< Luke 4 >

1 Yeshua [Salvation], full of Ruach haKodesh [Spirit of the Holiness], teshuvah ·completely returned· from the Jordan [Descender], and was led by haRuach [the Spirit] into the wilderness
Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani. Akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi nyikani,
2 for forty days, being tempted by the devil. He ate nothing in those days. Afterward, when they were completed, he was hungry.
mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula chochote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.
3 The devil said to him, “If you are the Ben-Elohim ·Son of Elohim God·, command this stone to become bread.”
Ibilisi akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
4 Yeshua [Salvation] answered him, saying, “It is written, ‘Man shall not live by bread alone, but by every d'var Elohim ·word of God·.’”
Yesu akajibu akamwambia, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu.’”
5 The devil, leading him up on a high mountain, showed him all the kingdoms of the world in a moment of time.
Ibilisi akampeleka hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia kwa mara moja.
6 The devil said to him, “I will give you all this authority, and their glory, for it has been delivered to me; and I give it to whomever I want.
Akamwambia, “Nitakupa mamlaka juu ya milki hizi na fahari zake zote, kwa maana zimekabidhiwa mkononi mwangu nami ninaweza kumpa yeyote ninayetaka.
7 If you therefore will worship before me, it will all be yours.”
Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”
8 Yeshua [Salvation] answered him, “Get behind me Satan [Adversary]! For it is written, ‘You shall worship MarYah [Master Yahweh] your God, and you shall serve him only.’”
Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’”
9 He led him to Jerusalem [City of peace], and set him on the pinnacle of the temple, and said to him, “If you are the Ben-Elohim ·Son of Elohim God·, cast yourself down from here,
Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,
10 for it is written, ‘He will enjoin his angels concerning you, to guard you;’
kwa maana imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake ili wakulinde;
11 and, ‘On their hands they will bear you up, lest perhaps you dash your foot against a stone.’”
nao watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
12 Yeshua [Salvation] answering, said to him, “It has been said, ‘You shall not tempt Yahweh your God.’”
Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
13 When the devil had completed every temptation, he departed from him until another time.
Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.
14 Yeshua [Salvation] teshuvah ·completely returned· in the power of haRuach [the Spirit] into Galilee [District, Circuit], and news about him spread through all the surrounding area.
Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
15 He taught in their synagogues, being glorified by all.
Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.
16 He came to Nazareth [Branch, Separated one], where he had been brought up. He entered, as was his custom, into the synagogue on the Sabbath ·To cease· day, and stood up to read.
Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
17 The book of the prophet Isaiah [Salvation of Yah] was handed to him. He opened the book, and found the place where it was written,
naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
18 “The Ruach of MarYah [Spirit of Master Yahweh] is on me, because he has anointed me to preach good news to the poor. He has sent me to heal the broken hearted, to proclaim release to the captives, recovering of sight to the blind, to deliver those who are crushed,
“Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
19 and to proclaim the acceptable year of MarYah [Master Yahweh].”
na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
20 He closed the book, gave it back to the attendant, and sat down. The eyes of all in the synagogue were fastened on him.
Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
21 He began to tell them, “Today, this Scripture has been fulfilled in your hearing.”
Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”
22 All testified about him, and wondered at the gracious words which proceeded out of his mouth, and they said, “Is not this Joseph [May he add]’s son?”
Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
23 He said to them, “Doubtless you will tell me this parable, ‘Physician, heal yourself! Whatever we have heard done at Capernaum [Village-Comfort, Village-Compassion], do also here in your hometown.’”
Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’”
24 He said, “Most certainly I tell you, no prophet is acceptable in his hometown.
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe.
25 But truly I tell you, there were many widows in Israel [God prevails] in the days of Elijah [My God Yah], when the sky was shut up three years and six months, when a great famine came over all the land.
Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.
26 Elijah [My God Yah] was sent to none of them, except to Zarephath, in the land of Sidon, to a woman who was a widow.
Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
27 There were many people with tzara'at in Israel [God prevails] in the time of Elisha [My God salvation] the prophet, yet not one of them was cleansed, except Naaman, the Syrian.”
Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”
28 They were all filled with wrath in the synagogue, as they heard these things.
Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana.
29 They rose up, threw him out of the city, and led him to the brow of the hill that their city was built on, that they might throw him off the cliff.
Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali.
30 But he, passing through the middle of them, went his way.
Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.
31 He came down to Capernaum [Village-Comfort, Village-Compassion], a city of Galilee [District, Circuit]. He was teaching them on the Sabbath ·To cease· day,
Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha.
32 and they were astonished at his teaching, for his word was with authority.
Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka.
33 In the synagogue there was a man who had a spirit of an unclean demon, and he cried out with a loud voice,
Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu. Naye akapiga kelele kwa nguvu akisema,
34 saying, “Ah! what have we to do with you, Yeshua [Salvation] of Nazareth [Branch, Separated one]? Have you come to destroy us? I know you who you are: haKadosh Elohim [the Holy One of God]!”
“Tuache! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
35 Yeshua [Salvation] rebuked him, saying, “Be silent, and come out of him!” When the demon had thrown him down in the middle of them, he came out of him, having done him no harm.
Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha yule mtu chini mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru.
36 Amazement came on all, and they spoke together, one with another, saying, “What is this word? For with authority and power he commands the unclean spirits, and they come out!”
Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!”
37 News about him went out into every place of the surrounding region.
Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.
38 He rose up from the synagogue, and entered into Simeon [Hearing]’s house. Simeon [Hearing]’s mother-in-law was afflicted with a great fever, and they begged him for her.
Yesu akatoka katika sinagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mama mkwe wa Simoni akiwa ameshikwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie.
39 He stood over her, and rebuked the fever; and it left her. Immediately she rose up and served them.
Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile, naye akaanza kuwahudumia.
40 When the sun was setting, all those who had any sick with various diseases brought them to him; and he laid his hands on every one of them, and healed them.
Jua lilipokuwa linatua, watu wakamletea Yesu watu wote waliokuwa na maradhi mbalimbali, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, naye akawaponya.
41 Demons also came out of many, crying out, and saying, “You are the Messiah [Anointed one], the Ben-Elohim ·Son of Elohim God·!” Rebuking them, he didn’t allow them to speak, because they knew that he was the Messiah [Anointed one].
Pepo wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.
42 When it was day, he departed and went into an uninhabited place, and the multitudes looked for him, and came to him, and held on to him, so that he would not go away from them.
Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke.
43 But he said to them, “I must preach the good news of God’s Kingdom to the other cities also. For this reason I have been sent.”
Lakini yeye akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.”
44 He was preaching in the synagogues of Galilee [District, Circuit].
Naye aliendelea kuhubiri katika masinagogi ya Uyahudi.

< Luke 4 >