< Acts 18 >

1 On leaving Athens, Paul next went to Corinth.
Baada ya hayo, Paulo aliondoka Athene, akaenda Korintho.
2 There he met a Jew of the name of Aquila, from Pontus, who, with his wife Priscilla, had lately come from Italy, in consequence of the order which had been issued by the Emperor Claudius for all Jews to leave Rome. Paul paid them a visit,
Huko Korintho, alimkuta Myahudi mmoja aitwaye Akula, mzaliwa wa Ponto. Akula pamoja na mkewe aitwaye Priskila, walikuwa wamerudi kutoka Italia siku hizohizo kwa sababu Kaisari Klaudio alikuwa ameamuru Wayahudi wote waondoke Roma. Paulo alikwenda kuwaona,
3 and, since their trade was the same as his, he stayed and worked with them – their trade was tent-making.
na kwa vile wao walikuwa mafundi wa kushona mahema kama alivyokuwa yeye, Paulo alikaa nao akafanya kazi.
4 Every Sabbath Paul gave addresses in the synagogue, trying to convince both Jews and Greeks.
Kila Sabato alifanya majadiliano katika sunagogi akijaribu kuwavuta Wayahudi na Wagiriki.
5 But, when Silas and Timothy had come down from Macedonia, Paul devoted himself entirely to delivering the message, earnestly maintaining before the Jews that Jesus was the Christ.
Baada ya Sila na Timotheo kuwasili kutoka Makedonia, Paulo alianza kutumia wakati wake wote kwa ajili ya kuhubiri, akawathibitishia Wayahudi kwamba Yesu ndiye Kristo.
6 However, as they set themselves against him and became abusive, Paul shook his clothes in protest and said to them, ‘Your blood be on your own heads. My conscience is clear. From this time forward I will go to the Gentiles.’
Walipompinga na kuanza kumtukana, aliyakung'uta mavazi yake mbele yao akisema, “Mkipotea ni shauri lenu wenyewe; mimi sina lawama yoyote juu ya jambo hilo. Na tangu sasa nitawaendea watu na mataifa mengine.”
7 So he left, and went to the house of a certain Titius Justus, who had been accustomed to join in the worship of God, and whose house was next door to the synagogue.
Basi, akatoka hapo akaenda kukaa nyumbani kwa mtu mmoja mcha Mungu aitwaye Tito Yusto. Nyumba yake Tito ilikuwa karibu na lile sunagogi.
8 Crispus, the synagogue leader, came to believe in the Lord, and so did all his household; and many of the Corinthians, as they listened to Paul, became believers in Christ and were baptized.
Lakini Krispo, mkuu wa sunagogi, alimwamini Bwana yeye pamoja na jamaa yake yote. Wakorintho wengi waliusikiliza ujumbe huo, wakaamini na kubatizwa.
9 One night the Lord said to Paul, in a vision, ‘Have no fear, but continue to speak, and refuse to be silenced;
Siku moja usiku, Bwana alimwambia Paulo katika maono: “Usiogope, endelea kuhubiri tu bila kufa moyo,
10 for I am with you, and no one will do you harm, for I have many people in this city.’
maana mimi niko pamoja nawe. Hakuna mtu atakayejaribu kukudhuru maana hapa mjini pana watu wengi walio upande wangu.”
11 So he settled there for a year and a half, and taught God’s message among the people.
Basi, Paulo alikaa huko akifundisha neno la Mungu kati yao kwa muda wa mwaka mmoja na nusu.
12 While Gallio was governor of Greece, some of the Jewish leaders made a combined attack on Paul, and brought him before the Governor’s Bench,
Lakini wakati Galio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Akaya, Wayahudi walimvamia Paulo kwa pamoja na kumpeleka mahakamani.
13 charging him with persuading people to worship God in a way forbidden by the Law.
Wakasema, “Tunamshtaki mtu huyu kwa sababu ya kuwashawishi watu wamwabudu Mungu kwa namna inayopingana na Sheria.”
14 Just as Paul was on the point of speaking, Gallio said to them, ‘If this were a case of misdemeanour or some serious crime, there would be some reason for my listening patiently to you;
Kabla tu Paulo hajaanza kusema, Galio aliwaambia Wayahudi, “Sikilizeni enyi Wayahudi! Kama kweli jambo hili lingekuwa juu ya uhalifu au uovu ningekuwa tayari kuwasikilizeni.
