< Acts 20 >

1 When the uproar had ceased, Paul sent for the disciples, and, with encouraging words, bade them goodbye, and started on his journey to Macedonia.
Ile ghasia ya Efeso ilipokwisha tulia Paulo aliwaita pamoja wale waumini, akawatia moyo. Kisha akawaaga, akasafiri kwenda Makedonia.
2 After going through those districts and speaking many encouraging words to the disciples, he went into Greece, where he stayed three months.
Alipitia sehemu za nchi zile akiwatia watu moyo kwa maneno mengi. Halafu akafika Ugiriki.
3 He was about to sail to Syria, when he learned that a plot had been laid against him by several of the Jewish leaders; so he decided to return by way of Macedonia.
ambako alikaa kwa miezi mitatu. Alipokuwa anajitayarisha kwenda Siria, aligundua kwamba Wayahudi walikuwa wanamfanyia mpango mbaya; hivyo aliamua kurudi kwa kupitia Makedonia.
4 He was accompanied by Sopater the son of Pyrrhus, of Beroea, Aristarchus and Secundus from Thessalonica, Gaius of Derbe, and Timothy, as well as by Tychicus and Trophimus of Roman Asia.
Sopatro, mwana wa Pirho kutoka Berea, aliandamana naye; pia Aristarko na Sekundo kutoka Thesalonika, Gayo kutoka Derbe, Timotheo, Tukiko na Trofimo wa mkoa wa Asia.
5 These people went to Troas and waited for us there;
Hao walitutangulia na kutungojea kule Troa.
6 while we ourselves sailed from Philippi after the Passover, and joined them five days later at Troas, where we stayed for a week.
Sisi, baada ya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, tulipanda meli kutoka Filipi na baada ya siku tatu tukawafikia kule Troa. Huko tulikaa kwa muda wa juma moja.
7 On the first day of the week, when we had met for the breaking of bread, Paul, who was intending to leave the next day, began to address those who were present, and prolonged his address until midnight.
Jumamosi jioni, tulikutana ili kumega mkate. Kwa vile Paulo alikuwa amekusudia kuondoka kesho yake, aliwahutubia watu na kuendelea kuongea nao hadi usiku wa manane.
8 There were a good many lamps in the upstairs room, where we had met;
Katika chumba tulimokuwa, ghorofani, kulikuwa na taa nyingi zinawaka.
9 and a young man named Eutychus, sitting at the window, was gradually overcome with great drowsiness, as Paul continued his address. At last, quite overpowered by his drowsiness, he fell from the third story to the ground, and was picked up for dead.
Kijana mmoja aitwaye Eutuko alikuwa ameketi dirishani wakati Paulo alipokuwa anaendelea kuhutubu. Eutuko alianza kusinzia kidogokidogo na hatimaye usingizi ukambana, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu. Wakamwokota amekwisha kufa.
10 But Paul went down, threw himself on him, and put his arms round him. ‘Do not be alarmed,’ he said, ‘he is still alive.’
Lakini Paulo alishuka chini, akainama, akamkumbatia na kusema, “Msiwe na wasiwasi maana kuna uhai bado ndani yake.”
11 Then he went upstairs; and, after breaking and partaking of the bread, he talked with them at great length until daybreak, and then left.
Kisha akapanda tena ghorofani, akamega mkate, akala. Aliendelea kuhubiri kwa muda mrefu hadi alfajiri, halafu akaondoka.
12 Meanwhile they had taken the lad away alive, and were greatly comforted.
Wale watu walimchukua yule kijana nyumbani akiwa mzima kabisa, wakapata kitulizo kikubwa.
13 We started first, went on board ship, and sailed for Assos, intending to take Paul on board there. This was by his own arrangement, as he intended to go by land himself.
Sisi tulipanda meli tukatangulia kwenda Aso ambako tungemchukua Paulo. Ndivyo alivyopanga; maana alitaka kufika huko kwa kupitia nchi kavu.
14 So, when he met us at Assos, we took him on board and went on to Mitylene.
Basi, alitukuta kule Aso, tukampandisha melini, tukaenda Mitulene.
15 The day after we had sailed from there, we arrived off Chios, touched at Samos the following day, and the next day reached Miletus;
Kutoka huko tulisafiri tukafika Kio kesho yake. Siku ya pili, tulitia nanga Samo na kesho yake tukafika Mileto.
16 for Paul had decided to sail past Ephesus, so as to avoid spending much time in Roman Asia. He was making haste to reach Jerusalem, if possible, by the Festival at the close of the Harvest.
Paulo alikuwa amekusudia kuendelea na safari kwa meli bila kupitia Efeso ili asikawie zaidi huko Asia. Alikuwa na haraka ya kufika Yerusalemu kwa sikukuu ya Pentekoste kama ingewezekana.
17 From Miletus, however, he sent to Ephesus and invited the church elders to meet him;
Kutoka Mileto Paulo alituma ujumbe kwa wazee wa Efeso wakutane naye.
18 and, when they came, he said to them, ‘You know well the life that I always led among you from the very first day that I set foot in Roman Asia,
Walipofika kwake aliwaambia, “Mnajua jinsi nilivyotumia wakati wote pamoja nanyi tangu siku ile ya kwanza nilipofika Asia.
19 serving the Lord, as I did, in all humility, amid the tears and trials which fell to my lot through the plots of some of the Jewish leaders.
