< 1 Corinthians 8 >

1 With reference to food that has been offered in sacrifice to idols – We are aware that all of us have knowledge! Knowledge breeds conceit, while love builds up character.
Yahusu sasa vyakula vilivyotambikiwa sanamu: Tunajua kwamba sisi sote tuna ujuzi, lakini ujuzi huo huwafanya watu wawe na majivuno; lakini mapendo hujenga.
2 If someone thinks that they know anything, they have not yet reached that knowledge which they ought to have reached.
Anayefikiri kwamba anajua kitu, kwa kweli hajui chochote kama inavyompasa.
3 On the other hand, if a person loves God, they are known by God.
Lakini anayempenda Mungu huyo anajulikana naye.
4 With reference, then, to eating food that has been offered to idols – we are aware that an idol is nothing in the world, and that there is no God but one.
Kwa hiyo, kuhusu vyakula vilivyotambikiwa sanamu, twajua kwamba sanamu si kitu duniani; twajua kwamba Mungu ni mmoja tu.
5 Even supposing that there are so-called “gods” either in heaven or on earth – and there are many such “gods” and “lords” –
Hata kama viko vitu viitwavyo miungu duniani au mbinguni, na hata kama wako miungu na mabwana wengi,
6 Yet for us there is only one God, the Father, from whom all things come (and for him we live), and one Lord, Jesus Christ, through whom all things come (and through him we live).
hata hivyo, kwetu sisi yuko Mungu mmoja tu: Baba, Muumba wa vyote, ambaye kwa ajili yake sisi tuko. Pia yuko Bwana mmoja tu, Yesu Kristo, ambaye kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, na sisi twaishi kwa njia yake.
7 Still, it is not everyone that has this knowledge. Some people, because of their association with idols, continued down to the present time, eat the food as food offered to an idol; and their consciences, while still weak, are dulled.
Lakini, si kila mtu anao ujuzi huu. Maana wako watu wengine waliokwisha zoea sanamu, watu ambao mpaka hivi sasa wanapokula vyakula huviona bado kama vyakula vilivyotambikiwa sanamu. Na kwa vile dhamiri zao ni dhaifu, hutiwa unajisi.
8 What we eat, however, will not bring us nearer to God. We lose nothing by not eating this food, and we gain nothing by eating it.
Lakini chakula hakiwezi kutupeleka karibu zaidi na Mungu. Tukiacha kukila hatupungukiwi kitu, tukikila hatuongezewi kitu.
9 But take care that this right of yours does not become in any way a stumbling-block to the weak.
Lakini, jihadharini: huu uhuru wenu usiwafanye walio na imani dhaifu waanguke katika dhambi.
10 For if someone should see you who possess this knowledge, feasting in an idol’s temple, will not their conscience, if they are weak, become so hardened that they, too, will eat food offered to idols?
Maana, mtu ambaye dhamiri yake ni dhaifu, akikuona wewe mwenye ujuzi unakula vyakula hivyo ndani ya hekalu la sanamu, je, hatatiwa moyo wa kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu?
11 And so, through this knowledge of yours, the weak person is ruined – someone for whose sake Christ died!
Hivyo, huyo ndugu yako dhaifu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake, atapotea kwa sababu ya ujuzi wako.
12 In this way, by sinning against your fellow followers of the Lord and injuring their consciences, while still weak, you sin against Christ.
Kama mkiwakosesha ndugu zenu jinsi hiyo na kuzijeruhi dhamiri zao dhaifu, mtakuwa mmemkosea Kristo.
13 Therefore, if what I eat makes a follower of the Lord fall, rather than make them fall, I will never eat meat again. (aiōn g165)
Kwa hiyo, ikiwa chakula husababisha kuanguka kwa ndugu yangu, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi. (aiōn g165)

< 1 Corinthians 8 >