15 but, since it is a dispute about words, and names, and your own Law, you must see to it yourselves. I do not choose to be a judge in such matters.’
Lakini kama ni shauri la ubishi kuhusu maneno na majina ya Sheria yenu, amueni ninyi wenyewe. Mimi sitaki kuwa hakimu wa mambo haya!”
16 Saying this, he drove them back from the Bench.
Basi, akawafukuza kutoka mahakamani.
17 Then they all set on Sosthenes, the synagogue leader, and beat him in front of the Bench, but Gallio did not trouble himself about any of these things.
Nao wote wakamkamata Sosthene ambaye alikuwa kiongozi wa sunagogi, wakampiga palepale mbele ya mahakama. Lakini Galio hakujali kitendo hicho hata kidogo.
18 Paul remained there some time after this, and then took leave of the followers, and sailed to Syria with Priscilla and Aquila, but not before his head had been shaved at Cenchreae, because he was under a vow.
Paulo alikaa bado na wale ndugu huko Korintho kwa siku nyingi. Kisha aliwaaga, akapanda meli kwenda Siria pamoja na Priskila na Akula. Huko Kenkrea, alinyoa nywele zake kwa sababu ya nadhiri aliyokuwa ameweka.
19 They put into Ephesus, and there Paul, leaving his companions, went into the synagogue and addressed the Jews.
Walifika Efeso na hapo Paulo aliwaacha Priskila na Akula, akaenda katika sunagogi, akajadiliana na Wayahudi.
20 When they asked him to prolong his stay, he declined, saying however,
Walimwomba akae nao muda mrefu zaidi, lakini hakupenda.
21 as he took his leave, ‘I will come back again to you, please God,’ and then set sail from Ephesus.
Bali alipokuwa anaondoka, alisema, “Mungu akipenda nitakuja kwenu tena.” Akaondoka Efeso kwa meli.
22 On reaching Caesarea, he went up to Jerusalem and exchanged greetings with the church, and then went down to Antioch.
Meli ilitia nanga Kaisarea, naye Paulo akaenda Yerusalemu kulisalimia lile kanisa, kisha akaenda Antiokia.
23 After making some stay in Antioch, he set out on a tour through the Phrygian district of Galatia, strengthening the faith of all the disciples as he went.
Alikaa huko muda mfupi, halafu akaendelea na safari kwa kupitia sehemu za Galatia na Frugia akiwatia moyo wafuasi wote.
24 Meanwhile there had come to Ephesus an Alexandrian Jew, named Apollos, an eloquent man, who was well-versed in the scriptures.
Myahudi mmoja aitwaye Apolo, mzaliwa wa Aleksandria, alifika Efeso. Alikuwa mtu mwenye ufasaha wa kuongea na mwenye ujuzi mkubwa wa Maandiko Matakatifu.
25 He had been well-instructed in the Way of the Lord, and with burning zeal he spoke of, and taught carefully, the facts about Jesus, though he knew of no baptism but John’s.
Alikuwa amefundishwa juu ya hiyo njia ya Bwana, na akiwa motomoto, aliongea juu ya habari za Yesu. Akafundisha kwa usahihi ingawa alikuwa amepata ubatizo wa Yohane tu.
26 This man began to speak out fearlessly in the synagogue; and when Priscilla and Aquila heard him, they took him home and explained the Way of God to him more carefully still.
Priskila na Akula walipomsikia akiongea kwa uhodari ndani ya sunagogi, walimchukua kwao wakamfundisha hiyo Njia ya Mungu kwa usahihi zaidi.
27 When he wanted to cross to Greece, the followers furthered his plans, and wrote to the disciples there to welcome him. On his arrival he proved of great assistance to those who had, through the loving kindness of God, become believers in Christ,
Apolo alipoamua kwenda Akaya, wale ndugu walimtia moyo kwa kuwaandikia wafuasi kule Akaya wampokee. Alipofika huko, aliweza kwa msaada wa neema ya Mungu, kuwasaidia sana wale ndugu waliopata kuwa waumini;
28 for he vigorously confuted the Jews, publicly proving by the scriptures that Jesus was the Christ.
kwa maana aliendelea kwa uhodari kuwashinda Wayahudi hadharani akithibitisha kwa Maandiko Matakatifu kuwa Yesu ni Kristo.

< Acts 18 >