Mnajua jinsi nilivyomtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote, kwa machozi na matatizo yaliyonipata kutokana na mipango ya hila ya Wayahudi.
20 I never shrank from telling you anything that could be helpful to you, or from teaching you both in public and in private.
Mnajua kwamba sikusita hata kidogo kuwahubiria hadharani na nyumbani mwenu na kuwafundisha chochote ambacho kingewasaidieni.
21 I earnestly pointed both Jews and Greeks to the repentance that leads to God, and to faith in Jesus, our Lord.
Niliwaonya wote—Wayahudi kadhalika na watu wa mataifa, wamgeukie Mungu na kumwamini Bwana wetu Yesu.
22 And now, under spiritual constraint, I am here on my way to Jerusalem, not knowing what will happen to me there,
Sasa, sikilizeni! Mimi, nikiwa ninamtii Roho, nakwenda Yerusalemu bila kufahamu yatakayonipata huko.
23 except that in town after town the Holy Spirit plainly declares to me that imprisonment and troubles await me.
Ninachojua tu ni kwamba Roho Mtakatifu ananithibitishia katika kila mji kwamba vifungo na mateso ndivyo vinavyoningojea.
24 But I count my life of no value to myself, if only I may complete the course marked out for me, and the task that was allotted me by the Lord Jesus – which was to declare the good news of the love of God.
Lakini, siuthamini uhai wangu kuwa ni kitu sana kwangu. Nataka tu nikamilishe ule utume wangu na kumaliza ile kazi aliyonipa Bwana Yesu niifanye, yaani nitangaze Habari Njema ya neema ya Mungu.
25 And now, I tell you, I know that none of you will ever see my face again – you among whom I have gone about proclaiming the kingdom.
“Nimekuwa nikienda huko na huko kati yenu nikiuhubiri Ufalme wa Mungu. Sasa lakini, najua hakuna hata mmoja wenu atakayeniona tena.
26 Therefore I declare to you this day, that my conscience is clear in regard to the fate of any of you,
Hivyo, leo hii ninawathibitishieni rasmi kwamba ikijatokea akapotea mmoja wenu, mimi sina lawama yoyote.
27 for I have not shrunk from announcing the whole purpose of God regarding you.
Kwa maana sikusita hata kidogo kuwatangazieni azimio lote la Mungu.
28 Be watchful over yourselves, and over the whole flock, of which the Holy Spirit has placed you in charge, to shepherd the church of God, which he won for himself at the cost of his life.
Jihadharini wenyewe; lilindeni lile kundi ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi muwe walezi wake. Lichungeni kanisa la Mungu ambalo amejipatia kwa damu ya Mwanae.
29 I know that, after my departure, merciless wolves will get in among you, who will not spare the flock;
Nafahamu vizuri sana kwamba baada ya kuondoka kwangu mbwa mwitu wakali watawavamieni, na hawatakuwa na huruma kwa kundi hilo.
30 and from among yourselves, too, people will arise, who will teach perversions of truth, so as to draw away the disciples after them.
Hata kutoka miongoni mwenu watatokea watu ambao watasema mambo ya uongo ili kuwapotosha watu na kuwafanya wawafuate wao tu.
31 Therefore, be on your guard, remembering how for three years, night and day, I never ceased, even with tears, to warn each one of you.
Kwa hiyo, muwe macho mkikumbuka kwamba kwa muda wa miaka mitatu, usiku na mchana, sikuchoka kumwonya kila mmoja wenu kwa machozi.
32 And now I commend you to the Lord and to the message of his love – a message which has the power to build up your characters, and to give you your place among all those who have become Christ’s people.
“Na sasa basi, ninawaweka ninyi chini ya ulinzi wa Mungu na ujumbe wa neema yake. Yeye anao uwezo wa kuwajenga ninyi na kuwawezesha mzipate zile baraka alizowawekea watu wake.
33 I have never coveted anyone’s gold or silver or clothing.
Mimi sikutamani hata mara moja fedha, wala dhahabu, wala nguo za mtu yeyote.
34 You, yourselves, know that these hands of mine provided not only for my own wants, but for my companions also.
Mnajua ninyi wenyewe kwamba nimefanya kazi kwa mikono yangu mwenyewe, ili kujipatia mahitaji yangu na ya wenzangu.
35 I left nothing undone to show you that, labouring as I laboured, you ought to help the weak, and to remember the words of the Lord Jesus, how he said himself – “It is more blessed to give than to receive.”’
Nimekuwa nikiwapeni daima mfano kwamba kwa kufanya kazi mithili hiyo tunapaswa kuwasaidia walio dhaifu, tukikumbuka maneno ya Bwana Yesu mwenyewe: Heri zaidi kutoa kuliko kupokea.”
36 When Paul had finished speaking, he knelt down and prayed with them all.
Baada ya kusema hayo, Paulo alipiga magoti pamoja nao wote, akasali.
37 All were in tears; and throwing their arms round Paul’s neck, they kissed him again and again,
Wote walikuwa wanalia; wakamwaga kwa kumkumbatia na kumbusu.
38 grieving most of all over what he had said – that they would never see his face again. Then they escorted him to the ship.
Jambo lililowahuzunisha zaidi lilikuwa neno alilosema kwamba hawangemwona tena. Basi, wakamsindikiza hadi melini.

< Acts 20 >