao kimeondoka wakaendelea kufanya uzinzi; watawala wake hupenda sana aibu yao.
19 A windstorm will wrap them in its wings and they will be ashamed of their sacrifices.
Upepo utamfunga kwa mabawa yake; nao wataona aibu kwa sababu ya dhabihu zao.

< Hosea 4 >