< Esther 7 >

1 So the king and Haman went to drink with Queen Esther.
Kwa hiyo mfalme na Hamani wakaenda kausherekea na malkia Esta.
2 As they were drinking wine on that second day, the king again said to Esther, ‘Whatever your petition is, Queen Esther, it will be granted to you. Whatever you request it will be done, even if it takes half of the kingdom.’
Katika siku ya pili, baada ya kuletwa mvinyo, mfalme akamwambia Esta, “Ni nini haja ya moyo wako? Na nini ombi lako? Hata nusu ya ufalme wangu utapewa.”
3 Then Queen Esther answered, ‘Your Majesty, if I have won your favour, and if it seems best to Your Majesty, let my life be given me as my petition, and my people as my request,
Kisha Malkia amwambia mfalme, kama nimepata kibali machoni pako, na kama ikikupendeza, nipewe maisha yangu, na hili ndio haja ya moyo wangu, na hili pia ni ombi kwa watu wangu pia.
4 for I and my people have been sold to be destroyed, killed, and completely annihilated! If we had been merely sold into slavery I would not have disturbed your peace, because such a fate would not have affected the interests of the king.’
Kwa kuwa mimi na watu wangu tumeuzwa, ili tuharibiwe, tuuwawe, na tungamizwe. Kama tungeuzwa utumwani, kama wanaume na wanawake, ningenyamaza kimya, na nisingeweza kumsumbua mfame.”
5 Then King Ahasuerus said to Queen Esther, ‘Who is he and where is he whose heart has impelled him to do this?’
Kisha Mfalme Ahusiero akamwambia malkia Esta, “Ni nani huyo? Ni nani aliyekusudia moyoni mwake kutenda jambo hili?
6 ‘A foe, an enemy: this wicked Haman.’ Esther answered. Haman shrank in terror before the king and the queen.
Esta akasema, “Ni huyu mwovu Hamani, adui!” Hamani akashikwa na Hofu mbele za mfalme na malkia.
7 In his wrath the king rose from the place where he was drinking wine and went into the palace garden. Haman stayed to beg Queen Esther for his life, for he saw that the king was fully determined to bring calamity upon him.
Na kwa ghadhabu mfalme akatoka karamuni katika sehemu ya mvinyo na akaenda katika bustani ya ikulu, Lakini Hamani alibaki akimsihi Malkia Esta ili aokoe maisha yake. Kwa sababu aliona mfalme amemkusudia ubaya.
8 As the king returned from the palace garden to the banquet hall, Haman had flung himself on Esther’s couch. The king cried, ‘Is he going to rape my queen while I am present in my own house?’ As the king spoke these words, the attendants covered Haman’s face
Mfalme akarudi kutoka katika bustani ya ikulu, na kuingia katika chumba ambamo kulikuwamo mvinyo. Hamani alikuwa ameanguka chini ya kochi alilokuwa ameketi Esta. Mfalme akakasirika na kusema, “atamdharirisha malkia mbele zangu katika nyumba yangu?” Mara tu maneno haya yalipotoka kinywani mwa mfalme, watumizhi wakafunika uso wa Hamani.
9 and Harbonah, one of those who waited on the king, said, ‘There are the gallows, seventy-five feet high, which Hainan erected for Mordecai, who spoke a good word in behalf of the king, standing in the house of Haman!’ The king said ‘Hang him on them.’
Kisha Habona, mmoja wa watumishi aliye mtumikia mfalme akamwambia mfalme, “Mti wenye urefu wa futi hamsini uko nyumbani kwa Hamani. Ulikuwa umeandaliwa kwa ajili ya Modekai, aliye toa taarifa kuhusu mpango wa kuangamizwa kwako.” Mfalme akesema,”Mtundikeni Hamani juu yake.”
10 So they hanged Haman on the gallows that he had prepared for Mordecai. Then the wrath of the king was pacified.
Kwa hiyo wakamtundika Hamani kwenye mti aliuandaa kwa ajili ya Modekai. Na hasira ya mfalme ikatulia.

< Esther 7 >