< Amos 7 >

1 This is what the Lord God showed me: he was forming a swarm of locusts, when the late spring grass began to come up after the king’s share had been harvested.
Hivi ndivyo ambavyo Bwana Yahwe alivyonionyesha. Tazama, aliumba kundi kubwa la nzige wakati wa kuchipuka kwa mmea, na, tazama, ulikuwa ni mmea wa mwisho baada ya mavuno ya mfalme.
2 And when they had finished devouring all the land’s vegetation, I said: ‘Lord God, forgive, I beg you! How can Jacob survive, for he is so helpless?’
Wakati walipomaliza kula mbogamboga za nchi, kisha nikasema, “Bwana Yahwe, tafadhali nisamehe; Je Yakobo ataishije? kwa kuwa yeye ni mdogo sana.”
3 The Lord relented. This will not happen,’ said the Lord.
Yahwe akapunguza hasira kuhusu hili. “Haitatokea,” akasema.
4 This is what he showed me: the Lord God was giving command to execute judgment by fire. It burned up the great deep, and had begun to devour the fields, and I said:
Hivi ndivyo ambavyo Bwana Yahwe alivyonionyesha: Tazama, Bwana Yahwe aliita juu ya moto kuhukumu. Nao ukakausha sana, kilindi chini ya dunia na kutaka kuitekeza nchi, pia.
5 ‘Lord God, forgive, I beg you! How can Jacob survive, for he is so helpless?’
Lakini nikasema, “Bwana Yahwe, acha tafadhali; Yakobo ataishije? Kwa kuwa yeye ni mdigo sana.”
6 The Lord relented. ‘This will not happen either,’ said the Lord.
Yahwe akagairi kuhusiana na hili, “Hili halitajitokeza pia,” asema Bwana Yahwe.
7 This is what the Lord God showed me: the Lord was standing beside a wall built with a plumb line, with a plumb line in his hand.
Hivi ndivyo ambavyo Yahwe alivyo nionyesha: Tazama, Bwana amesimama karibu na ukuta, pamoja na uzi wa timiza kwenye mkono wake.
8 And the Lord said to me, ‘What do you see, Amos?’ And I answered, ‘A plumb line,’ Then the Lord said, ‘Watch: I am setting a plumb line in the midst of my people Israel, I will no longer overlook their crookedness.
Yahwe akanambia, “Amosi, unaona nini?” nikasema, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, nitaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli. Sintowaharibu tena.
9 And the high places of Isaac will be desolate, the sanctuaries of Israel will be laid waste, and I will rise up against the house of Jeroboam with the sword.’
Mahala pa juu pa Isaka pataharibiwa, patakatifu pa Israeli pataangamia, na nitainuka juu ya nyumba ya Yeroboamu kwa upanga.”
10 Then Amaziah, chief priest of Bethel sent this message to King Jeroboam of Israel: ‘Amos has conspired against you right in the heart of Israel. The country cannot survive all his words.
Kisha Amazia, yule kuhani wa Betheli, akatuma ujumbe kwa Yeroboamu, mfalme wa Israeli: “amosi amefanya njama dhidi yako katikati ya nyumba ya Israeli. Nchi haiwezi kubeba maneno yote haya.
11 Amos has said, “Jeroboam will die by the sword, and Israel will be led away captive out of their land.”’
Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Amosi, 'Yeroboamu atakufa kwa upanga, na hakika Israeli itakwenda utumwani kutoka nchi yake.”'
12 And Amaziah said to Amos, ‘Leave, you who see visions, go to the land of Judah. Earn your bread there and prophesy there,
Amazia akamwambia Amosi, “Mwonaji, nenda, kimbia irudie nchi ya Yuda, na hapo ule mkate na kutabiri.
13 but don’t prophesy any more at Bethel, for it is the king’s sanctuary, and it is the royal residence.’
Lakini usitabiri tena hapa katika Betheli, kwa kuwa ni patakatifu pa mfalme na nyumba ya kifalme.”
14 ‘I am no prophet,’ Amos answered Amaziah, ‘nor trained as one. I am a shepherd and a keeper of sycamores fig trees.
Kisha Amosi akamwambia Amazia, “Mimi sio nabii wala mwana wa nabii. Mimi ni mchungaji wa mifugo, na mtunza mikuyu.
15 But the Lord took me away from following the flock, and the Lord said to me, “Go, prophesy to my people Israel.”
Lakini Yahwe akanichukua kutoka kuchunga mifugo na kunambia, 'Nenda, katabiri kwa watu wangu Israeli.'
16 Now therefore listen to the Lord’s message: “You say not to prophesy against Israel, nor to preach against the house of Isaac.
Sasa sikia neno la Yahwe. Wewe usemaye, 'Usitabiri juu ya Israeli, na usiongee juu ya nyumba ya Isaka.
17 But the Lord says: Your wife will become a prostitute in the city, your sons and your daughters will fall by the sword, your land will be divided up, you will die on unclean soil, and Israel will be led away captive out of their land.”’
Kwa hiyo hivi ndivyo Yahwe asemavyo, 'Mke wako atakuwa kahaba katika mji; wana wako waume na binti zako wataanguka kwa upanga; nchi yako itapimwa na kugawanywa; utakufa katika nchi najisi, na Israeli hakika itakwenda utumwani kutoka nchi yake.”'

< Amos 7 >