< 1 Timothy 2 >

1 First of all, then, I ask that petitions, prayers, intercessions, and thanksgivings should be offered for everyone,
Awali ya yote, nasihi kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote:
2 especially for kings and all who are in high positions, in order that we may lead a quiet and peaceful life in a deeply religious and reverent spirit.
kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa amani na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu.
3 This will be good and acceptable in the eyes of God, our Saviour,
Jambo hili ni jema, tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu,
4 whose will is that everyone should be saved, and attain to a full knowledge of the truth.
anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.
5 There is but one God, and one mediator between God and humanity – the human, Christ Jesus,
Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu,
6 who gave himself as a ransom on behalf of all. This must be our testimony, as opportunities present themselves;
aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu wote: jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ufaao.
7 and it was for this that I was myself appointed a herald and an apostle (I am telling the simple truth and no lie) – a teacher of the Gentiles in the faith and truth.
Nami kwa kusudi hili nimewekwa niwe mhubiri na mtume (nasema kweli katika Kristo wala sisemi uongo), mwalimu wa watu wa Mataifa katika imani na kweli.
8 My desire, then, is that it should be the custom everywhere for the men to lead the prayers, with hands reverently uplifted, avoiding heated controversy.
Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira wala kugombana.
9 I also desire that women should adorn themselves with appropriate dress, worn quietly and modestly, and not with wreaths or gold ornaments for the hair, or pearls, or costly clothing,
Vivyo hivyo nataka wanawake wajipambe kwa adabu na kwa heshima katika mavazi yanayostahili, si kwa kusuka nywele, kuvalia dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10 but – as is proper for women who profess to be religious – with good actions.
bali kwa matendo mazuri kama iwapasavyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu.
11 They must learn, listening quietly to their teachers and showing them all deference.
Mwanamke na ajifunze kwa utulivu na kwa utiifu wote.
12 I do not consent to them becoming teachers, or exercising authority over men; they ought to not make a fuss.
Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume. Mwanamke inampasa kukaa kimya.
13 Adam was formed first, not Eve.
Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
14 And it was not Adam who was deceived; it was the woman who was entirely deceived and fell into sin.
Wala si Adamu aliyedanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa akawa mkosaji.
15 But she will be saved by the birth of a child, if they never abandon faith, love, or holiness, and behave with modesty.
Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.

< 1 Timothy 2 >